baharia 1
JF-Expert Member
- Sep 13, 2019
- 2,973
- 4,332
Wagambo na Sungusungu acheni ushamba! Mna uafande wa mchongo, sura za kauzu na njaa kali
Hawa Sungusungu/Wagambo (Nyungu) mbona wana roho mbaya hivi? Wakifanikiwa kuwa Maaskari kamili si watavunja watu viuno.
Wakuu wa jukwaa, kwanza salamu.
Leo nataka niwape makavu laivu Hawa viumbe, bila kuremba wala kuweka urembo wa aina yoyote.
Kuna hili kundi la watu wanaojiita ulinzi shirikishi, maarufu kama Sungusungu, Wagambo, au Nyungu.
Hivi hawa viumbe mbona wana roho mbaya na roho za kwanini kiasi hiki?
Unakuta mtu ni mlinzi tu wa mtaani lakini akikatiza mchana kweupe sura ameikunja kama amekunywa shubiri. Hawacheki na wowote, wamejaa kauzi utafikiri wanalipwa mamilioni.
Kichekesho sasa, wanapenda sifa za kijinga kufa mtu Ukikutana naye ukamwambia "Mambo vipi Afande?" au "Inakuwaje Kamanda/Soja?" basi utaona anachekelea hadi jino la mwisho. Anajiona yeye ndio CDF wa mtaa. Anakuwa rafiki yako kisa sifa za kijinga, roho mbaya inamshuka kidogo. Hivi hawa mbwa wana shida gani kichwani
Mfano Huyu Juma huyu Juma nilimpokea mimi mwenyewe kutoka kijijini miaka 7 iliyopita. Alikuja hana mbele wala nyuma, hata shule ya msingi la saba hakumaliza, hajui hata kusoma vizuri. Sasa hivi amefanikiwa kuingia kwenye hizi kamati za Nyungu za mtaani. Ohoo! Kujikuta sasa hivi kumepitiliza.
Mtaani hacheki na mtu kabisa, yani akipita anajiona yeye ndio mmiliki wa mji. Kumbe ukweli ni kwamba, elimu yenyewe hana, na hata angefika kidato cha nne Form 4 nchi hii ajira hakuna angeishia hapo hapo.
Cha kusikitisha sasa, huyu Juma na washirika wake wakiwa mtaani wanajifanya wajuaji mbele ya watu wasiojua sheria wala haki zao.
Wanawatishia raia, wanasingizia watu makosa, na kujifanya wao ndio mahakama na polisi kwa pamoja. Wananyanyasa watu wanyonge kisa tu wenevaa vile viraka vyao na kushika virungu
Wakikuotea Usiku Mkubwa Hapa sasa ndio utajua hawana tofauti na wanyama. Ole wako wakukute usiku mkubwa ukitoka kwenye mihangaiko yako au mtoko. Hawataki maelezo, hawataki kuelewa. Utawekwa chini ya ulinzi na kuanza kutembea nao mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba. Unakuwa kama mateka wao!
Utalinda nao doria usiku mzima kwenye baridi kali hadi asubuhi pasipo makosa yoyote ya msingi, kisa tu unakatalia kutoa hela ya sigara au "chai"
Wanakupelekesha utafikiri wewe ni mhalifu wa kimataifa, kumbe ni njaa tu inawasumbua. Wakikukuta na mpenzi wako ndio kabisa, wataanza kukutolea maneno machafu ya kashfa na kukutishia kuwapeleka polisi ili tu muwaongezee dau la rushwa.
Mna roho mbaya kwa sababu mnaumia kuona wenzenu wamepambana na wana maisha yao mazuri, wakati ninyi mnaambulia kulipwa posho za elfu mbili mbili za mchango wa ulinzi wa kila nyumba, tena kwa mbinde
Kazi yenu kubwa imebaki kuwa ni kukamata machokoraa, kufukuza kuku mtaani, na kukimbiza wamachinga wanaouza nyanya barabarani. Hiyo ndio "level" yenu ya juu kabisa ya uafande.
Mkishalewa viroba vya jioni mnaanza kujiona ninyi ni makomando wa JWTZ waliorudi kutoka vitani DRC. Amkeni ninyi! Hamna hadhi hiyo na hamtakuja kuipata kwa tabia zenu hizo za kishamba.
Hapa najiuliza swali moja la msingi sana, Hawa watu wenye njaa zao na elimu za kuunga-unga, wakija kufanikiwa kuvaa magwanda ya uaskari kamili wa JWTZ au Polisi, si watavunja watu miguu na viuno mitaani
Kama tu cheo cha kuvaa viraka na virungu vya miti kinawapa ulevi wa namna hii na kuwafanya wajione miungu watu, wakipewa SMG si watamaliza raia
Wagambo na Sungusungu acheni ushamba. Kazi yenu ni kulinda usalama wa raia na mali zao, sio kuleta uafande wa mchongo, unyanyasaji, na roho mbaya kwa watu waliowapokea mjini.
