BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Nani kakuambia tunashea? Yule anayemwita mkewe kwani anafanya nini zaidi ya kumfulia nguo na kumtandikia kitanda mwenzie apumzike baada ya kunitimizia mpenzie wajibu. Ni kwamba pale anakwenda kulala tu, na siku mojamoja kupozea ile kidogo ya kutunzia nyumba, mwanamke mwenyewe hovyo, ni kwamba tu ndoa za kikristo zina kasoro hiyo huwezi kumwacha lakini pale ni hana mke.
Unaulizia kutongoza wengine, ataanzia wapi? Alivyoshikwa uzuri anajua mwenyewe, hafurukuti hata chembe. Hivi unajua kuna siku huwa nafanya kabisa bidii kumfukuza aende kwa mkewe maana sasa keshakuwa kama zuzu, analia kama mtoto kujutia alivyovaa mkenge wa huyo asiyejua maana ya kuolewa.
Eh! hahahahahahahahaha we kiboko!!!! unampa nini mpaka umemshika vizuri kiasi hicho?...LOL! kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa