SMS01:
"Sipigi simu na wala sijishughulishi na huyo mamako. Hata ukisafiri simpeleki hospital nisingekuwa mimi ungejua kama mama yako ana tatizo hilo. Hilo la mzigo umeona nalo neno la kukasirika, kama mme wake anasema mnao mzigo why me nisiseme. Kama kukasirika kasirika tu".
SMS02:
Mimi nataka kuondoka kwenye nyumba yako. Naomba unipe go ahead.
Kwa ufupi huu ni ujumbe wa SMS ulioandikwa na mke kwenda kwa mume wake wa ndoa baada ya kutokea kutoelewana juu ya uwepo wa mama ya mume (yaani mamamkwe) nyumbani kwao. Ulifuatana kwa tofauti ya takribani wiki moja.
Mama mkwe huyo ni mtu mzima mwenye umri wa zaidi ya miaka sabini na ni mgonjwa ambaye hawezi tena kujitegemea. Hivyo mama huyu anahitaji msaada wa karibu wa watoto wake ili aweze kuishi.
Mke ana mtazamo kuwa mama mkwe wake amekuwa ni mzigo usiobebeka unaohitajika kuondolewa hapo nyumbani wakati ambapo mme anasisitiza kuwa mama yake kamwe hawezi kuwa hawezi kamwe kuwa mzigo kwake. Kimsingi mume anaamini kuwa anawajibika kumtunza mama yake katika hali hiyo mpaka hapo ama atakapopona au vinginevyo. Pia mume hapendi kusikia mama yake akifananishwa na mzigo kwani mama huyu ndiye hasa aliyemlea mme mtu akiwa mdogo baada ya baba yake kuwatelekeza na mama huyu na kuamua kuoa mke mwingine.
Baada ya sintofahamu kutokea mke ameamua kugoma kuongea (na kutoa ile huduma nyingine) na mume wake na kama haitoshi amemtumia ujumbe huu wa SMS akirejea mazungumzo yao ya awali ambayo walishindwa kuelewana. Kuhusu simu mume alimwomba mke wake ampigie daktar anaye ndiye anamtibu mama huyu ili kuweka appointment ya kwenda kumuona.
Ndugu zangu wake kwa waume hebu tushauriane hatua muafaka za kuchukua kutatua changamoto kama hii.
"Sipigi simu na wala sijishughulishi na huyo mamako. Hata ukisafiri simpeleki hospital nisingekuwa mimi ungejua kama mama yako ana tatizo hilo. Hilo la mzigo umeona nalo neno la kukasirika, kama mme wake anasema mnao mzigo why me nisiseme. Kama kukasirika kasirika tu".
SMS02:
Mimi nataka kuondoka kwenye nyumba yako. Naomba unipe go ahead.
Kwa ufupi huu ni ujumbe wa SMS ulioandikwa na mke kwenda kwa mume wake wa ndoa baada ya kutokea kutoelewana juu ya uwepo wa mama ya mume (yaani mamamkwe) nyumbani kwao. Ulifuatana kwa tofauti ya takribani wiki moja.
Mama mkwe huyo ni mtu mzima mwenye umri wa zaidi ya miaka sabini na ni mgonjwa ambaye hawezi tena kujitegemea. Hivyo mama huyu anahitaji msaada wa karibu wa watoto wake ili aweze kuishi.
Mke ana mtazamo kuwa mama mkwe wake amekuwa ni mzigo usiobebeka unaohitajika kuondolewa hapo nyumbani wakati ambapo mme anasisitiza kuwa mama yake kamwe hawezi kuwa hawezi kamwe kuwa mzigo kwake. Kimsingi mume anaamini kuwa anawajibika kumtunza mama yake katika hali hiyo mpaka hapo ama atakapopona au vinginevyo. Pia mume hapendi kusikia mama yake akifananishwa na mzigo kwani mama huyu ndiye hasa aliyemlea mme mtu akiwa mdogo baada ya baba yake kuwatelekeza na mama huyu na kuamua kuoa mke mwingine.
Baada ya sintofahamu kutokea mke ameamua kugoma kuongea (na kutoa ile huduma nyingine) na mume wake na kama haitoshi amemtumia ujumbe huu wa SMS akirejea mazungumzo yao ya awali ambayo walishindwa kuelewana. Kuhusu simu mume alimwomba mke wake ampigie daktar anaye ndiye anamtibu mama huyu ili kuweka appointment ya kwenda kumuona.
Ndugu zangu wake kwa waume hebu tushauriane hatua muafaka za kuchukua kutatua changamoto kama hii.