Kama kuvaa nusu uchi ni kinyume na maadili ya Kitanzania mbona wamasai wanavaa lakini hawakamatwi?

Jensen salamone

JF-Expert Member
Sep 28, 2019
320
639
Awali kabla ya ujio wa wazungu Waafrika hatukuwahi kujua kitu kinachoitwa nguo. Na haya mavazi tunayovaa kufunika mwili mzima ni utamaduni tumeiga toka kwa wazungu.

Sisi Waafrika mavazi yetu makuu yalikuwa ni magome ya miti, majani na ngozi za wanyama tena katika uvaaji tulikuwa tunastiri sehemu nyeti tu huku sehemu kubwa ya mwili ikibaki wazi(uchi).

Hivyo mamlaka zinapowachukulia hatua wanaovaa nusu uchi kwa madai kwamba wanakiuka maadili ya Kitanzania ni ukatili na uonevu.

Ukweli ni kwamba wote wanaovaa nusu uchi wana enzi utamaduni wa Kiafrika kwa vitendo ndio maana Wamasai na Wahadzabe wameendelea kuenzi utamaduni huo.

Kwahiyo ikiwa mamlaka zinazohusika na maadili zinaona kuvaa nusu uchi ni kinyume na maadili ya kitanzania, tunaziomba zianze kwa kuwakamata Wamasai wanaozunguka mitaani wakiwa wamevaa lubega huku wakiacha vimapaja nje na sio kuonea akina Amber Lulu, Gigy na mastaa wengine ambao kimsingi wana enzi utamaduni wa Mwafrika kwa vitendo.
 
Ukisikia wanasema "hayo si maadili ya mtanzania au hiki nikinyume cha maadili yetu" unaweza dhani tulikuwaga malaika.

Ukifuatilia a vizuri utakuta maadili yetu ilikuwa ni kuacha maziwa nje. Hata leo wamama hawaogopi kutoa maziwa na kunyonyesha watoto hadharani, maziwa siyo uchi kwetu. Maadili yetu ilikuwa ni kuacha mapaja nje na kucheza erotic dances. Au nasema uongo ndugu zangu?

Leo ukifanya hayo utaambiwa siyo maadili yetu.
 
Awali kabla ya ujio wa wazungu waafrika hatukuwahi kujua kitu kinachoitwa nguo. Na haya mavazi tunayovaa kufunika mwili mzima ni utamaduni tumeiga toka kwa wazungu..

kwahiyo ikiwa mamlaka zinazohusika na maadili zinaona kuvaa nusu uchi ni kinyume na maadili ya kitanzania, tunaziomba zianze kwa kuwakamata wamasai wanaozunguka mitaani wakiwa wamevaa lubega huku wakiacha vimapaja nje na sio kuonea
Pumba ya kufungia mwaka 2020
 
Ukisikia wanasema "hayo si maadili ya mtanzania au hiki nikinyume cha maadili yetu" unaweza dhani tulikuwaga malaika.

Ukifuatilia a vizuri utakuta maadili yetu ilikuwa ni kuacha maziwa nje. Hata leo wamama hawaogopi kutoa maziwa na kunyonyesha watoto hadharani, maziwa siyo uchi kwetu. Maadili yetu ilikuwa ni kuacha mapaja nje na kucheza erotic dances.
Au nasema uongo ndugu zangu?

Leo ukifanya hayo utaambiwa siyo maadili yetu.

Hujadanganya ndugu, siku hizi hadi dada zetu kuvaa shanga imekuwa kinyume na maadili ya mtanzania

Na atakuja mtu kusema hapa shanga zilikuwa zinavaliwa faragha
 
Wala hujakosea Mkuu. Ni hawa mapunguani wanaodai maadili ya Watanzania wakati si kweli.

Ukisikia wanasema "hayo si maadili ya mtanzania au hiki nikinyume cha maadili yetu" unaweza dhani tulikuwaga malaika.


Ukifuatilia a vizuri utakuta maadili yetu ilikuwa ni kuacha maziwa nje. Hata leo wamama hawaogopi kutoa maziwa na kunyonyesha watoto hadharani, maziwa siyo uchi kwetu. Maadili yetu ilikuwa ni kuacha mapaja nje na kucheza erotic dances.
Au nasema uongo ndugu zangu?

