Parachichi ya kilo moja 1500 uiweke na sangara 7000 kwa kilo hapo hujauza bondo, miti ya mbao tena bei zimeshuka ulinganishe na dhahabu gram inachezea kwenye 130k , hapana nimetafakari nimestuka kahawa ipo kagera na kigoma pia, Mwanza inategemewa na mikoa ya Geita, shinyanga, mara, tabora, katavi, simiyu, kagera, wote hufunga mizigo mwanza, mikoa tajwa hufanya biashara na eastern congo, uganda, rwanda, burundi, kenya, south sudan directly wanapeleka mazao kama udaga, mahindi, magimbi, mchele na kadhalika, wamefuga ng’ombe nyingi hata kama ni za kienyeji, ndizi kagera hasa karagwe. Kahawa muleba na karagwe, yaani kanda ya ziwa iko mbali kiuchumi kuliko nyanda za juu kusini huu ni ukweli mchungu maana naona pesa inatoka lake zone inafuata mahindi ileje isongole means kusini ni wakulima wakulima sana lakini wanunuzi wako kanda ya ziwa