Tuna maslahi kubwa sana na Kongo, unajua ni asilimia ngapi ya Mizigo ya nje ya Kongo mashariki inapita kutumia bandari ya Dar es Salaam? Nenda Kasanga ziwa Tanganyika ndio utajua tunamaslahi gani na Kongo.
Join Date : 14th May 2014
Posts : 40
Rep Power : 311
Likes Received19
Likes Given0
Karibu janvini kijakazi wa Kagame naona una speed.
Nakukubal sana mkuu ila kwahil hapana......watanzania tuna mengi ya kufanya kwanza huku kwetu.sio kukurupikia ya wenzio tunasindwa kupambana na mafisadi tunakimbilia vita isiyotuhusu,kuna kitu hapa mkuu...think big
nyie majasusi wa kagame sisi ni mafia kuwazd kwanza wote jeshi tumewafundsha na mjue hatukuwapa mbnu zote....mnataka tucheze ngoma mnayoitaka kwa kuprempty ajenda za kijnga kuptia mitandao ya kijamii taarfa zenu tunazo na mlkua mksubri bajeti ya foreign affairs mkiamni hii ajenda itakuwepo na ndio eneo la kuanzia sasa msmamo wetu ni kumchapa kagame popote atakapoleta upuuuzi
Nakukubal sana mkuu ila kwahil hapana......watanzania tuna mengi ya kufanya kwanza huku kwetu.sio kukurupikia ya wenzio tunasindwa kupambana na mafisadi tunakimbilia vita isiyotuhusu,kuna kitu hapa mkuu...think big
Kama umesoma post zote, kuna mdau mmoja alisema si tz tu iliyopeleka majesho congo kuna nchi nyingine kama South Africa n.k
Hii ni kitu kama ulinzi shirikishi vile, leo yanatokea congo huwezi jua kesho yanaweza tokea tz, kwa sababu tz ilisaidia bas na wao hawatakuwa na budi kusaidia tz.
Haya mambo hayatabiriki mkuu.
Jibu kwa kutumia kichwa na si mat@k0 maswali haya: Kenya ipo na inapigana vita Somalia kwa sababu zipi?. Uganda ipo na inapigana vita Somalia na South Sudan kwa sababu zipi. South Africa ina battalion ya jeshi DRC.Malawi ina kikosi DRC.Kwa nini nyie watusi muishangae Tanzania kuwa na battalion Congo DRC!? Ni kwasababu askari wa Tanzania ni tishio kwenye uwanja wa mapambano kwa sababu ndio waliokuwa frontline on the ground na ndio waliowatoa mule kwenye milima mliokua mnaikalia,au?. Kwa maneno yote haya,nimegundua jeshi letu la JWTZ linaogopwa Africa nzima!
Sawa hv ushawahi kukutana na watoto wa mbwa,mbwa mwitu na kuna kikundi kingine kimezuka kinaitwa panya road mtaani kwetu huku hali si shwali juzi tumefunga maduka yetu mkuu haya yote yana sababishwa na watoto wa mtaani kuwa wengi bado hawatutoshi tunataka kuongeza wengine...unaweza kuona kama nafurahisha ila habari ndio hiyo na wanatembea zaid ya watoto 50 wakiwa na mapanga na marungu usiombee ukutane nao
Aisee, wewe utakuwa sio mtanzania.
Kwa mtz aliye mzalendo na nchi yake hawezi zungumza uliyozungumza wewe
Mod, mada za kipuuzi kama hii muwe mnazifuta. Tukiendelea kujadili utumbo huu tunaharibu heshima ya jukwaa hili zuri.
Huyu ni mtanzania halisi, na ndiyo maana ana uchungu na damu za watanzania wenzake zinazomwagika huko kongo pasipo faida kwa tanzania.
