KAFULILA aeleze alipata wapi Shahada ya "BBA" na Mwaka gani

hebu tuthibitishe na sio kumshambulia mtoa mada .

athibitisheje, ameshaeleza kuwa hajamaliza UDSM sasa wewe unajua tofauti na hivyo ndo tumwagie data. Kosa litabaki kuwa kosa bila kujali nani kalifanya.
 
Kafulila kama kweli umejimaliza kisiasa...kwa nini usiwe kama wenzako kina Mbowe na Lema, wao kidato cha nne, hawana shinda na BBA.
Wametulia na elimu zao za mtaani

Ritz, you are likely to be the next on my "ignore" list kwa sababu ya upupu wako unaouandika. Kwa Lema sijui, lakini Mbowe amekwenda shule sio kilaza kama wewe!!!!!

Tiba
 
Mavyuo yoooote haya yamejaa dunia mzima leo unauliza alipata wapi BBA? Kama aliipata Nigeria ulitaka akutaarifu wakati anaenda kuichukua? na kama alisoma mtandaoni ulitaka akutangazie? au BBA ni UDSM pekee?
SaharaVoice uko mitaa gani ndugu yangu, uko Dar au Arusha mwaka huu tunauanzaje???? Heri ya Mwaka mpya u can PM for more communication!!!!!!!!!!
 
Bado ninsistiza, atueleze aliipata wapi na vyeti vyake vipo wapi? inaeleweka kuwa mpo wapenzi wa kafulila ambao mliwahi kuwashikia bango mawazili kadhaa kuwa ni mafisadi wa elimu, tunamtaka na jamaa yenu atueleze alisoma na kupata wapi shahada yake ya kwanza katika BBA na siyo kuja kubwabwaja? Atueleze, amezoea kusema uwongo sasa amekamatwa pabaya waziwazi, ktk hili hawezi kukwepa, akanunue vyeti udsm tuone kama anaweza. Aliipata wapi shahada yake? Umma unataka kujua, siyo kusema sema uongo halafu adhani hatujui
Nini Maslahi yako KATIKA HILI?
 
Mkuu hapa ni suala la kutumwa ama ni mtu kujitokeza na kusema habari hizi ni za uongo nakutoa ushahidi kwamba mwaka fulani Kafulila alipata shahada ya BBA mahala fulani. Mimi binafsi huwa sipendi suala la kusema mtu katumwa. Jamaa katoa tuhuma ni jukumu la Kafulila (kama yupo) ajibu ama wanaomjua wajibu siyo kukimbia ati mtu katumwa. Kama hana hiyo BBA kwa nini akanajisi kumbukumbu za bunge kwa kusema kwamba anayo? Naye anaingia kwenye kundi la Msemakweli Kanerugaba lile la Mafisadi wa Elimu kama kweli hana!!
Alikuwa wapi siku zote? Why now? ...just curious!!
 
Ukweli utabaki kuwa ukweli na uongo utabaki kuwa uongo no matter umetendwa na nani? Mwenye ukweli kuhusu hili atujuze ili kumaliza Uzi huu kwani naona wachangiaji wengi wapo kiushabiki zaidi
 
Kafulila kama kweli umejimaliza kisiasa...kwa nini usiwe kama wenzako kina Mbowe na Lema, wao kidato cha nne, hawana shinda na BBA.
Wametulia na elimu zao za mtaani
Kwani Ritz huko Mwandiga wanahitaji BBA, WAO WANAHITAJI MTU MAKINI WA KUPELEKA HOJA ZAO BUNGENI NA MTU HUYO PIGA HUA GARAGAZA NI KAFULILA PERIOD!!!!!!!!!!

