Kadri mti wake ulivyokuwa unakua, ndivyo na yeye alivyozidi kupata nguvu

Burkinabe

JF-Expert Member
Feb 12, 2023
1,892
3,196
Ooh!
Sawa kabisa.
Usipoelewa sasa, utaelewa baadaye.
Basi bhana, Mfalme Nebukadneza katika fahari yake, akawa anatembea kwenye kuta za mji wa Babeli huku akijisifu namna alivyoiboresha Babeli ndani ya kipindi chake cha uongozi.

Ni kweli hadi kufikia muda huo, Babeli ilikuwepo muda mrefu wa mamia ya miaka. Lakini ni wakati wa uongozi wake ndipo Babeli ilifikia kilele chake cha ustawi kutokana na hekima na uongozi wake bora. Kwa kweli kipindi cha Nebukadneza ilikuwa ni "Hapa Kazi Tu". Na kweli bhana, kazi ilifanyika, ikafanyika kwelikweli matokeo yake, Babeli likawa jiji la kuvutia duniani kote. Babeli ikawa "Super Power" ya dunia.

Baadhi ya vitabu vya dini, huipa Babeli hadhi ya Utawala wa DHAHABU. Hii ni kutokana na utajiri mkubwa sana iliokuwa nao kiasi kwamba vitu vingi vilitengenezwa kwa dhahabu na hata sarafu yao ilikuwa ni dhahabu pia.

Ni kutokana na utajiri huo, basi Mfalme Nebukadneza licha ya kuonywa mara nyingi na Mungu kupitia kwa watumishi wake, bado akaonesha kiburi na kujiona yeye ndo yeye!

Basi bhana, sauti ikasikika ikimwambia atafukuzwa atoke kwenye kiti chake cha enzi kwa muda wa miaka 7. Na kwamba, kwa muda huo wote, atakuwa pamoja na wanyama wa porini na kwamba chakula chake kitakuwa ni nyasi!

Haya bhana, ikawa hivyo. Miaka 7 akawapo porini akiwa na wanyama wa porini, akila nyasi. Baada ya miaka hiyo 7, akarudishwa ikulu na kuendelea na utawala wake huku kiburi chote alichokuwa nacho mwanzoni kikawa kimeisha. Kwa wale wasoma Biblia, mkasome Danieli sura ya 3 na 4.

Mfalme Nebukadneza akaona kwenye ndoto mti ukikatwa na kubakia kisiki ambacho kilikaa hivyo hivyo kwa muda wa miaka 7 kabla hakijaanza kuchipua tena. Baada ya miaka 7, kisiki kikaanza kuchipua na kadri siku zilipokuwa zinaendelea, nacho kikawa kinazidi kuchipua na kukua zaidi na zaidi! Kumbe haya maono yalimuhusu Mfalme Nebukadneza, na kwamba fahari yake ya mwisho ingekuwa maradufu kulinganisha na ile aliyokuwa nayo kabla ya kufukuzwa porini....

Basi bhana, mti wake wa kwanza ukakauka. Lakini ukajitokeza mwingine palepale ulipokuwa umepandwa wa kwanza uliokauka. Na kadri huo mti ulivyozidi kukua, ndivyo na nguvu zake zilivyozidi kuongezeka siku hadi siku.

Mara pap, aliyekuwa anaota ndoto za mchana, akaamka na kuanza kuitafakari ndoto yake.

Nyie!

Haya bhana.

Tafakari njema.


Rejea:
1. Holy Bible
2. The Richest Man In Babylon
 
🤔🤔
.....

Kadri unavyomzingua paka, ndivyo hunyanyua.

maisha ni safari ambayo tayari imekwisha kwa zake juhudi
alipokimbilia ni mbali humchosha akifikiria kurudi,
pole pole ndo mwendo kila akikumbuka ina muuma,
kwanza viliumbwa vidole binadamu ndo akaunda uma, anaamini ye ni mwema na wabaya mungu hawahitaji. wanasema samaki anamengi ya kusema lakini mdomoni ana maji.
muhadithiaji akiwa mmoja story huwaga haikamiliki.
 
