Hapakua na fursa ya kuunda joint command, ndio ilikua mara yetu ya kwanza kuvamiwa na magaidi waliongia kwenye jengo na kuanza kuua kila asiye muislamu. Ikawa kila kikosi kufanya mchakato wa kufika pale haraka iwezekanavyo, kwa vile makomando huwa wamesubiria matukio kama haya, wao walifika mara moja na kutathmini ngoma ilivyo, wakabuni fasta mkakati wa kufunga kitabu kwa dakika thelathini na wakaanza shughuli kishujaa na kikomando.
Ghafla KDF wakaingia kwa vurugu na ubabe, maana wao wamefunzwa kupiga bila kukamata. Kwa bahati mbaya wakampiga askari mmoja ambaye alikua kiongozi wa wale makomando, alikua anaongoza jeshi lake kwa mbele. Pakaibuka majibizano na ugomvi baina yao, makomando wakaona busara wageuze na kuwaachia wababe.
Sasa baada ya hilo tukio, mikakati imebuniwa ya kuwawezesha kufanya kazi pamoja, kifupi ni kwamba wakati inatokea ngoma kama hii, makomando wanapewa kipao mbele. Kama jinsi ilitendeka pale Garissa, makomando walifika na kuzima ngoma ndani ya dakika 12. Tazama hii video