Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Jamani jibu la hoja hii mbona liko wazi kabisa!Hakika inashangaza sana kuona baadhi ya Viongozi wetu Walioapa Kuilinda Katiba lakini ndio Wanaikanyaga kwa Makusudi tena Hadharani.Kwa Mujibu wa Katiba tuna aina mbili za Wabunge Wakuchaguliwa na Wakuteuliwa.
Na ili uwe Mbunge lazima uwe Mwanachama wa Chama cha Siasa. Moja ya Sababu za kukoma kwa Ubunge ni pamoja na Kufukuzwa Uanachama. Chadema imewafukuza Wabunge 19 Uanachama wao lakini Mpaka leo bado ni Wabunge. Swali la kujiuliza:
Kwanini bado ni Wabunge?
Nani anawalinda?
Kwanini awalinde licha ya kuwa wamemfukuzwa Uanachama?
Tunakuomba Mh. Rais hebu ingilia kati suala hilo kwa Hao Wanaoichezea Katiba na pia Kuokoa Pesa wanazolipwa Wabunge hao ambazo ni Kodi za Wananchi Masikini wa nchi hii.
Anayewalinda Wabunge 19(a.k.a Covid-19) ni Spika Job Ndugai wakti ule akisaidiana na Mwendazake JPM.
Huu ni uvunjaji mkubwa wa KATIBA hii mbovu ya JMT ambayo imejaa viraka vya kukibeba CHAMA TWAWALA CCM!!
Mhe. Rais Samia tunaomba achukue hatua madhubuti za kuwang'oa hawa Covid-19 maana hawamwakilishi yeyote wala chama chochote hawana tija kwa Taifa na wanapoteza fedha za walipa kodi kwa kulipwa WASICHOSTAHILI!