Danieli 4:1-37
[1]Mfalme Nebukadreza, kwa watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wanaokaa katika dunia yote; Amani iongezeke kwenu.
[2]Mimi nimeona vema kutangaza habari za ishara na maajabu, aliyonitendea Mungu aliye juu.
[3]Ishara zake ni kubwa kama nini! Na maajabu yake yana uweza kama nini! Ufalme wake ni ufalme wa milele; na mamlaka yake ni ya kizazi hata kizazi.
[4]Mimi, Nebukadreza, nalikuwa nikistarehe katika nyumba yangu, nikisitawi katika nyumba yangu ya enzi.
[5]Nikaota ndoto iliyonitia hofu; mawazo niliyokuwa nayo kitandani mwangu, na njozi za kichwa changu, zikanifadhaisha.
[6]Basi nikatoa amri kwamba wenye hekima wote wa Babeli, waletwe mbele yangu, ili kunijulisha tafsiri ya ndoto ile.
[7]Ndipo wakaingia waganga, na wachawi, na Wakaldayo, na wanajimu; nikawahadithia ile ndoto; wao wasiweze kunijulisha tafsiri yake.
[8]Bali hatimaye Danieli akaingia mbele yangu, ambaye jina lake ni Belteshaza, kwa kufuata jina la mungu wangu; tena ndani yake inakaa roho ya miungu watakatifu; nikamhadithia ile ndoto, nikisema,
[9]Ee Belteshaza, mkuu wa waganga, kwa sababu ninajua ya kuwa roho ya miungu watakatifu inakaa ndani yako, na ya kuwa hapana neno la siri likushindalo, niambie njozi za ndoto yangu niliyoiona, na tafsiri yake.
[10]Njozi za kichwa changu kitandani mwangu zilikuwa hivi; naliona, na tazama, palikuwa na mti katikati ya nchi, urefu wake mkubwa sana.
[11]Mti ule ukakua, ukawa na nguvu, urefu wake ulifika mpaka mbinguni, na kuonekana kwake mpaka mwisho wa dunia.
[12]Majani yake yalikuwa mazuri, na matunda yake mengi, na ndani yake chakula cha kuwatosha watu wote; wanyama wa kondeni walipata uvuli chini yake, na ndege wa angani walikaa katika matawi yake; kila kitu chenye mwili kilipata chakula kwake.
[13]Nikaona katika njozi za kichwa changu kitandani mwangu, na tazama, mlinzi, naye ni mtakatifu, alishuka kutoka mbinguni.
[14]Akapaza sauti yake, akasema, Ukateni mti huu, yafyekeni matawi yake, yapukusieni mbali majani yake, na kuyatawanya matunda yake, wanyama na waondoke hapo chini yake, na ndege katika matawi yake.
[15]Walakini kiacheni kisiki cha shina lake katika ardhi, pamoja na pingu ya chuma na shaba, katika majani mororo ya kondeni; kikapate maji kwa umande wa mbinguni, na sehemu yake iwe pamoja na wanyama katika majani ya nchi;
[16]moyo wake ubadilike, usiwe moyo wa binadamu, na apewe moyo wa mnyama; nyakati saba zikapite juu yake.
[17]Hukumu hii imekuja kwa agizo la walinzi, na amri hii kwa neno la watakatifu; kusudi walio hai wapate kujua ya kuwa Aliye juu anatawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, tena humtawaza juu yake aliye mnyonge.
[18]Mimi, Nebukadreza, nimeiona ndoto hii; na wewe, Ee Belteshaza, eleza tafsiri yake, kwa maana wenye hekima wote wa ufalme wangu hawawezi kunijulisha tafsiri yake; bali wewe waweza, maana roho ya miungu watakatifu inakaa ndani yako.
[19]Ndipo Danieli, aliyeitwa jina lake Belteshaza, akashangaa kwa muda, na fikira zake zikamfadhaisha. Mfalme akajibu akasema, Ee Belteshaza, ndoto ile isikufadhaishe wala tafsiri yake. Belteshaza akajibu, akasema, Bwana wangu, ndoto hii iwapate wao wakuchukiao, na tafsiri yake iwapate adui zako.
