Kaini alipata wapi mke wake?

Kaini alipata wapi mke wake?

Alimuoa dada yake kwa kipindi hicho ilikuwa halali tu ndiyo maana hata Ibrahimu naye alimuoa dafa yake pia, Yakobo na Isaka walioa ndugu zako simply kwa sababu popn haikuwa kubwa sana na wengi walitoka kwa Adam baada ya jamii kupanuka na watu kuongezeka ndiyo hilo Mungu akalikataza
wapi imeandikwa ruksa kumuoa dada yako? na

wapi mungu akazuia?
 
Ukisoma "The book of Adam and Eve" (Hakipo kwenye biblia ya kawaida),Utakuta mistari hii hapa chini.

2 And thereafter, Cain slew Abel, but Adam was then one hundred and thirty years old, but Abel was slain when he was one hundred and twenty-two years. And thereafter Adam knew his wife and he begat a son and called his name Seth.

xxiv 1 And Adam said to Eve, 'Behold, I have begotten a son, in place of Abel, whom Cain slew.'

2 And after Adam had begotten Seth, he lived eight hundred years and begat thirty sons and thirty daughters; in all sixty-three children. And they were increased over the face of the earth in their nations.
Hapo utaona Adam alizaa watoto 63 jumla wakike 30 na wakiume 33,walioana wao kwa kwao na kuzaliana.So kuna uwezekano mkubwa pia Cain alimuoa moja ya dada zake pia.
"kuna uwezekano" hizi doubt ndo zinazofanya watu tuconclude ni hadithi tu
 
wapi imeandikwa ruksa kumuoa dada yako? na

wapi mungu akazuia?
Mambo ya Walawi 18:5
Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.
18:6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.
18:7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake.
18:8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako.
18:9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue.
18:10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe.
18:11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake.
18:12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu.
18:13 Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu.
18:14 Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako.
18:15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo.
18:16 Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo.
18:17 Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu.
18:18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai.
18:19 Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake.
18:20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye.
18:21 Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana.
18:22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.
18:23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko.
18:24 Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote.
 
Biblia imekamilika.
Ukweli ni kwamba Mungu hakuandika kila kitu alichokifanya hapa Ulimwenguni.
Mambo mengine alituachia wanadamu tuyagundue kwa akili zetu alizotupatia na alijua tutaendelea kuyagundua.
Ndio maana tafiti za Kisayansi zinaendelea kugundua mambo kadhaa wa kadha.

(Kuku jibu swali lako la Mke wa Kaini)

Ki ushahidi wa Kiteolojia Mwanadamu wa kwanza aliishi Mashariki ya Kati kama sio Iran basi ni Iraq ambapo ndipo kulipokuwa Bustani ya Aden.
Kuna ushahidi wa Mto Tigris ambao unapita huko.

Lakini tafiti za Kiakolojia zinatuambia Mwanadamu wa Kwanza aliisha Tanzania Kondoa Irangi Olduvai Gorge. Kutokana na Ugunduzi wa Dr Leakey.
Hivyo Zinjanthropas anaweza kusemekana kama Binadamu wa Kwanza kutokana na ushahidi wa Kihistoria.

Tunagundua nini hapa.
Bila shaka hapa tunagundua kuwa Mungu, kwanza kabisa aliumba Adam na Eva (Hawa) huko Iraq.
Hao walikuwa race ya ama Kiarabu, Kishirazi, au Kikuresh, yaani moja ya hizo race za Mashariki yakati.
Hapo akatuambia ktk Biblia.

Baada ya hapo Mungu akawaumba Binadamu wengine wawili Mume na Mke ktk Race ya Kiafrika ( weusi )
Weusi akawaweka katika Bonde la Olduvai, ndio Babu zetu sisi blacks.

Akawaumba Wanadamu wawili Mke na Mume Wazungu akawaweka nchi moja huko kwa Wazungu.
Vivyo hivyo kwa Race nyingine za Wahindi, Wachina ambao ni jamii moja na Wakorea, Wajapan Nk.

Wote hao wakazaliana na baadae kuweza kuongezeka na kukutana na kuoleana na race nyingine na kutengeneza watu Chotara.

Hao ndio aliokutana nao Kaini baada ya kuondoka kwao.
Inasadikiwa kuwa Kijakazi wa baba wa Imani Ibrahimu, Hajiri, alikuwa Mwarabu ndio maana akamzalia Ibrahim watoto Maseyidi.
Leo ukienda uarabuni utakuta watu wanajulikana kama Seyidina Abubakar nk.

