JWTZ na Polisi mna ugomvi gani usioisha!

JWTZ na Polisi mna ugomvi gani usioisha!

Wacha wapigwe tu maana wakiwakamata raia wema wanawapa kipigo sana kinyume na masharti ya kazi yao.
 
Ukisikia polisi kapigwa ujue kapigwa na mwanajeshi zaidi ya mmoja

Ukisikia mwanajeshi kapigwa ujue kapigwa na polisi zaidi ya moja...

Askari ndivyo walivyo, wakiwa zaidi ya mmoja wanakuwa na akili fulani hivi ya kibabe, akibaki mmoja anapooza kama maji ya mtungini...

Sijawahi Kusikia polisi mmoja au JW mmoja kampiga polisi au JW
 
Huko porini kuna ugomvi mmoja ambao ni very natural; upo tangu mwanzo hadi ukamilifu wa dahari; hauwezi kusuluhishwa kwa namna yoyote kwa sababu kujaribu kufanya hivyo ni kumtakia mmojawapo kifo. Hawa jamaa wanaitwa "eternal enemies" na sio wengine bali ni simba na fisi.

Simba hawezi akavikuta vichanga vya fisi akaviacha ni lazima aviue na fisi naye hivyo hivyo ni lazima aviue vichanga vya simba vinapokuja katika anga zake. Always wao ni mapigano wakigombea msosi na kuuliana vichanga - ndivyo ilivyo kwa JW na Polisi wa nchi hii ugomvi wao hauelezeki wala hauna sababu ila hautaisha - upo tu naturally. Hata kama wakubwa majukwaani watachekeana kinafiki lakini mioyoni wanagombana.
MMOJA ANALINDA MIPAKA YA NCHI ISIVAMIWE NA MAADUI,mmoja analinda usalama wa raia ndani ya nchi. MMOJA MKUBWA,mwingine mdogo......
kuna nchi moja yalifanyika mapinduzi wanajeshi wakatangaza 'kuanzia sasa polisi wote ni raia' ikabidi polisi wafiche nguo na kukimbia kambi zao. kwa ujumla wote wanafanya kazi zao vizuri ila kuna baba na mtoto. nilihudhuria mazishi ya generali mmoja, wakati wa kupiga mizinga ya heshima hawa wa 'ndani' tulijaa nao hofu kwa mingurumo!!
 
Hivi wajua physical fitness z wanajeshi? Wana vitengo vingi ambavyo vinakaribiana na commando level.....acha kabisa polisi w mafunzo ya kawaida sana karate basic na general fitness! Wanajeshi wanafundishwa kukupiga na kukuua ndani muda mfupi sana! Hajafundishwa kukamata! Anaua.....!! Hata mazingira, wale wanajeshi wako kambini ful time wako mazoezi kila siku ndio order....polisi akitoka depo....yuko kazini muda mwingi hata mazoezi hawana tena!

Hata Juzi umesikia Mh. Rais (Mkuu wa Nchi) akiwaambia Makanda wa Polisi pale Dodoma kuwa wanapokea rushwa na kuwaacha vijana walioenda kwenye mafunzo ya kipolisi kukaa hotelini hata gwaride hawapigi. Kwa mtindo huu unategemea Polisi apambane na mwanajeshi? Mwanajeshi hata atoke leo kwenye mafunzo lazima atamdhibiti tu polisi, hasa kama polisi wetu wenyewe ndo hao wa kutoa rushwa pale CCP ili wakae hotelini hata mazoezini hawaendi.
 
Walikujaga mtaani kwetu 2008 walizurula vijiwe vyote wanatoa vipigo Kuna jamaa mmoja kocha wa mpira alimjibu jeuri mmoja wao dah alichapika, mpaka mama yake akajaribu kuomba Msamaha wakamtimua baadaye wakamchukua wakampeleka mto tenge hulikuwa hauna maji mengi sana akambiwa atafute kambale
 
Hizi habari za JWTZ kuwapiga Polisi au Polisi kuwapiga JWTZ huwa ni za kujirudia kila mara

Sijawahi sikia JWTZ kampiga magereza au zimamoto.



Hasa Polisi mnatia aibu sana! kila siku mnakungutwa nyie! JWTZ wana nini cha ziada cha kuwapiga kila siku. Mbona mnatukunguta sana mkitukamata sisi raia!


JWTZ na POLISI mna ugomvi gani usioisha? sijawahi sikia viongozi wa Polisi au JWTZ wakiliongelea hili.
View attachment 344869
ilikuwa zamani ila cku hizi wakikujua ww jwtz uliompiga polisi mwenzao watakomaa mpk utiwe ndani aisee
 
Aisee mkuu hii kitu imekatazwa. Yaani ungeweza kurekodi tukio mpaka muda huu huyo mwanajeshi angekua Segerea ananyea ndoo. Sasa hivi wakubwa wao wameweka sheria kali dhidi ya askari wao ambao miaka ya nyuma kidogo walijitia uwendawazimu ktk matendo yao. Mfano mara kufunga mtaa na kutembeza kisago kwa anayehusika na asiyehusika.
Segerea kufanya nini?
 
huo ugomvi hautaisha na ndio kwanza unazidi kukuzwa.

afande:kuruta makofiiiiiiiiii
kuruta😛a pa pa pa....
afande:sengwile makamandaaaaaa...
kuruta:sengwile makamanda..
afande:nalela kumanya...
kuruta:aiyeeeeeeeeeeeeeee
afande:kazi ya jeshi ni ngumu
kuruta:aiyeeeeeeee
afande:yahitaji kuvumilia
kuruta:aiyeeeeeeee
afande:usiwe kama polisi
kuruta:aiyeeeeeeeee
afande😛ushapu kwenye godoro
kuruta:aiyeeeeeee
afande:uwe kama lisoja..
kuruta:aiyeeeeeee
afande😛ushapu kwenye kokoto
kuruta:haiwezekani kamanda kupigwa na polisi
kuruta:haiwezekani kamanda kupigwa na polisi
afande:usiwe kama polisi
kuruta:aiyeeeeeeeee
afande:kutwa kucha nakirungu
kuruta:aiyeeeeeeeeeeeee

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
afande:
ole wako siku nimeshuka ubungo nakuona umekunjwa na polisi au teja .

hahahaha

mahovyo hovyo....
 
Kama umesikiliza clip ya mke wa Waziri Mahiga na polisi ndio utajua kwanini wanapigana hawa jamaa. Polisi kuna busara ndogo sana ya kiuongozi wamekosa ndipo tatizo linapoanzia hapo jambo dogo la kumaliza kiuongozi au kama kiongozi unawaza pesa au unalifikisha ngazi za juu.
 
Back
Top Bottom