[20]Ule mti uliouona, uliokua, ukawa na nguvu, urefu wake ukafika mpaka mbinguni, na kuonekana kwake mpaka dunia yote;
[21]ambao majani yake yalikuwa mazuri, na matunda yake mengi, na ndani yake chakula cha kuwatosha wote; ambao chini yake wanyama wa kondeni walikaa, na ndege wa angani walikuwa na makao yao katika matawi yake;
[22]ni wewe, Ee mfalme, uliyekua, na kupata nguvu; maana ukuu wako umekua na kufika mpaka mbinguni, na mamlaka yako yamefika mpaka mwisho wa dunia.
[23]Tena, kwa kuwa mfalme alimwona mlinzi, naye ni mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni, akisema, Ukateni mti huu, mkauangamize; ila kiacheni kisiki cha shina lake katika ardhi, pamoja na pingu ya chuma na shaba, katika majani mororo ya kondeni; kikatiwe maji kwa umande wa mbinguni, na sehemu yake iwe pamoja na wanyama wa kondeni, hata nyakati saba zipite juu yake;
[24]tafsiri yake ni hii, Ee mfalme, nayo ni amri yake Aliye juu, iliyomjia bwana wangu, mfalme;
[25]ya kuwa utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni, nawe utalazimishwa kula majani kama ng’ombe, nawe utatiwa maji kwa umande wa mbinguni, na nyakati saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote.
[26]Na kwa kuwa waliamuru kukiacha kisiki cha shina lake; ufalme wako utakuwa imara kwako, baada ya wewe kujua ya kuwa mbingu ndizo zinazotawala.
[27]Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha.
[28]Hayo yote yakampata mfalme Nebukadreza.
[29]Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli.
[30]Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu?
[31]Hata neno lile lilipokuwa katika kinywa cha mfalme, sauti ilikuja kutoka mbinguni, ikisema, Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako.
[32]Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni; utalishwa majani kama ng’ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote.
[33]Saa iyo hiyo jambo hilo likatimizwa, likampata Nebukadreza; alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ng’ombe, na mwili wake ulilowa maji kwa umande wa mbinguni, hata nywele zake zikakua, zikawa kama manyoya ya tai, na kucha zake kama kucha za ndege.
[34]Hata mwisho wa siku hizo, mimi, Nebukadreza, nikainua macho yangu kuelekea mbingu, fahamu zangu zikanirudia; nikamhimidi Yeye aliye juu, nikamsifu na kumheshimu Yeye aishiye milele; kwa maana mamlaka yake ni mamlaka ya milele, na ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi;
[35]na watu wote wanaokaa duniani wamehesabiwa kuwa si kitu, naye hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, Unafanya nini wewe?
[36]Basi wakati uo huo fahamu zangu zikanirudia, na kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu, enzi yangu na fahari yangu zikanirudia; na mawaziri wangu, na madiwani wangu, wakaja kunitafuta; nami nikathibitika katika ufalme wangu, nikaongezewa enzi kupita kiasi.
[37]Basi mimi, Nebukadreza, namhimidi Mfalme wa mbinguni, namtukuza na kumheshimu; maana matendo yake yote ni kweli, na njia zake ni za adili; na wale waendao kwa kutakabari, yeye aweza kuwadhili.
 
