Kama ni kweli na ushahidi upo....

Kama ni kweli na ushahidi upo....

Mm naamini nyie mnatoa cotations kuwa mchungaji kasema, wewe unamwamini kiasi gani? Yeye ni binadamu kama sisi, Mimi naunga mkono akae kimya kafanya kazi kubwa mnoo ya kuokoa maisha ya vijana, mtakaa kimya na ataendelea kusafisha jiji
 
Kama, kama ni Mtanzania kama mimi basi anahusika.
Haujajibu swali mkuu, wewe unao ushahidi kuwa.Makonda amefoji cheti?

Labda niulize hivi, kwa kuwa umesema Makonda amefoji cheti, tukikupeleka mahakamani utoe ushahidi wa kufoji kwake cheti utautoa??? Usiseme 'fulani' kasema, kwa kuwa hapa tunaongelea cheti, tunataka hicho cheti kilichofojiwa na orijinal tukione, je, unaweza ukatupatia?
 
Mchungaji ni yule anaye chunga kondoo wake wasipotee sio yule sio yule akiona jambo kwenye magazeti au kwenye mitandao ya kijamii ndio yanakua mahubiri yake.inshu ni madawa ya kulevya sio vyeti vya MTU .tuache kupotosha.

Sent from my itel_it1502 using JamiiForums mobile app
 
Sina cheti. Labda niulize, nini maana ya mawasiliano kuwepo. Halafu cheti ni kimoja tu, hakiwezi kuwa Dar alafu kikawa Mtwara kwa wakati huo huo.
 
Kesi ya jinai inaendeshwa na serikali na sio mtu binafsi.

Mwenye wajibu wa kuchunguza na kumpeleka huyo jamaa mahakamani ni serikali.
It's, however, not a hard and fast rule. Mtu binafsi anaweza kufungua kesi ya jinai.
 
Sina cheti. Labda niulize, nini maana ya mawasiliano kuwepo. Halafu cheti ni kimoja tu, hakiwezi kuwa Dar alafu kikawa Mtwara kwa wakati huo huo.
Kwa hiyo hauna uhakika kama kweli cheti kipo, kama kina ziro au laa, kama kipo kimoja au laa, na wala haujakiona?

Unao uhakika gani kama kweli cheti hicho kimefojiwa au original?

Ushahidi pekee ni 'fulani kasema' hivi unauhakika gani na huyo fulani kama anachosema ni kweli? Kwa nini yeye asikionyeshe hicho cheti?

Chadema wamekaa miaka 8 wanamsema Lowasa ni fisadi, lakini 2015 ndio akawa mgombea wao huku wakitumia nguvu kubwa kusema sio fisadi, simply kwa kuwa waliposema fisadi hawakutupa ushahidi, ndio maana wakakimbilia kusema kuwa mwenye ushahidi kuwa ni fisadi aende mahakaamani kwa kuwa wanajua walimuwa wanacheza mchezo wa siasa tu kuchafuana.

Hivi Lowasa alishatoka na kujibu tuhuma za upinzani kuwa yeye ni fisadi? Si alikaa kimya? Maana qewe ukisema mimi ni mwizi, wewe ndionunatakiwa uthibitishe uizi wangu. Kwa nini sasa mnamtaka Makonda aje ajibu tuhuma ambazo mmezipika wenyewe kwa kisa cha kumchafulia jina?
 
Mkuu Nyani Ngabu,mfumo wa kisheria wa nchi yetu ya Tanzania hauruhusu mtu binafsi kumfungulia mwingine,na kuendesha kesi mahakamani,kesi ya jinai. Kinachotakiwa ni kwa mtu mwenye ushahidi dhidi ya jinai ya mwingine kuuwasilisha ushahidi huo kwa mamlaka zinazohusika,mfano polisi au TAKUKURU,ili hatua stahiki zichukukiwe. Mamlaka hizo na nyinginezo,kama Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ndizo zitakazomshtaki mhusika. Ndiyo kusema,wenye kuamua kushtaki au la ni watawala waliopo kwenye mamlaka hizo iwe ushahidi umekabidhiwa au ule walionao wenyewe.
Lakini nani kawasilisha hata kwenye mahakama ya umma tunayoisema yaani humu kwenye social media ama hata tradional media kwa maana magazeti na TV ama kwenye "familia" kama ya Gwajima si angetoa photocopy za kutosha na kusambaza? Sasa kote nahangaika naona maneno matupu kama anavyosema Mkuu Nyani Ngabu

Sent from my SM-N920C using JamiiForums mobile app
 
He/she who alleges must prove.

Allegations don't just prove themselves.