Kuhitimisha ni kuwa kila Race ilikuwa na Adam na Hawa wao.
Mungu baada ya kuwaumba Adam na Eva. Aliendelewa kuwaumba Wanadamu wawili tena Mume na Mke katika Race nyingine na kuwaweka ktk mabara mengine ndio maana ktk kila bara kuna race flani tofauti na nyingine.

Inasadikiwa Wahindi wekendu waligundulika zamani kabisa huko bara la Amerika, walikutwa wao tu bila mchanganyiko na race
nyingine

Waafrika tulikutwa na watafiti wa kale hapa Afrika.
Mungu hakuwaamuru Manabii waandike ktk Biblia hiyo habari. Aliacha watu kama Dr. Leakey wavumbue.
Sawa mkuu
 
niulize hapa hayo maswali nikujibu mie...

Biblia tunayosoma ni summary tu ya kile alicho fanya Mungu.

Km tungeandika kila kitu Biblia ni kubwaaa mno km ghorofa 16 hivi!!kkm ingeandikwa kila kitu.


Hii. ya leo Ukisoma na vima tumboni kamwe hutaelewa wala usipoteze muda.ni mali ya wateule tu!

Na kweli imeandikwa umo kuwa IMANI SI MALI YA KILA MTU. km huielewi iache!...tu
Sawa
 
Natumai ni mzima na unaendelea vyema na majukumu, Kama unaumwa utapona kwa uwezo wa muumba wako.

HOJA YA MSINGI:

“Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, na baadae Seth, Je, mke wa Kaini alitoka wapi?”
Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa, na kwenye hii mada tutajibu hili swali linalo wachanga sana watu.
MUKTASARI:
Katika Mwanzo sura ya 3 na ya 4 tunapata habari zifuatazo:

(1) Hawa alikuwa “mama ya kila mtu anayeishi.”

(2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu.

(3) Baada ya kufukuzwa na kuwa “mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,” Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ‘mtu yeyote akakutana naye’ na kujaribu kumuua. [Angalia hoja hapa "Kaini anaogopa kuuwawa na watu wengine"] Hapa panaonyesha kuwa Kaini alikuwa na ndugu wengine.

(4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. Kumbe basi Kaini alikuwa na ndugu wengine zaidi ya Abel na Seth.

(5) “Baadaye” Kaini alilala na mke wake “katika nchi ya Ukimbizi.”—Mwanzo 3:20; 4:3, 12, 14-17.

Naomba majibu tafadhari.
Adam aliishi miaka 930,sasa ukiangalia hiyo miaka jiulize mtu huyo akiamua kuzaa anaweza zaa watoto wangapi? Na enzi hizo hakukua na hizi mambo za kulea kwa gharama kubwa sana.
Kiasili kabisa mtoto wa kiume alikua anapewa kipaumbele tangu mwanzo na inawezekana adam alikua na watoto wengine wa kike ambao hawajatajwa katika BIBLIA na ndio maana ukifatilia hata katika mila za kiafrika hasa haoa tz kwa makabila mengi wanawake walikuwa hawaruhusiwi kupata urithi wowote ule, so tangu awali wanawke hawakupewa priority sana.
Hata MUNGU mwenyewe sio muumini wa GENDER EQUALITY ingekuwa sivyo asingetangulia kumuumba adamu then hawa baadaye...... Haya mambo ni magumu kuelewa ila yanaeleweka
 
Unamzungumzia adam alaf unaweka ushahidi wa vitabu vya dini vilivyokuja baada ya adam!

Binaadam ni Adam, mwanaume

Lilith, Hawa, huyu kiumbe mwingine kabisa ambaye ame advance! Na ndio maana vitabu vimekuwa vikikimbia kumzungumzia kabisa, kuna utata mkubwa katika kuumbwa ama kutengenezwa kwa Adam na kisha mwanamke, naamini kuna kiumbe jinsia Ke kabla ya Eve, kabla ya Adam pia. Hii siri imebaki kule kwenye maktaba iliyochomwa moto miaka hiyo, dini hizi tunazofuata sasa hivi inawezekana kwa namna moja ama nyingine tunamuabudu Mungu ambaye hatumkusudii kumuabudu (Tunaabudu Miungu ) kama fikra zetu pandikizi zinavyotupelekesha, ukiangalia vizuri hizi imani kuna mambo mengi sana ambayo kwa namna moja ama nyingine zimejitahidi kuficha asili hasa ya mwanaadamu na kulisha matango pori.