Leo ukifanya hayo utaambiwa siyo maadili yetu.
 
Kwahiyo ni kama unataka tusiwe na Maadili yetu sio?

Kama unataka tuwe nayo ndio hayo yaliyokwisha wekwa na hayawezi kubadirishwa kwa hizo hoja nyepesi za Kimasai.

Na hakuna sehem iliyokosa maadili yake.
 
Awali kabla ya ujio wa wazungu waafrika hatukuwahi kujua kitu kinachoitwa nguo. Na haya mavazi tunayovaa kufunika mwili mzima ni utamaduni tumeiga toka kwa wazungu..

Sisi waafrika mavazi yetu makuu yalikuwa ni magome ya miti, majani na ngozi za wanyama tena katika uvaaji tulikuwa tunastiri sehemu nyeti tu huku sehemu kubwa ya mwili ikibaki wazi(uchi)...

hivyo mamlaka zinapowachukulia hatua wanaovaa nusu uchi kwa madai kwamba wanakiuka maadili ya kitanzania ni ukatili na uonevu..

ukweli ni kwamba wote wanaovaa nusu uchi wana enzi utamaduni wa kiafrika kwa vitendo ndio maana wamasai na wahadzabe wameendelea kuenzi utamaduni huo..

kwahiyo ikiwa mamlaka zinazohusika na maadili zinaona kuvaa nusu uchi ni kinyume na maadili ya kitanzania, tunaziomba zianze kwa kuwakamata wamasai wanaozunguka mitaani wakiwa wamevaa lubega huku wakiacha vimapaja nje na sio kuonea akina amber lulu, gigy na mastaa wengine ambao kimsingi wana enzi utamaduni wa mwafrika kwa vitendo.
Swali lako lina mantiki kubwa sana mkuu.

Kutembea na silaha (sime) hadharani vile vile ni kosa kwa mujibu wa sheria, lakini wamasai wanaruhusiwa kwa maana ni sehemu ya mila na desturi yao na haijawahi kudhiirika popote kama mwenendo huo uliwahi kusababisha uvunjifu wa amani kwa namna yoyote ile.
 
People who have made up their mind to go, will only go anyhow, even though seemingly there is no any means of doing so whatsoever -- but still they will invent one anyway, and go they will go!
 
Kwahiyo ni kama unataka tusiwe na Maadili yetu sio ?

Kama unataka tuwe nayo ndio hayo yaliyokwisha wekwa na hayawezi kubadirishwa kwa hizo hoja nyepesi za kimasai

Na hakuna sehem iliyokosa maadili yake
Maadili yetu ni yapi,yaliorodheshwa wapi,lini Kama taifa tulikubaliana haya ndo maadili yetu.
Vile vile,mavazi yetu ya asili ni yapi ili tujue?
Hua tunadanganyana tu,kinyume Cha maadili,au Kama kwenye katiba yamefafanuliwa,tuelekezane mkuu.
 
...ulishawai kumtamani masai maungo yake kwa kuvaa vile..?
si kwa sababu ameshazoeleka unamuona kawaida tu ila hata mimi binafsi nashangaaga sana kusema eti mtu kavaana uchi tafuten picha za kusin mwa africa mbaka sasa wanavaa kuficha uchi tu kwingine wazi kabisa matiti yapo wazi na ndio utamadun kabisa mbaka sasa
 
vipi kuhusu kuvaa chupi na brazia? mbona kuna ambao hawavai ni kawaida tu.Kuna suala la kuoga mtoni au ziwani nalo ni kawaida tu hakuna wa kushagaa.Ni miaka ya jana tu vijana wa kike na kiume walikuwa hawavai nguo hasa huko machungoni na hakuna kutamaniana wala kushangaana.

Miaka michache iliyopita ilikuwa si ajabu kuona wanafunzi wamevaa lubega sare nyeupe shuleni huku miguuni wako peku hawana viatu.

Suala la kuvaa nguo ni mtindo tu au ni kujisitiri na baridi kama mwili haujazoea hali ya hewa ya mahali hapo.Jamii nzima ikiamua kutembea uchu haitakuwa ajabu,itakuwa kawaida tu,sasa kama mtoto anazaliwa anakuta wazazi wake wako kama walivyozaliwa atashangaa nini cha ajabu wakati naye yuko hivyo?
 
Back
Top Bottom