So did I miss the memo or something?
Jamani kama kila kiongozi ama kila raia akutuhumiwa anatakiwa ajitete yeye itakua zogo maana mnataka kuhalalisha hata makosa yao waliyoyafanya kuwatuhumu watu hadharani kwa serious offences na nyie munarudia tena bila kuwa na ushahidi wowote halafu mtuhumiwa ndio atoe ushahidi. Kesho mtawatuhumu watu ni mashoga mtataka watoe ushahidi gani kuwa wao si mashoga? Maana juzijuzi Naibu Waziri alitaka kutoa list

Sent from my SM-N920C using JamiiForums mobile app
 
Pia mm nimekuerewa mtoa madaa lakn?mm pia elimu yangu cyo kubwa Nilitaman sn kuona wasomi hususani wanale wana shelia,wakilizungumuzia ?Kama wana ushahidi kwann asipelekwe mahakaman ?Kwann wana toa tu maneno mm naomba wana shelia ebu tusaidie kwa hilo.?
 
Watetezi wa Makonda naona mnavyozidi kujitokeza...walianza washikaji, wakaja wenzi, wakaja marafiki na sasa ndugu nao wameamua kujitokeza, hawataki kubaki nyuma. Ninao ushauri mzuri kwenu wote mliotajwa hapo juu, kama kweli mna nia thabiti ya kumsaidia, kwamba mtakuwa mmemtendea haki isiyo na kifani kama mtampa ushauri huu.

Akusanye vyeti vyake vyote aende navyo kwa Waziri Ndalichako vithibitishwe halafu awaite waandishi wa habari kuwapa tahadhari wote waliovalia njuga swala la elimu yake kwamba kuanzia sasa jina Daudi Bashite limepigwa marufuku kutajwa na kuwaagiza polisi wakiongozwa na kamanda Sirro kumshughulikia bila huruma yeyote atakayekaidi.

Pamoja na umri wako unayumbishwa na maneno ya Gwajima na Mange! Ama kweli chadema mmefubazwa! Hatred won't do you any good old man!
 
Come on now, what's in a name? If Paul could be Daudi and Makonda could be Bashite, why do we need names when the picture says it all? Remember a picture is worth a thousand words and a drawing shows at one glance what might be spread over ten pages in a book

Mnaanza hdi kubishana na wazazi (supposing what is alleged is true). You are getting even more ridiculous. It's high time you acted and came of age.
 
Believe me, kumiliki cheti feki kunapunguza kujiamini sehemu yeyote ya kazi hata kama una cheo gani.

Confidence alivyokuwa nayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda aka Bashite, imeanza kupungua tangu kuibuliwa kwa sakata la yeye kumiliki vyeti feki.

Ni ajabu sana operation muhimu kama hili ya kupiga marufuku matumizi ya viroba kuanza bila kusikia tamko lolote kutoka kwa mwenye mkoa wake.

Awali alikuwa mstari wa mbele kuandaa press conference kutoa matamko kwa mambo mengine yasiyokuwa na maana kama, kutolala gesti mchana, kupaka rangi nyumba zote mkoani kwake, kuorodhesha wageni wanaoingia Dar, ila kwa hili lililo na uzito karibu sawa na madawa ya kulevya yuko kimya kigugumizi hiki kimeanza lini, tatizo cheti, pole sana Bashite.

Nimeamini kweli dunia duara, enzi zile wewe ndio ulikuwa ukiwaita waandishi wa habari, leo waandishi wanakuita wewe lakini hutokei.

Conclusion:
Kuwa na vyeti halisi raha sana (CONFIDENCE).

Kipimio cha confidence ni kipi?
 
Kwa hiyo mimi nikija hapo ulipo na kukutwanga ngumi kwenye chembe huwezi kwenda mahakamani kunifungulia mashitaka ya kukushambulia?
Hapo ss yani nilikuwa nataka nikamtwange makofi jamma mmoja hiv namdai hela hapa jirani nikifikiri hawezi kushtaki mpaka serikali iamuee
 
Mnaanza hdi kubishana na wazazi (supposing what is alleged is true). You are getting even more ridiculous. It's high time you acted and came of age.
Amini usiamini vilaza wa kutupwa nchini Tanzania waliweza kuungaunga elimu hadi wengine wao wakaukwaa uprofessa. Hebu fikiria mtu aliyepata sufuri darasa la saba, akapata sufuri darasa la kumi na mbili, akapata mwanya wa kutoka nje ya Tanzania na baada ya miaka kumi anarudi akiwa ni profesa na kuanza kufundisha chuo kikuu! Huu ni mfano moja tu kati ya mengi tu na kuficha na kukwepa fedheha inayoweza kuwapata wanakimbilia siasa...na wako wengi!

Yeyote anayemtetea Makonda namweka kwenye kundi hili...wanajishuku yanaweza yakawapata yanayompata Bashite hivyo lazima watafute namna ya kujihami. Ukipitia JF utakuta mada inayowasema madaktari wetu feki waliojaa kwenye taasisi mbalimbali. Mimi huyo Mange unayemsema hata simjui wala sisomi habari zake, nasikia tu akitajwa humu. Je na wewe Ibambasi uko kundini? Mkuki kachomwa Tomaso, mbona damu unavuja wewe?
 
Back
Top Bottom