Naomba kusema machache ingawa baadhi yenu mtanishangaa. Mimi mume wangu anatoka nje ya ndoa na tena anayetoka nae ni mtu aliyekuwa rafiki yake kabla yangu. mara ya kwanza kufahamu iliniuma sana. Lakini nikasema nitamuomba Mungu tu hadi hii tabia itaisha. Nilikuja kupata wazo hebu nijitafakari na mimi ni wapi nimekosea hadi nisiweze kuwa wake peke yake hadi anitafutie mwingine. niligundua machache nikarekebisha ukweli ni kwamba hata siku moja upendo kwa nyumba yangu na mume wangu haujapungua wala sijawahi kulalamika kukosa haki yangu hakuna jambo naweza lalamika kwake au kwenda kwa washenga au kanisani. ukweli sijawahi kumuuliza nilitumiwa msg najua ni na shoga yangu na nilihakikisha lakini sijamuambia mzee wala shoga yangu kuhusu hayo niliyoyaona ila niliamua kutafuta mikakati yangu ya kuhakikisha haki yangu, heshima yangu ipo pale pale.
ukweli najua bado yupo na huyo hawara yake, wanayoridhishana siyajui na wala sitaki kuyajua ila mimi na yeye, kila sekunde nahakikisha wajibu wangu uliondani ya uwezo wangu ninautimiza juu yake sitaki kuwa mtumwa na sasa ndoa yangu ina miaka 14.
kwa upande wangu nadhani hawa wanaume tukiacha tabia ya kuwauliza uliza kuhusu mahusiano ya nje hata kama tumeyaona watatulia na mmoja na suala la ugonjwa wa ukimwi na mengine mtakuwa mnakumbushana mara kwa mara, Mungu yupo pamoja nasi tuzidi kuomba kwani mengi yapo juu ya uwezo wetu ila kwa yeye yote yawezekana. Kuweni huru mtunze watoto wenu achane malumbano. .