 
Unahitajika kuwa na degree zifuatazo:

1) Kujishinda mwenyewe, ili usiwaibie watz rasilimali kidogo zilizoachwa na mafisadi;
2)Kutambua kuwa wapiga kura ndo waajiri wako, hivyo una-ahidi kuishi pamoja nao na kupata mawazo ya kero zao kila wakati; na siyo kuwa pamoja nao mwaka wa 4.5 ukiwaunanyemelea kuchaguliwa tena;
3) Ufisadi kwako uwe kama kum-tizama mama mkwe sehemu nyeti;
4) Mwenye dhamira hai - unasema unacho maanisha na unatenda hivyo hivyo - tehe tehe, maisha bora kwa ......; ili hali wengine wanatama jana, wanafunzi wamekaa chini, mwalim kakopwa miezi 12 na dktr kakopwa miezi 6 wakati msinziaji pale mjengoni anavuta Sh 200K/day;

Ongeza zingine kwa kadri inavyofaa

Big up mkuu hapo umenena hao degree na udokta,ndio wametufikisha hapa tulipo,hatuna shida na elimu ya mtu hapa shida yetu ni uadilifu,na kujali maslahi ya taifa na watu wake!
 
Watu wengine bana kama ni unafiki umepitiliza. Alipoumbuliwa Nyalandu hapa jukwaani kuhusu tuhuma za uhalifu sikumbuki kama kuna mtu alosema tusijadili watu tujadili issues, lakini leo watu wanatoka poovu kumtetea Kafulila wakati kitu chenyewe kipo wazi tu. Kama jamaa yenu aliongopea acheni achanwe siyo mnaleta mijazba hapa.
Acheni ushabiki wa kibwege huo, acha ukweli uchukue nafasi yake, kama kuna mwenye uthibitisho kwamba jamaa ana hiyo BBA leta data kama huna kaa kimya itakusaidia.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, imenishangaza kuona kafulila akiwa amelidanganya bunge la Tanzania na Dunia nzima kuwa yeye ni Graduate wa BBA(UDSM), huku ikijulikana kuwa hakumaliza chuo bali alifukuzwa akiwa mwaka wa kwanza ambapo alikuwa anasoma Evening class udsm. Tunamtaka atueleze hiyo BACHELOR OF BUSINESS ADMINISTRATION aliipata wapi na mwaka gani?

Aidha Bunge nalo linashangaza kwa kukubali kudanganywa kirahisi, hivi ina maana Bunge letu huwa haliagizi wabunge wake wakawasilisha vyeti vyao ili kuvihakiki? Tunataka Bunge nalo litueleze ukweli juu ya Shahada ya BBA ya David Kafulila imetoka wapi?

Huu ni ufisadi mwingine, Kinachoeleweka Kafulila ni Form six leaver tu. Mbaya zaidi Bunge limechapisha sifa za kitaaluma za kafulila na kuweka kwenye website kuwa kafulila ni graduate wa BBA,aliipata wapi na lini? Ufisadi hadi kwenye kughushi elimu! maajabu haya. Twende UDSM wakatueleze kafulila alimaliza lini? Na Bunge litueleze wamepata wapi wasifu huo wa elimu ya Kafulila kama siyo ufisadi?

umetumwa na Mbatia wewe huna lolote, hoja haieleweki, wewe ni mnafiki tu
 
mpaka sasa page ya 5 mbona sion kama kweli jamaa ana BBA??!!!
 
Mtoa mada naona amejiunga JF juzi juzi tu specially kuja kumshughulikia Kafulila humu ndani. Dec 5 alikuja na jina la Wabusara, MaAdmin wakamlima Ban kwa posti zake za kipuuzi, kesho yak Dec 6 akajiunga tena kwa jina la Malagarasi, na toka hapo posti zake zote ni kumhusu Kafulila tuuu....

Malagarasi acha chuki binafsi, hazikufikishi popote.
Malagarasi ni mwajiliwa wa Mbatia, kila akiposti hapa ananyaka mshiko sisi tunamsindikiza, hongera Bwn kwa kazi nzuri !!!!!!!!!!

 
Wakuu, nadhani hatuitendei haki hoja hii kama Great Thinkers. Nakumbuka kuwa hoja kama hii imewahi kuletwa hapa. Watu hawakuhoji why now au why ameileta huyu. let us stick to the issue. Kama Kafulila amefoji elimu inanekana kwua si issue, kwa nini wanapofanya wengine hivyo ionekane kuwa ni issue kubwa na kuwacondemn?
Tuwe msumemo, tukate kotekote bila kumuonea mtu.
NOTE: Sijasema kuwa Kafulila amefoji au hajafoji elimu kwa sababu sijui chochote kuhuisiana na elimu yake mbali ya yale niliyoyasoma hapa
 