Wa Kuvunja Matofali Ya Udongo Kwa Kichwa au Kuvunjiwa Mbao Za Kutengenezea Madawati? Mkwara Wa Miaka 50 Ya Muungano Usikupe Jeuri Huna Jeshi La Kupambana Na Kagame na Rwanda Yake na Ukianzisha Tu Vita Na Kagame Shughuli Itaanzia Hapa Hapa Tanzania Kwani Wanyarwanda Wamejazana ktk Kila Idara Yako Nyeti Unayoijua Wewe ktk Nchi Hii. Kama Kweli Tupo Vizuri Mbona Hadi Leo Hatujamkamata Yule Mwanajeshi Jasusi Wa Rwanda Aliyefanya Kazi JWTZ Kwa Takribani Miaka Saba Iliyopita na Akaondoka Laptop Computer Iliyokuwa Na Vitu na Mambo Nyeti Ya Tanzania? Sasa Kama Huyo Mtu Mmoja tu Anatutoa Jasho Kumsaka Je Hii Inaashiria Nini ktk Medani Za Intelligence Na Millitary? Mimi Nawashauri tu Hebu Mwambieni Mjomba Alianzishe Kisha Muone Mtiti Wake!!!!!!!!!!!!!!
uvamizi wa Rwanda Eastern Congo unafunga dirisha la Tanzania kufanya biashara na DRC Congo yenye watu zaidi ya milioni 60 maana kila wakati wanajikuta wakihamahama makazi yao kukimbia waasi na kushindwa kujihushisha na shughuli za kiuchumi!Nawashangaa mainterahamwe kushangilia Tanzania kupeleka kikosi kule Congo kupambana na M23 kikundi ambacho kinasemekana kinafadhiliwa na Kagame ili kupora mali za wakongo
Hivi kama Kagame ameamua kutumia fursa kupora mali kwa ajili ya wanyarwanda sisi inatuuma nini? au ndo wivu wa maendeleo, hizo mali za Congo zinatusaidia nini mpaka tuzipiganie, Tumesaidia sana ukombozi kusini mwa jangwa la Sahara tena kwa kumwaga damu lakini hamna chochote tunachothaminiwa na mataifa hayo leo hii vijana wetu wanamwaga damu kwa ajili ya wacongo ili mali zao zisichukuliwe na mjanja Kagame ambae anazitumia kujenga nchi yake ifike sehemu tuache kiherehere.
Idi AMINI HAKUWA MWEHU AISE Ni sisi Tanzania tuliruhusu wanajeshi wa Obote kutumia ardhi yetu kwenda kushaburia ndani ya Ugada kwa lengo la kumrudisha Obote a friend of Nyerere. Idi amini alipojibu mapigo kwa kuwafuata maadui wake akageuziwa kibao kwamba katuvamiwa watanzania tukarishwa maneno mengi kuwa iddi amini ni mbaya kupita kiasi Komba naye akimuita joka kuu!!!! lakini kilichotupata watanzania vita hii ilitumaliza kabisa miaka 36 baadae bado tunafunga mikanda!!!!!!"Ugonvi" binafsi upi? Na unaposema Iddi Amin alikuwa na "ugonvi" binafsi na Nyerere, hilo eneo la Kagera alilovamia Iddi Amin lilikuwa ni mali binafsi ya Nyerere?
Hujui unachokiandika fikir tena alafu uje hapa na sio kutukana hovyo taratibu utanielewa kwasababu maafa yanapotokea sisi ndio tunakuwa wa kwanza kuathirika
Hebu jibu maswali niliyokuuliza kwanza. Uganda ipo South Sudan na ipo Somalia kwa maslahi ya nani?. Kenya na Ethiopia zipo Somalia kwa maslahi ya nani? Ukipatia majibu yako ndipo utajua pia kwa nini Tanzania,South Africa na Malawi zipo DRC. Jibu maswali usikwepe!
kumchukia kagame wewe binafsi sio mbaya! Lakini chuki ya watu wachache dhidi ya mtu/nchi isipelekee kuliingiza taifa letu katika uadui na nchi jirani. Mbona uganda jirani zetu pia wanatuhumiwa kusaidia waasi huko congo? Pia je unafikiri raia wa rwanda wote wanampenda rais wetu jk?