Kama natoka na mumeo...

Kama natoka na mumeo...

Nimesikia kajukuu. Namsubiria anipruvie kuwa hazinitoshi. Otherwise nitaprove otherwise.

Samahani kaka zinakutosha sana, ulimi uliniteleza. Lakini napenda ujue kuwa sikuhitaji wewe wala bwana mwingine, ninaye huyu ananitosha upo hapo? Na usitegemee eti atanitema nije kwako, hilo halitatokea ng'o. Kwanza sina shida na mwanaume wa alimradi anavaa suruali au ana pesa, no. Kama suruali hata mie navaa na pesa ninazo za kunitosha, sihitaji buzi. Penzi ninalohitaji ndilo huyu bwana ananipatia nami namkidhi vilivyo, watu wazima tunajilia vyetu kwa raha zetu, wa kununa wakinuna hainihusu. Anayechunguza achunguze, akichoka ataacha. Mwanamke mzima na elimu tele midigrii kibao hadi ya ulaya anahangaika hadi kumnyang'anya mume wake simu eti akae nayo aone wanaompigia, kang'ang'ania simu ya mtu miezi 3 anaenda nayo ofisini anarudi nayo kaambulia patupu, vya kuliwa vimeendelea kuliwa. Kama hulipi hulipi tu, halohaloooo msitake ncheke mie.
 
kweli hapa kuna mtu anatafutwa tena yupo JF kwakweli naomba ajitambue kuwa anapewa mambo
 
Samahani kaka zinakutosha sana, ulimi uliniteleza. Lakini napenda ujue kuwa sikuhitaji wewe wala bwana mwingine, ninaye huyu ananitosha upo hapo? Na usitegemee eti atanitema nije kwako, hilo halitatokea ng'o. Kwanza sina shida na mwanaume wa alimradi anavaa suruali au ana pesa, no. Kama suruali hata mie navaa na pesa ninazo za kunitosha, sihitaji buzi. Penzi ninalohitaji ndilo huyu bwana ananipatia nami namkidhi vilivyo, watu wazima tunajilia vyetu kwa raha zetu, wa kununa wakinuna hainihusu. Anayechunguza achunguze, akichoka ataacha. Mwanamke mzima na elimu tele midigrii kibao hadi ya ulaya anahangaika hadi kumnyang'anya mume wake simu eti akae nayo aone wanaompigia, kang'ang'ania simu ya mtu miezi 3 anaenda nayo ofisini anarudi nayo kaambulia patupu, vya kuliwa vimeendelea kuliwa. Kama hulipi hulipi tu, halohaloooo msitake ncheke mie.

Da Sophy nimepata picha halisi sasa!!

unayemwibia mume wake amekupata!!!
 
Kutoka na mume wa mtu ni utovu wa nidhamu, nafikiri kuna vijana wengi tu wako wanakuhitaji kwa nini ujipe karaha na lawama zisizo za msingi? Ni ushauri na siyo lazima uuchukue: imagine wewe unachukua mume wa mtu kesho unaolewa wenzio wanachukua utajisikiaje?

nafikiri siyo kitendo kizuri kutembea naa wanaume wa wenzenu.

Hayo ni mawazo yako, labda hujawahi kupendwa au kupenda.
 
mwenye ma degree ya ulaya kisha halipi .....plz stand up! hahaha kazi kweli kweli

ukisikia mtu kudanganywa akadanganyika ndo huyu da sophy
 
Na si ajabu ndo mapya yaani hata miezi kadhaa hayana so ni ile novelity hali ya upya wa mapenzi ndo unampa wendawazimu. Ngoja jamaa akinai atafute makazi mapya. Atajibeba

Mapya kakwambia nani? Niko nae sambamba, mbanano kwa kwenda mbele hakai kando mtu hapa, kama vipi akiona msongamano atasepa yeye anayejifanya FBI. Na sijataka tu mtoto saa hizi angekuwa anaenda shule, upo shosti?
 
da sophy ni kimada mzoefu!

yaani kwa nini usianzishe pertition ya vimada wote ya kupewa cheo chenu stahili mnapojitambulisha rasmi kama kwenye mikutano au kwenye passport!
 
with a mentality like this kisha useme unajiheshimu?! hujiheshimu my dear .................mwenye kijiheshimu hawezi kumvunjia heshima mwenziwe kwa maneno ya kifedhuli ya namna hii hata siku moja

Kayataka mwenyewe aliyeanza kuita wenzie mapozeo. Jino kwa jino ati!
 
Kwa hiyo wewe watimiziwa chumbani kwa mke mwenzio? Kweli unajiheshimu dada yangu.
Nikwambie siri
Huyo mke mwenzio siku akiamua kumchanganya mumeo kwa mahaba wewe pasi yako ni rahisi kufutika maana imeandikwa kwa penseli. na kwa maana hiyo anakuja kwako kupoza mapungufu anayoyapata kwa mkewe au kwenye familia yake. ukubali usikubali MAPOZEO ni wewe na wewe utabaki MAPOZEO na vile vile ukishachuja litatafutwa POZEO lingine au atarudi kwa mkewe. Hakunaga nyumba ndogo ya daima bibie!!

Thubutuuu! Si ampe basi kama anacho cha kumpa.
 
jamani jamani ...................da sophy unacheza na hatari. unajua kuwa mtu akikudhuru anaweza kuepuka kufungwa kisa mapenzi? usijesema hujaambiwa.

am out of here ...........
 
Tatizo lako ni kutotaka kuelewa, ushaambiwa siti zimejaa we wang'ang'ana kuingia kwanini usitafute usafiri mwingine na haraka huna? Tafuta wako ufunge nae ndoa na utulie naye!

Tunabanana humohumo, atakayeona shida kusongamana atashuka tutakalia siti kama kawa ikibidi na safari inaendelea
 
Wadada wa dizaini hii wanao penda kudandia waume za watu, huwa hawaolewi inakuwa kama gundu vile,
Si kaonja hata mseme vp kesha ona raha ya mme wa mtu hapo usikute kaaidiwa mkoko au mjengo.

Aniahidi mkoko na mjengo wa kazi gani. Nina nyumba yangu na gari zangu mwenyewe. Kama mnawaza mambo ya kuchuna buzi mie simo humo nina biashara zangu za maana. Na anakuja nyumbani kwangu kama kwake, ndio maana anayetaka kuchunguza na kuvizia fumanizi analialia tu, huwezi kuvamia nyumbani kwangu full geti na ulinzi, namuingiza na kumtoa kwa gari yangu sina shida na pesa ya mtu.
 
hadi ule mtandao una mpa?? maana nasikia ndo hasa wanachofata huko kwenu......

Ndio mawazo yenu potofu hayo. Wewe kama unampa mumeo tiGo mpe kivyako, lakini kama ni wa kutoka atatoka kufuata mapenzi ya kiukweli na kwako atakuwa anarudi kufuata ufirauni wa tiGo tu. Utaja..!
 
Back
Top Bottom