Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,305
- 12,969
Katika hali ya kawaida ungetegemea serikali iwe mfano wa kuigwa kwa kufuata na kutekeleza katiba na sheria. Lakini toka awamu ya tano imeingia na hii iliyopo ya kurithi tunashuhudia uvunjaji na usiginaji mkubwa wa katiba na sheria unaofanywa na watu walioapa kuilinda katiba na kufuata sheria huku wakiwa wameshika vitabu vitakatifu.
Kuzuiwa kwa mikutano, maandamano na shughuli huru za kisiasa ni mfano wa kwanza kabisa alioanza nao wendazake na sasa kurithiwa na mwenza wake.
Suala lawabunge 19 waliofukuzwa uanachama na chama chao lakini wakiwa wanakingiwa kifua na serikali ni mfano wa dhahiri wa uvunjwaji na usiginaji wa katiba na sheria.
Tumeshuhudia huko nyuma vyama ikiwemo CCM na CUF vikifukuza wanachama wao ambao ni wabunge na kwa mujibu wa sheria watu hao walitolewa bungeni wakiwa wamefungua kesi mahakamani au hawajafungua kesi kwakuwa kufungua kesi au kukata rufaa hakubatilishi uamuzi uliotolewa na chama mpaka hapo mahakama itakapoamua vinginevyo.
Kama ingekuwa kukata rufaa kunamuweka aliyehukumiwa huru ilipaswa Sabaya naye aachiwe maratu alipokata rufaa lakini aliendelea kubaki ndani hadi uamuzi ulipopitishwa. Hata CUF ilipowavua uanachama wabunge wake wa viti maalumu waliondokewa bungeni licha yakuwa walifungua kesi mamahakamani. Lakini leo tunashuhudia jinsi spika mwanasheria anavyoshiriki uhalifu dhidi ya katiba na sheria za nchi.
Kuzuiwa kwa mikutano, maandamano na shughuli huru za kisiasa ni mfano wa kwanza kabisa alioanza nao wendazake na sasa kurithiwa na mwenza wake.
Suala lawabunge 19 waliofukuzwa uanachama na chama chao lakini wakiwa wanakingiwa kifua na serikali ni mfano wa dhahiri wa uvunjwaji na usiginaji wa katiba na sheria.
Tumeshuhudia huko nyuma vyama ikiwemo CCM na CUF vikifukuza wanachama wao ambao ni wabunge na kwa mujibu wa sheria watu hao walitolewa bungeni wakiwa wamefungua kesi mahakamani au hawajafungua kesi kwakuwa kufungua kesi au kukata rufaa hakubatilishi uamuzi uliotolewa na chama mpaka hapo mahakama itakapoamua vinginevyo.
Kama ingekuwa kukata rufaa kunamuweka aliyehukumiwa huru ilipaswa Sabaya naye aachiwe maratu alipokata rufaa lakini aliendelea kubaki ndani hadi uamuzi ulipopitishwa. Hata CUF ilipowavua uanachama wabunge wake wa viti maalumu waliondokewa bungeni licha yakuwa walifungua kesi mamahakamani. Lakini leo tunashuhudia jinsi spika mwanasheria anavyoshiriki uhalifu dhidi ya katiba na sheria za nchi.