Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
Habari za Jumapili,

Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.

Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.

Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.

Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao. Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.

Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.

Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali. Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.

Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa. Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika. Ni Tekniko Knockout.

Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.

Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.

Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.

Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu

Suleiman aliwahi kusema;

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.

Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Kwenye. MUNGU hapo ndo vijana wanakwama.

Kuna Andiko lako ulisema nguvu nyuma ya mtu supernatural power itamfanya afike anapopahitaji kwa haraka. nakubaliana hili jambo.

Pia ulitoa mwongozo wa kuukataa uzinzi kuwa unaua Bahati na future nakubaliana na hilo pia.

Succces inawezekana ikiwa tutaishi Kwa MPANGO
 
Nilipokuwa kijana mdogo niliona wenye miaka 30 ni wakubwa kweli kweli, baada ya kuifikia nikaanza kuona ni wadogo kweli kweli.

Miaka 40 kama sifa ya kugombea urais nchi hii niliona ni umri mrefu kweli kweli.

Sasa nimebakiwa na LIFE BEGINS AT 40, kikubwa uhai tu.
 
Sikubaliani na hoja kuwa mipango ya kimaisha ya vijana wengi inaharibika kwasabb hawamhusishi ama hawamuombi Mungu. Wapo walokole ama mashekhe promax wamefika 50 bado hawana hata kitanda.

Kila mtu ana FATE yake, yaani Kila mtu kachorewa roadmap ya maisha yake na mwenyezi Mungu. Ndiyo maana akina Laizer wanaokota tanzanite yenye thamani ya mabilioni wakati wengine hata mia mbovu hamuokoti.
 
Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Kujenga nyumba na kununua gari ni matokeo, mafanikio ni kufikia lengo katika kazi au biashara unayofanya imekuwa kwa kiasi gani. Kuna watu wamefanya investment kubwa lakini wanaishi nyumba za kupanga

Kitu kingine vijana wana give up mapema sababu wanataka matokeo makubwa kwa haraka bila kuelewa kabla haujafanikiwa kuna indicator huwa zinakuonesha jambo unalolifanya linaenda kukupa matokeo makubwa haijalishi upo chini au kati kuna muda unahitaji subira wengi hawalifahamu
 
Kila mtu ana FATE yake, yaani Kila mtu kachorewa roadmap ya maisha yake na mwenyezi Mungu.
Hakuna mjanja wa kuchora fate yangu mimi.
am the only one to do that.
Mungu mwenyewe hafanyi hicho kitu.
Mungu anamuwazia mema kila mtu, na mpango wake ni kila mtu afanikiwe na aishi maisha bora yanayo reflect viwango vya utukufu wake.

Ila sasa ,bad news ni kwamba, Mungu anawapa watu wooote same ground ya kupambania ili kuyafikia mafanikio.

Pambana wewe.. Lala wewe. Hapo Mungu anakaa kando kuwaangalia wajuz wa kufuata principles and systems za ku unlock secretes of riches.

Success is predictable , so as Failure
 
Sijui ndio ridhki ama ndio zali, bahati, uwezo binafsi au nyota ya mtu..

Ila nilichokisoma kwenye life, unahitaji mtu wa kukuinua maana hata Mungu hashuki chini kuja kukuinua ila hutumia watu.

Nimekutana na watu ambao wapo hardworking, passionate, God fearing, talented and skilled yaani wana kila sifa za kutoboa ila hawajapata sehemu na watu sahihi wa kuwainua

Halafu kuna wale ambao ni average tu na wengine ni wavivu pasee kama hawa tunaokutana nao kwenye ofisi za umma lakini wanatoboa kwa sababu wapo kwenye system lakini pia wana back up

Kwa hiyo maisha ukiyafikiria kiundani utakosa majibu ila cha msingi uishi tu
 
Nakumbuka Jamaa mmoja shule nilimuuliza vipi milioni 80 unapiga kalamu chini na kuacha shule akasema hata milioni 100 hawezi kuufanya huo ujinga. Kwa kipindi kile milioni 100 ilikuwa pesa haswa.

Jamaa kweli kapiga one Form four na six kapiga one pia kasoma UDSM ila sasa maisha yanamkimbiza kama alivyokuwa anayakimbiza masomo.
🤣🤣🤣🤣
 
Kwenye. MUNGU hapo ndo vijana wanakwama

Kuna Andiko lako ulisema nguvu nyuma ya MTU supernatural power itamfanya afike anapopahitaji Kwa haraka . nakubaliana hili jambo.

Pia ulitoa mwongozo wa kuukataa uzinzi kuwa unaua Bahati na future nakubaliana na hilo pia.