Na mwisho zikaweka mwisho wa kuhoji/kufikiri, ukifikia kiwango cha kukaribia kupata majibu, unawehuka, unakufuru, kuna saa huwa naamini hayawani ( wanyama ) wanajua ukweli zaidi yetu.
 
Nilishwahi uliza swali hili kwa mchungaji wangu mmoja na alinipa majibu haya.

1. Biblia tunayotumia haina rekodi ya kila kitu kilichotokea mwanzo, yaani siyo vyote viliandikwa na inasemekana kuna biblia ambayo ina record ya yote yaliyotokea mwanzo ( binafsi sijawahi kuiona ).

2. Matukio ya kwenye Bible yalikuwa yanaandikwa baada ya kupita muda fulani, yaani utaratibu wa kukusanya mistari ilikuwa ikifanyika ambapo kuna mistari ilibeba rekodi za miaka kadhaa mpaka mstari mwingine kutokea.

Kwa mfano hilo la Kaini, haijulikani ni baada ya miaka mingapi tukio hilo lilitokea na ndani ya huo muda Je, Adam na Hawa hawakufanikiwa kupata watoto wengine ? Ambao nao walitapakaa maeneo tofautitofauti.

3. Kupitia sababu hiyo ya pili ndipo hapo Kaini alipata mke ambaye inaonekana alikuwa ndugu yake either wa damu au alikuwa ndugu yake na ndugu zake wa damu.

Nilimuuliza mchungaji, kwanini sasa kwasasa mtu kumuoa dada yake au ndugu yake ni dhambi ilihali hapo zamani Kaini aliweza kufanya hivyo??

Alinipa jibu hili:

Kwa kipindi kile Mungu aliruhusu iwe hivyo ili watu waendelee kuzaliana na kuijaza dunia hivyo haikuwa dhambi tofauti na inavyotafsirika leo.

Baada ya kunipa ufafanuzi huo nilikuwa na maswali mengi sana ila nilimuaga mchungaji ili nisijeibua maswali yasiyokuwa na majibu
Kitu ninachokisikia kwamba waarabu wanaoana hata ndugu yaweza kua ilianzia huku, mana nasikia hata dini inaruhusu.
 
Natumai ni mzima na unaendelea vyema na majukumu, Kama unaumwa utapona kwa uwezo wa muumba wako.

HOJA YA MSINGI:

“Ikiwa Adamu na Hawa walikuwa na wana wawili, Kaini na Abeli, na baadae Seth, Je, mke wa Kaini alitoka wapi?”
Biblia ina habari za kutosha kujibu swali hilo kwa njia inayofaa, na kwenye hii mada tutajibu hili swali linalo wachanga sana watu.
MUKTASARI:
Katika Mwanzo sura ya 3 na ya 4 tunapata habari zifuatazo:

(1) Hawa alikuwa “mama ya kila mtu anayeishi.”

(2) Muda fulani ulipita kuanzia wakati Kaini alipozaliwa mpaka wakati alipotoa dhabihu ambayo ilikataliwa na Mungu.

(3) Baada ya kufukuzwa na kuwa “mwenye kutanga-tanga na mkimbizi,” Kaini alikuwa na wasiwasi kwamba huenda ‘mtu yeyote akakutana naye’ na kujaribu kumuua. [Angalia hoja hapa "Kaini anaogopa kuuwawa na watu wengine"] Hapa panaonyesha kuwa Kaini alikuwa na ndugu wengine.

(4) Mungu aliweka ishara ya kumlinda Kaini, jambo lililoonyesha kwamba ndugu au dada zake, au watu wengine wa ukoo wangejaribu kumuua. Kumbe basi Kaini alikuwa na ndugu wengine zaidi ya Abel na Seth.

(5) “Baadaye” Kaini alilala na mke wake “katika nchi ya Ukimbizi.”—Mwanzo 3:20; 4:3, 12, 14-17.

Naomba majibu tafadhari.
Simply Kaini alimkula Dada yake
 
Mungu Mwenyewe alipunguza umri wa mwanadamu, Kutoka hiyo miaka hadi Umri wa Mwisho kuwa miaka 120
Mwanzo 5-3.
Bwana akasema ,Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama,
basi siku zitakuwa miaka mia na ishirini.
Ni 6:3
Mwanzo 6:3
Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.
 