Ooh!
Sawa kabisa.
Usipoelewa sasa, utaelewa baadaye.
Basi bhana, Mfalme Nebukadneza katika fahari yake, akawa anatembea kwenye kuta za mji wa Babeli huku akijisifu namna alivyoiboresha Babeli ndani ya kipindi chake cha uongozi.

Ni kweli hadi kufikia muda huo, Babeli ilikuwepo muda mrefu wa mamia ya miaka. Lakini ni wakati wa uongozi wake ndipo Babeli ilifikia kilele chake cha ustawi kutokana na hekima na uongozi wake bora. Kwa kweli kipindi cha Nebukadneza ilikuwa ni "Hapa Kazi Tu". Na kweli bhana, kazi ilifanyika, ikafanyika kwelikweli matokeo yake, Babeli likawa jiji la kuvutia duniani kote. Babeli ikawa "Super Power" ya dunia.

Baadhi ya vitabu vya dini, huipa Babeli hadhi ya Utawala wa DHAHABU. Hii ni kutokana na utajiri mkubwa sana iliokuwa nao kiasi kwamba vitu vingi vilitengenezwa kwa dhahabu na hata sarafu yao ilikuwa ni dhahabu pia.

Ni kutokana na utajiri huo, basi Mfalme Nebukadneza licha ya kuonywa mara nyingi na Mungu kupitia kwa watumishi wake, bado akaonesha kiburi na kujiona yeye ndo yeye!

Basi bhana, sauti ikasikika ikimwambia atafukuzwa atoke kwenye kiti chake cha enzi kwa muda wa miaka 7. Na kwamba, kwa muda huo wote, atakuwa pamoja na wanyama wa porini na kwamba chakula chake kitakuwa ni nyasi!

Haya bhana, ikawa hivyo. Miaka 7 akawapo porini akiwa na wanyama wa porini, akila nyasi. Baada ya miaka hiyo 7, akarudishwa ikulu na kuendelea na utawala wake huku kiburi chote alichokuwa nacho mwanzoni kikawa kimeisha. Kwa wale wasoma Biblia, mkasome Danieli sura ya 3 na 4.

Mfalme Nebukadneza akaona kwenye ndoto mti ukikatwa na kubakia kisiki ambacho kilikaa hivyo hivyo kwa muda wa miaka 7 kabla hakijaanza kuchipua tena. Baada ya miaka 7, kisiki kikaanza kuchipua na kadri siku zilipokuwa zinaendelea, nacho kikawa kinazidi kuchipua na kukua zaidi na zaidi! Kumbe haya maono yalimuhusu Mfalme Nebukadneza, na kwamba fahari yake ya mwisho ingekuwa maradufu kulinganisha na ile aliyokuwa nayo kabla ya kufukuzwa porini....

Basi bhana, mti ukakauka. Lakini ukajitokeza mwingine palepale ulipokuwa umepandwa wa kwanza ukakauka. Na kadri huo mti ulivyozidi kukua, ndivyo na nguvu zake zilivyozidi kuongezeka siku hadi siku.

Mara pap, aliyekuwa anaota ndoto za mchana, akaamka na kuanza kuitafakari ndoto yake.

Nyie!

Haya bhana.

Tafakari njema.


Rejea:
1. Holy Bible
2. The Richest Man In Babylon
Hujui kusimulia/uandishi usiovutia. Unataka kunogesha kumbe unaharibu.
 
Punguza mazereu bana😀

At least katufikirisha
Kawafikirisha na nini hapo member wa JF? Hamna kipya ametoa hadithi ya kwenye Biblia. Kajaribu kuipamba ndo kaharibu hajui kusimulia. Amebaki kusema basi bhana, mara paap... Usimuliaji wa kitoto. Ni bora hata angeandika kama ilivyokuwa. Uandishi unataka akili siyo tu kujua kusoma na kuandika.
 
Kawafikirisha na nini hapo member wa JF? Hamna kipya ametoa hadithi ya kwenye Biblia. Kajaribu kuipamba ndo kaharibu hajui kusimulia. Amebaki kusema basi bhana, mara paap... Usimuliaji wa kitoto. Ni bora hata angeandika kama ilivyokuwa. Uandishi unataka akili siyo tu kujua kusoma na kuandika.
Sawa
 
Kawafikirisha na nini hapo member wa JF? Hamna kipya ametoa hadithi ya kwenye Biblia. Kajaribu kuipamba ndo kaharibu hajui kusimulia. Amebaki kusema basi bhana, mara paap... Usimuliaji wa kitoto. Ni bora hata angeandika kama ilivyokuwa. Uandishi unataka akili siyo tu kujua kusoma na kuandika.
Soma aya yake ya mwisho kabisa.

Kuna neno hapo😄
 
Historia inaonesha watu wenye akili sana wakati fulani hueleweka vibaya katika jamii.
Wengine huonekana vichaa kabisa mfano ni yule mgunduzi wa radio. Marafiki zake walimpeleka hospitali baada ya kuwa amewasimulia amegundua kifaa cha kusafirisha sauti bila kutumia waya!
So, hata mimi nisipoeleweka, hata sitajali.

Ila, KADRI MTI WAKE ULIVYOKUWA UNAKUA, NDIVYO NA NGUVU ZAKE ZILIPOONGEZEKA.
 
Back
Top Bottom