Succces inawezekana ikiwa tutaishi Kwa MPANGO

Vîjana sasa hawamini katika supernatural powers
 
Nskumbuka Jamaa mmoja shule nilimuuliza vipi milioni 80 unapiga kalamu chini na kuacha shule akasema hata milioni 100 hawezi kuufanya huo ujinga.
Jamaa kweli kapiga one Form four na six kapiga one pia kasoma UDSM ila sasa maisha yanamkimbiza kama alivyokuwa anayakimbiza masomo.
🤣🤣🤣🤣

Hiyo milioni mia moja hata akiajiriwa hawezi kuipata kwa pamoja bila wizi
 
Sijui ndio ridhki ama ndio zali, bahati, uwezo binafsi au nyota ya mtu..

Ila nilichokisoma kwenye life, unahitaji mtu wa kukuinua maana hata Mungu hashuki chini kuja kukuinua ila hutumia watu.

Nimekutana na watu ambao wapo hardworking, passionate, God fearing, talented and skilled yaani wana kila sifa za kutoboa ila hawajapata sehemu na watu sahihi wa kuwainua

Halafu kuna wale ambao ni average tu na wengine ni wavivu pasee kama hawa tunaokutana nao kwenye ofisi za umma lakini wanatoboa kwa sababu wapo kwenye system lakini pia wana back up

Kwa hiyo maisha ukiyafikiria kiundani utakosa majibu ila cha msingi uishi tu

Ndipo unapomkumbuka Suleiman aliposema,

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.
 
Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Kujenga nyumba na kununua gari ni hayo matokeo mafanikio ni kufikia lengo katika kazi au biashara unayofanya imekuwa kwa kiasi gani kuna watu wamefanya investment kubwa lakini wanaishi nyumba za kupanga

Kitu kingine vijana wana give up mapema sababu wanataka matokeo makubwa kwa haraka bila kuelewa kabla haujafanikiwa kuna indicator huwa zinakuonesha jambo unalolifanya linaenda kukupa matokeo makubwa haijalishi upo chini au kati kuna muda unahitaji subira

Kifupi, vijana wanataka ushindi kabla mechi haijaisha. Wakati ushindi ni mpaka kipenga cha mwisho kipulizwe
 
Sikubaliani na hoja kuwa mipango ya kimaisha ya vijana wengi inaharibika kwasabb hawamhusishi ama hawamuombi Mungu. Wapo walokole ama mashekhe promax wamefika 50 bado hawana hata kitanda.

Kila mtu ana FATE yake, yaani Kila mtu kachorewa roadmap ya maisha yake na mwenyezi Mungu. Ndiyo maana akina Laizer wanaokota tanzanite yenye thamani ya mabilioni wakati wengine hata mia mbovu hamuokoti.

Kuwa Mlokole au mwenye haki hakukufanyi ufanikiwe.
Unafanikiwa kwa sababu Mungu ndiye ameamua ufanikiwe.
Waliofanikiwa wengi wao wanakiri kuwa hawakutegemea kama wangefanikiwa. Yaani wanaita ni bahati.

Wengi wanaofeli wanafeli kwa sababu wanaamini katika uwezo wao wenyewe.

Tafuta waliofanikiwa wote wanafanana katika jambo moja. Kuamini kuwa mafanikio ni majaliwa ya Mungu
 
Hakuna mjanja wa kuchora fate yangu mimi.
am the only one to do that.
Mungu mwenyewe hafanyi hicho kitu.
Mungu anamuwazia mema kila mtu, na mpango wake ni kila mtu afanikiwe na aishi maisha bora yanayo reflect viwango vya utukufu wake.

Ila sasa ,bad news ni kwamba, Mungu anawapa watu wooote same ground ya kupambania ili kuyafikia mafanikio.

Pambana wewe.. Lala wewe. Hapo Mungu anakaa kando kuwaangalia wajuz wa kufuata principles and systems za ku unlock secretes of riches.

Success is predictable , so as Failure

Je, unaijua kesho yako itakuaje ?..

Je, unaweza kuamua kesho utakutana na nani au lipi ?...

Kama nikikurudisha 5 years back, je hapo ulipo ndipo ulipotaka kuwa kwa kitu ukifanyacho na kwa level uliyoifikia ?..

What I know, binadamu tuna control mchakato tu ili tuweze influence results ila hatuna UBAVU wa kutengeneza matokeo vile tunavyotaka sisi na kama ingekuwa hivyo, bhasi zaidi ya 80% ya biashara za Tanzania zisingekufa kabla ya kufikisha miaka 5 maana sidhani kama kuna mtu anaeanzisha biashara ili ife...

One thing nachoweza kukubaliana nawe ni kuwa kila kinachotokea mara nyingi hutokana na maamuzi tunayofanya ila sababu za kupelekea kufanya uamuzi fulani, kuna zile tunazoweza kuzicontrol na zile tusizoweza

Personally, huwa naamini sana katika jitihada sana na strategy za kufanya mambo lakini huwa sipuuzi uwepo wa circumstances ambazo zipo nje ya uwezo wangu, japo sizipi uzito sana ili nibaki persistent
 
Back
Top Bottom