Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,400
- 4,074
Wadau ni ukweli usiopingika kwani katiba iliyopo ipo wazi juu ya mbunge kupotexa ubunge wake na moja ya sababu ni kufukuzwa ktk chama chake. Suala la kuutetea uanachama wake ni jukumu lake lakini anautetea uanachama wake akiwa tayari kaondolewa bungeni.
Kitendo cha Hayati Magufuli na Spika Ndugai na tume ya uchaguzi kutowafukuza wabunge 19 waliofukuzwa uanachama wao na CHADEMA ni ukiukwaji mwingine mkubwa wa Katiba kufanywa na viongozi hao baada ya ule wa CAG Assad. Viongozi wetu wamekuwa wakiapa kwa kushika vitabu vitakatifu na kumtaja Mungu kuwa awasaidie ili wailinde waitetee katiba ya nchi lakini badala ya kuheshimu viapo vyao wao ndio wamekuwa wakiukwaji wakubwa tena kwa makusudi wa Katiba.
Toka upatikanaji wa hao wabunge kuteuliwa kwao kuapishwa kwao na mwingine kutolewa gerezani usiku ni ukiukwaji wa katiba.
Suala la wabunge kufukuzwa na vyama vyao sio jipya kwani CUF imewahi kuwafukuza uanachama wabunge wake na Bunge likawafukuza CCM imewahi kumfukuza Sophia Simba na Lazaro Nyalandu uanachama wao na Bungeni wakafukuzwa leo iweje hili la wabunge 19 waliofukuzwa CHADEMA liwe gumu kuwafukuza bungeni?
Ni aibu kwa CCM na Serikali yake kuvunja Katiba ya nchi kwa kukumbatia ujinga wa aina hii.
Ushauri kwa Rais Samia
Kwa kuwa umeamua kuleta maboresho ktk mfumo mzima wa Demokrasia ya vyama vingi hebu iondoe aibu hii ya CCM na Serikali yako kuendelea kuwakumbutia wabunge 19 haramu wanaolipwa kodi za masikini wa Tanzania.
Kwa kuwaondoa bungeni kwani wanaziba nafasi halali za wabunge ambao wangeteuliwa kwa mujibu wa katiba na kuwawakilisha wananchi kuliko hawa 19 wanaojiwakilisha wenyewe. Doa hili litaingia katika historia ya utawala wa awamu ya 5 na awamu ya 6.
Kitendo cha Hayati Magufuli na Spika Ndugai na tume ya uchaguzi kutowafukuza wabunge 19 waliofukuzwa uanachama wao na CHADEMA ni ukiukwaji mwingine mkubwa wa Katiba kufanywa na viongozi hao baada ya ule wa CAG Assad. Viongozi wetu wamekuwa wakiapa kwa kushika vitabu vitakatifu na kumtaja Mungu kuwa awasaidie ili wailinde waitetee katiba ya nchi lakini badala ya kuheshimu viapo vyao wao ndio wamekuwa wakiukwaji wakubwa tena kwa makusudi wa Katiba.
Toka upatikanaji wa hao wabunge kuteuliwa kwao kuapishwa kwao na mwingine kutolewa gerezani usiku ni ukiukwaji wa katiba.
Suala la wabunge kufukuzwa na vyama vyao sio jipya kwani CUF imewahi kuwafukuza uanachama wabunge wake na Bunge likawafukuza CCM imewahi kumfukuza Sophia Simba na Lazaro Nyalandu uanachama wao na Bungeni wakafukuzwa leo iweje hili la wabunge 19 waliofukuzwa CHADEMA liwe gumu kuwafukuza bungeni?
Ni aibu kwa CCM na Serikali yake kuvunja Katiba ya nchi kwa kukumbatia ujinga wa aina hii.
Ushauri kwa Rais Samia
Kwa kuwa umeamua kuleta maboresho ktk mfumo mzima wa Demokrasia ya vyama vingi hebu iondoe aibu hii ya CCM na Serikali yako kuendelea kuwakumbutia wabunge 19 haramu wanaolipwa kodi za masikini wa Tanzania.
Kwa kuwaondoa bungeni kwani wanaziba nafasi halali za wabunge ambao wangeteuliwa kwa mujibu wa katiba na kuwawakilisha wananchi kuliko hawa 19 wanaojiwakilisha wenyewe. Doa hili litaingia katika historia ya utawala wa awamu ya 5 na awamu ya 6.