JWTZ mpaka leo imeshindwa kuajiri wasomi wenye vipaji halisi, sababu hizi hapa...

wasomi walikuwa wanafungwa kamba viunoni wanaburuzwa mstari wa mbele na ma koplo kwenye vita ya kagera, digrii yako ya sheria ipeleke polisi
 
Ondoa upuuzi wako hapa. Watz na majungu tu, fanya kazi, masuala ya jeshi waachie wenyewe.
 
Huyu anaonekana ni mwanajeshi ambaye ana frustration...kama jeshi imekushinda rudisha jezi za watu alafu rocharocha, jeshini wanatafutwa wapiganaji PHD sio sehemu yake pale na ata akiwepo kama mrema ni kwa ajili ya propaganda.:A S angry:
 
Thanks much Yericko Nyerere Moshe Dayan Mtumishi Wetu na wadau wengine kwa maelezo murua kabisa juu ya JWTZ.
Bila shaka tuna kila sababu ya kujivunia jeshi letu. Kama wasemavyo wazaramo, kazi ya jeshi kugangamala, wasomi mgangamale basi msitafute slope hata katika kazi adhimu kama ya jeshi.
 
Last edited by a moderator:
Sina uhakika na madai yako; ila ninajua kuwa kwa muda mrefu sana aliyekuwa mkuu wa Nyumbu pale (General Mashauri) ni rafiki yangu wa siku nyingi sana tuliyejuana tangu akiwa Luteni wa Jeshi akiwa anasomea Masters in Mechanical Engineering huko Ireland; huyu ni msomi aliyeiva sana Mechanical Engineering. Nawafahamu wakuu kadhaa a hospitali ya Lugalo walipita, wote ni wasomi wa hali juu sana katika nyanja zao ama wakiwa MD au wakiwa na specialist degrees. Vile vile ninawafahamu makamanda kadhaa wa vita ya ardhini (Army) niliosoma nao shule za sekondari ambao wana elimu za juu sana za masters na zaidi ya hapo walizopata sehemu mbalimbali za dunia kama Canada, Egypt, UK, USA, South Africa na China.

Nadhani madai yako uliyoweka hapo juu siyo concrete sana, labda kama unamjua mtu mmoja tu ndani ya TPDF anayefanya unayodai, ila siyo kweli kuwa JWTZ yetu ya leo ni kama ile ya mwaka 1964 ambayo haikuwa na wasomi.

comrade,,, haya mambo hawajui ndio maana hua wanatoa kashfa sana, kuna wasomi na wamebobea hasa,, kwa mfano field engineers wengi wamesomeshwa nje kwenye vyuo vikubwa vya kijeshi,, yakitokea maafa, hawa mnaowadharau hua wanawajengea madaraja kwa siku mbili au tatu na baada ya hapo wizara ya ujenzi hujisahaulisha na madaraja haya hutumika miaka na miaka japo ni temporary.., kwa wale myopic hajui na daily anapita daraja la mlalakuwa

Baada ya mafuriko kilosa, nadhani mnakumbuka nani walijenga yale madaraja ya reli ya kati na in record time.., need we say more?
 
Ukiangalia mfumo mzima wa ajira utabaini yafuatayo
1. Waalimu waliopo vyuoni 90% ni kikwazo kwa wasomi wengi wanaojiunga na jeshi hilo, akitokea mwanafunzi mwenye elimu kubwa hata Phd watafanya kila mbinu wamfukuze kwa kisingizio cha utovu wa nidhamu au watacomment kuwa kafeli.

2. Trainning zao hazija base kutafuta vipaji vya kweli katika nyanja muhimu kitaifa, kama vile madaktari, Eng, nk. Mfano Nyumbu mpaka leo wameshindwa kuifanya iwe ya kizalishaji toka enzi za mwalimu. Lugalo mpaka leo hawana hata blood bank sababu wanasayansi tiba hawapo ndio maana wanashindwa kukabiliana na migomo ya MH, sababu huko wengi 80% ni AMO na CO.

3. TMA ni kikwazo kikubwa sana katika kuwapata wasomi wazuri ndani ya jeshi hilo, elimu ya rasilimali watu kwa waalimu inawezekana ikawa ni issue. So they are trying to reduce the number of students kwa visingizio vya nidhamu ambayo ukifuatilia kiundani sio nidhamu as such but ni kutojua ubaya wakumfundisha mtu at certain level na kumwachisha mafunzo. HILO N BOMU BAADAYE.

4. Mazingira dhaifu kuwawezesha wenye vipaji kubuni kwa uhuru na kutumia taaluma zao, kufanya tafiti chanya maeneo yao ya kazi, mpaka leo hatujaziona.

5. Officer aliyetokea uraiani moja kwa moja I mean those who have got a little knowledge kuwa mkufunzi, atafundisha nini kama sio kupika majungu na kukosa comfidence?

Hayo machache yaliyobainishwa hapo juu ni chanzo kikubwa cha jeshi letu kuwa kama lilivyo hivi leo.

mshkaji umekuja n hasira! wajeda walikutema nini?
 
Duh yaani we Mbayaaaaaa..kumbe siku hizi Masters of Law ni LLB??? na LLM itakuwa ndio Bachelor of Laws eti!!! we hatareeeee, duh, hakika we ni Mkalleeeeeee

Ni mhitimu wa Kampala International University huyo!
 
Thanks much Yericko Nyerere Moshe Dayan Mtumishi Wetu na wadau wengine kwa maelezo murua kabisa juu ya JWTZ.
Bila shaka tuna kila sababu ya kujivunia jeshi letu. Kama wasemavyo wazaramo, kazi ya jeshi kugangamala, wasomi mgangamale basi msitafute slope hata katika kazi adhimu kama ya jeshi.

Asante mkuu, ninaamini jeshi letu ni imara tena sana!
 
Last edited by a moderator:
We Kilaza, an army is an institution of its own kind (sui generis) ,sio taasisi ya fedha au chama cha wafanyakazi, na TMA is a war college, the only thing people talk there is war and its killing machines, so stop the non sense.
 
none sense!

kwani lazima ajira upate JWTZ?mbona zamani ilikuwa sio ishu?kwanza jeshini watu hawaajiriwi,wanaandikishwa!ndio maana hakuna barua ya ajira wala hawasherehekei may mosi!Kama unatafuta maslahi nenda Geta Gold Mine,period.
"army can do without u,either u r educated or not"
 
Back
Top Bottom