Duuu hii inanikumbusha yule mwanasheria aliyechapisha kitabu cha CV feki za waheshimiwa. Nimemsahau jina mwenye jina please?? Nafikiri nae keisha nunuliwa. Ukweli utabaki kuwa pale pale kosa ni kosa kama hajasoma ni kweli aweke wazi kwamba hasoma. Tatizo ni kwamba takwimu zinaonyesha amesoma UDSM na sio Nigeria... Tunajua kuna vyuo hata PHD unaweza pata kwa wiki hiyo hatukatai lakini kwa hili kama takwimu zinaonyesha alisoma UDSM aweke wazi au akanushe basi.
 
tunataka atueleze aliipata wapi? hata machali ana haki ya kuhoji iwapo anaelewa kuwa kafulila kalidanganya bunge kuhusu elimu yake?hoja ya msingi ni kafulila atueleze alisoma wapi na lini? kwa kuwa ni kfulila maneno kama ya chuki yameanza,ila kwa lukuvi, nchimbi,mkulo wakihojiwa elimu zao na kuitwa mafisadi wa elimu safi. Atueleze ilipata wapi hiyo BBA

Licha ya kusisitizwa uondoe neno 'TU' wewe bado umeling'ang'ania tu brother niaje?
Mbona huelewi haraka ukiambiwa? Nalazimika kufikiri pengine kuna fyuzi zimeachia kichwani hivii....
Leta hoja za msingi kwa intelligent minds here, kama huna facebook na twitter itakuaccomodate kwa hili sawa sawa?
 
Tujenge utaratibu wa kujibu Maswali. Sio rahisi kila swali linaloulizwa JF au wasiwasi unaotolewa JF utamfurahisha kila mtu. Ni vyema kujaribu kupambana na mada badala ya kuanza kebehi. Ni kweli wengi wana elimu za magumasi na wakiulizwa wanawaka kama vifuu.

Kama kuna utata na utambulisho wa viwango vya Elimu vya yeyote ni vyema wahusika wakajibu au watu wao wa karibu wanaojua ukweli badala ya malumbano bila majibu.

katiba inasema mbunge anatakiwa ajue kusoma na kuandika Kiswahili au kiingereza haisemi hata ufike darasa la saba. Kazi kweli kweli.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, imenishangaza kuona kafulila akiwa amelidanganya bunge la Tanzania na Dunia nzima kuwa yeye ni Graduate wa BBA(UDSM), huku ikijulikana kuwa hakumaliza chuo bali alifukuzwa akiwa mwaka wa kwanza ambapo alikuwa anasoma Evening class udsm. Tunamtaka atueleze hiyo BACHELOR OF BUSINESS ADMINISTRATION aliipata wapi na mwaka gani?

Aidha Bunge nalo linashangaza kwa kukubali kudanganywa kirahisi, hivi ina maana Bunge letu huwa haliagizi wabunge wake wakawasilisha vyeti vyao ili kuvihakiki? Tunataka Bunge nalo litueleze ukweli juu ya Shahada ya BBA ya David Kafulila imetoka wapi?

Huu ni ufisadi mwingine, Kinachoeleweka Kafulila ni Form six leaver tu. Mbaya zaidi Bunge limechapisha sifa za kitaaluma za kafulila na kuweka kwenye website kuwa kafulila ni graduate wa BBA,aliipata wapi na lini? Ufisadi hadi kwenye kughushi elimu! maajabu haya. Twende UDSM wakatueleze kafulila alimaliza lini? Na Bunge litueleze wamepata wapi wasifu huo wa elimu ya Kafulila kama siyo ufisadi?

Kamanda acha upotoshaji hapa
Kafulila hakufukuzwa UDSM bali alisimamishwa masomo mwaka 2008 kwa kukosa ada akiwa mwaka wa mwisho, na sasa amerudia mwaka 2010 hivyo yupo masomoni kwa Shahada yake ya BBA.

Nenda UDSM ukaangalie orodha ya wanafunzi wa mwaka wa tatu.
Next time uwe na ushahidi wa unayoyasema hapa la sivyo tutakupiga ban!
 
Back
Top Bottom