Najua humu JF mmo wengi mnaofanya hii kazi ya Nyungu na mnasoma huu uzi mkiwa mmekunja sura zenu za kauzu. lakini ukweli ndio huo ushawafika kooni
MWISH
Hawa Sungusungu/Wagambo (Nyungu) mbona wana roho mbaya hivi? Wakifanikiwa kuwa Maaskari kamili si watavunja watu viuno.
Wakuu wa jukwaa, kwanza salamu.
Leo nataka niwape makavu laivu Hawa viumbe, bila kuremba wala kuweka urembo wa aina yoyote.
Kuna hili kundi la watu wanaojiita ulinzi shirikishi, maarufu kama Sungusungu, Wagambo, au Nyungu.
Hivi hawa viumbe mbona wana roho mbaya na roho za kwanini kiasi hiki?
Unakuta mtu ni mlinzi tu wa mtaani lakini akikatiza mchana kweupe sura ameikunja kama amekunywa shubiri. Hawacheki na wowote, wamejaa kauzi utafikiri wanalipwa mamilioni.
Kichekesho sasa, wanapenda sifa za kijinga kufa mtu Ukikutana naye ukamwambia "Mambo vipi Afande?" au "Inakuwaje Kamanda/Soja?" basi utaona anachekelea hadi jino la mwisho. Anajiona yeye ndio CDF wa mtaa. Anakuwa rafiki yako kisa sifa za kijinga, roho mbaya inamshuka kidogo. Hivi hawa mbwa wana shida gani kichwani
Mfano Huyu Juma huyu Juma nilimpokea mimi mwenyewe kutoka kijijini miaka 7 iliyopita. Alikuja hana mbele wala nyuma, hata shule ya msingi la saba hakumaliza, hajui hata kusoma vizuri. Sasa hivi amefanikiwa kuingia kwenye hizi kamati za Nyungu za mtaani. Ohoo! Kujikuta sasa hivi kumepitiliza.
Mtaani hacheki na mtu kabisa, yani akipita anajiona yeye ndio mmiliki wa mji. Kumbe ukweli ni kwamba, elimu yenyewe hana, na hata angefika kidato cha nne Form 4 nchi hii ajira hakuna angeishia hapo hapo.
Cha kusikitisha sasa, huyu Juma na washirika wake wakiwa mtaani wanajifanya wajuaji mbele ya watu wasiojua sheria wala haki zao.
Wanawatishia raia, wanasingizia watu makosa, na kujifanya wao ndio mahakama na polisi kwa pamoja. Wananyanyasa watu wanyonge kisa tu wenevaa vile viraka vyao na kushika virungu
Wakikuotea Usiku Mkubwa Hapa sasa ndio utajua hawana tofauti na wanyama. Ole wako wakukute usiku mkubwa ukitoka kwenye mihangaiko yako au mtoko. Hawataki maelezo, hawataki kuelewa. Utawekwa chini ya ulinzi na kuanza kutembea nao mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba. Unakuwa kama mateka wao!
Utalinda nao doria usiku mzima kwenye baridi kali hadi asubuhi pasipo makosa yoyote ya msingi, kisa tu unakatalia kutoa hela ya sigara au "chai"
Wanakupelekesha utafikiri wewe ni mhalifu wa kimataifa, kumbe ni njaa tu inawasumbua. Wakikukuta na mpenzi wako ndio kabisa, wataanza kukutolea maneno machafu ya kashfa na kukutishia kuwapeleka polisi ili tu muwaongezee dau la rushwa.
Mna roho mbaya kwa sababu mnaumia kuona wenzenu wamepambana na wana maisha yao mazuri, wakati ninyi mnaambulia kulipwa posho za elfu mbili mbili za mchango wa ulinzi wa kila nyumba, tena kwa mbinde
Kazi yenu kubwa imebaki kuwa ni kukamata machokoraa, kufukuza kuku mtaani, na kukimbiza wamachinga wanaouza nyanya barabarani. Hiyo ndio "level" yenu ya juu kabisa ya uafande.
Mkishalewa viroba vya jioni mnaanza kujiona ninyi ni makomando wa JWTZ waliorudi kutoka vitani DRC. Amkeni ninyi! Hamna hadhi hiyo na hamtakuja kuipata kwa tabia zenu hizo za kishamba.
Hapa najiuliza swali moja la msingi sana, Hawa watu wenye njaa zao na elimu za kuunga-unga, wakija kufanikiwa kuvaa magwanda ya uaskari kamili wa JWTZ au Polisi, si watavunja watu miguu na viuno mitaani
Kama tu cheo cha kuvaa viraka na virungu vya miti kinawapa ulevi wa namna hii na kuwafanya wajione miungu watu, wakipewa SMG si watamaliza raia
Wagambo na Sungusungu acheni ushamba. Kazi yenu ni kulinda usalama wa raia na mali zao, sio kuleta uafande wa mchongo, unyanyasaji, na roho mbaya kwa watu waliowapokea mjini.
Najua humu JF mmo wengi mnaofanya hii kazi ya Nyungu na mnasoma huu uzi mkiwa mmekunja sura zenu za kauzu. lakini ukweli ndio huo ushawafika kooni
MWISH