Hii miaka 900 ya Adam ilikuwa ni hiihii ya mwezi 12, siku 30 kila mwezi au ?
Ndio
Ndio maana hadi leo
Hatuzidishi kuishi zaidi ya miaka 120
Ukivuka hapo huwi Binadamu tena bali Kiumbe tu.
Kutokana na tamko la Mwanzo 6:3
 
Hii miaka 900 ya Adam ilikuwa ni hiihii ya mwezi 12, siku 30 kila mwezi au ?
Mwanzo 5:3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.
Mwanzo 5:4 Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:5 Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.
Mwanzo 5:6 Sethi akaishi miaka mia na mitano, akamzaa Enoshi.
Mwanzo 5:7 Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:8 Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.
Mwanzo 5:9 Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Mwanzo 5:10 Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:11 Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa.
Mwanzo 5:12 Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Mwanzo 5:13 Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:14 Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa.
Mwanzo 5:15 Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Mwanzo 5:16 Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:17 Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa.
Mwanzo 5:18 Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko.
Mwanzo 5:19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa.
Mwanzo 5:21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Mwanzo 5:22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.
Mwanzo 5:24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.
Mwanzo 5:25 Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.
Mwanzo 5:26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:27 Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na kenda, akafa.
Mwanzo 5:28 Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana.
Mwanzo 5:29 Akamwita jina lake Nuhu, akinena, Huyu ndiye atakayetufariji kwa kazi yetu na kwa taabu ya mikono yetu katika nchi aliyoilaani Bwana.
Mwanzo 5:30 Lameki akaishi baada ya kumzaa Nuhu miaka mia na tisini na mitano, akazaa wana, waume na wake.
Mwanzo 5:31 Siku zote za Lameki ni miaka mia saba na sabini na saba, akafa.
Mwanzo 5:32 Nuhu alikuwa mwenye miaka mia tano, Nuhu akawazaa Shemu, na Hamu, na Yafethi.
 
Nahisi Ni kwa sababu biblia inataja vizazi vya watu kwa kupitia watoto wa kiume mfano Ni :Adam kumzaa kain,Abel na Seth so hii haimaanishi kuwa hao waliotajwa ndio peke yao tu walizaliwa na ADAM NA HAWA ukute Kain hata hakuwa wakwanza kuzaliwa kwa Hawa Bali waeza kuta walizaliwa wa kike wengi alafu yeye Ndo akafatia na kwa kuwa biblia kuhesabu watu ilikuwa inahesabu wanaume tu peke yao labda ndio maana
Ila haya ni mawazo yako si ndio?
 
Ndio.
Ukisoma biblia utanote kitu kimoja, watoto walitajwa wa kiume tu, watoto wa kike hawakutajwa.
Hawa alipata watoto waume kwa wake, lakini watoto wake waliotajwa kwa majina ni watoto wa kiume tu ambao ni WATATU.
Haya mengine umejiongeza mwenyewe maana hujui hata jina mtoto mmoja wa kike wa Hawa
 
Unamzungumzia adam alaf unaweka ushahidi wa vitabu vya dini vilivyokuja baada ya adam!

Binaadam ni Adam, mwanaume

Lilith, Hawa, huyu kiumbe mwingine kabisa ambaye ame advance! Na ndio maana vitabu vimekuwa vikikimbia kumzungumzia kabisa, kuna utata mkubwa katika kuumbwa ama kutengenezwa kwa Adam na kisha mwanamke, naamini kuna kiumbe jinsia Ke kabla ya Eve, kabla ya Adam pia. Hii siri imebaki kule kwenye maktaba iliyochomwa moto miaka hiyo, dini hizi tunazofuata sasa hivi inawezekana kwa namna moja ama nyingine tunamuabudu Mungu ambaye hatumkusudii kumuabudu (Tunaabudu Miungu ) kama fikra zetu pandikizi zinavyotupelekesha, ukiangalia vizuri hizi imani kuna mambo mengi sana ambayo kwa namna moja ama nyingine zimejitahidi kuficha asili hasa ya mwanaadamu na kulisha matango pori.

Na mwisho zikaweka mwisho wa kuhoji/kufikiri, ukifikia kiwango cha kukaribia kupata majibu, unawehuka, unakufuru, kuna saa huwa naamini hayawani ( wanyama ) wanajua ukweli zaidi yetu.
Duh!
 
Back
Top Bottom