Watetezi wa Makonda naona mnavyozidi kujitokeza...walianza washikaji, wakaja wenzi, wakaja marafiki na sasa ndugu nao wameamua kujitokeza, hawataki kubaki nyuma. Ninao ushauri mzuri kwenu wote mliotajwa hapo juu, kama kweli mna nia thabiti ya kumsaidia, kwamba mtakuwa mmemtendea haki isiyo na kifani kama mtampa ushauri huu.
Akusanye vyeti vyake vyote aende navyo kwa Waziri Ndalichako vithibitishwe halafu awaite waandishi wa habari kuwapa tahadhari wote waliovalia njuga swala la elimu yake kwamba kuanzia sasa jina Daudi Bashite limepigwa marufuku kutajwa na kuwaagiza polisi wakiongozwa na kamanda Sirro kumshughulikia bila huruma yeyote atakayekaidi.