Katika serikali zote zilizovunja katiba yetu waziwazi kabisa ni serikali ya awamu ya tano, yaani tulitawaliwa kama hakuna katiba vile, anachoamua mkuu na kundi lake dogo ndicho hicho hicho kinageuka kuwa sheria.Hakika inashangaza Sana kuona baadhi ya Viongozi wetu Walioapa Kuilinda Katiba lakini ndio Wanaikanyaga kwa Makusudi tena Hadharani.Kwa Mujibu wa Katiba tuna aina mbili za Wabunge Wakuchaguliwa na Wakuteuliwa.
Na ili uwe Mbunge lazima uwe Mwanachama wa Chama cha Siasa. Moja ya Sababu za kukoma kwa Ubunge ni pamoja na Kufukuzwa Uanachama. Chadema imewafukuza Wabunge 19 Uanachama wao lakini Mpaka leo bado ni Wabunge. Swali la kujiuliza:
Kwanini bado ni Wabunge?
Nani anawalinda?
Kwanini awalinde licha ya kuwa wamemfukuzwa Uanachama?
Tunakuomba Mh. Rais hebu ingilia kati suala hilo kwa Hao Wanaoichezea Katiba na pia Kuokoa Pesa wanazolipwa Wabunge hao ambazo ni Kodi za Wananchi Masikini wa nchi hii.
Hii ni aibu, mama yetu Samia tunaomba ugeukie na huku kwenye siasa, kuna madudu ya ajabu mno!!