Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

tusiwe na mtazamo finyu wana jf, waislamu hawawezi kuunda mahakama ya kadhi bila kupata muafaka wa serikali na hasa wa kisheria kwa sababu tayari zipo sheria ambazo zinasimamia makosa ambayo mahakama ya kadhi inatakiwa kusimamia. Kama mahakama ya kadhi itatokea kuhukumu kesi ambayo sheria ya nchi nayo inahukumu tofauti huoni kutakuwa na mkanganyiko wa maamuzi. Vilevile kuwepo kwa mahakama ya kadhi kutahitaji kubadilishwa/kurekebishwa kwa vifungu vya sheria za mirathi na ndoa ili waislamu zisiwaguse. Haitajuzu kwa muislamu mmoja kutawaliwa na sheria za nchi halafu na tena sheria za kiislamu. Tujadili kwa busara

raisi ashatoa maamuzi-huu mjadala unatakiwa kufungwa
 
Edward Teller: Una wazo linaloonekana kuwa zuri. Lakini ili lijadilike tunaomba mifano mizuri mitatu tu kama kielelzo cha hoja yako. Nijuavyo, maamuzi ya msingi ya kiislamu yanatambuliwa na serikali pale inapohusu watu ambao wanakubali kuwa ni waislamu, yaani wahusika wote ni waislamu hai ukiondoa masuala mengine kama ya kukashifu dini ya mtu mwingine haijalishi kuwa wote wahusika ni wa dini moja.

Hata hiyo mahakama ya kadhi ya serikali kwa waislamu ikiwapo, bado mahakama ya serikali ina nafasi ya kushughulikia mashauri ya dini.
Mfano kwa wakristo pale mke aliyeolewa kikristo anaomba talaka kwa sababu mume ameoa mke wa pili (bila shaka kwa makosa serikalini au kimila). Kama kanisa halimpi talaka mke huyu basi anaweza kwenda serikalini kwa sababu mwenzie si mkristo hai tena kwa kutokufuata sheria za kikristo. Hii ni kwa sababu dini haina uwezo wa kukaza utekelezaji wa sheria kwa muumini ambaye si hai. Mfano mwingine ni pale muumini anapobadili dini, hayo mambo mengine ya kidini yatokanayo na mwingine kubadili dini unayaamua na kuyatekelezaje kidini mbali na kumfukuza mumini katika dini husika lakini tatizo linabaki pale pale kwa mulalamikaji?
 
Islamic is a backward revolution, don't waste much of your time reasoning, wao wanafikiria kugawiwa pesa bila kuwajibika, kuzaana ovyo ovyo wake wannewanne ili percentage yao TZ iwe kubwa kuliko dini zingine, na mwishowe wanakosa chakula wanatupiana majini na kuuwana kugombea u-Sheik, u-Immam wa miskiti na vitu vingine vidogovidogo! Rais at least aliwaambia vizuri ila hakuchoma sawasawa mie nakazia 'Tafuteni na ninyi namna ya kupata taasisi mkiweza tumieni hela mnazopata za misaada kujijenga, sisi tunajenga shule wenyeye nyiye mkipewa mnaharibu kabisa watu wa kufa nyinyi! Angalia Kidatu, halafu wanategemea tu misaada ya serikali. Fanyeni harambee, muendelee kila mtu anaweza! acheni fitna , ati mnataka wengine wanyan'ganywe siyo mpewe ninyi bali tukose wote!
 
  • Kuandamana usiku na mchana kushinikiza Mahakama ya Kadhi
JUMUIYA ya Taasisi za Kisilamu, imesema utatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kwamba hatua hiyo inakuja baada ya kushindikana kwa njia ya kidiplomasia, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Hayo yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Shehe Issa Ponda, alipokuwa akisoma tamko la msimamo wa Taasisi za Kisilamu kufuatia kauli ya Rais Kikwete katika Baraza la Idd el Fitri, lililofanyika Septembe mosi mwaka huu mjini Dodoma, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Shehe Ponda alizitaja taasisi zilizokutana na kuazimia kutoa tamko hilo kuwa ni pamoja na Baraza Kuu, Jopo la Mashehe, Baraza la Vijana wa Kiislamu na Basuta.

Soma zaidi hapa Waislamu sasa kuandamana kushinikiza Mahakama ya Kadhi
 
JUMUIYA ya Taasisi za Kisilamu, imesema utatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kwamba hatua hiyo inakuja baada ya kushindikana kwa njia ya kidiplomasia, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo. Hayo yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Shehe Issa Ponda, alipokuwa akisoma tamko la msimamo wa Taasisi za Kisilamu kufuatia kauli ya Rais Kikwete katika Baraza la Idd el Fitri, lililofanyika Septembe mosi mwaka huu mjini Dodoma, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Shehe Ponda alizitaja taasisi zilizokutana na kuazimia kutoa tamko hilo kuwa ni pamoja na Baraza Kuu, Jopo la Mashehe, Baraza la Vijana wa Kiislamu na Basuta. Alisema, baada ya kukutana wameamua kutoa tamko la kupinga hotuba ya Rais Kikwete na kwamba hatua hiyo imetokana na kutokubaliana na baadhi ya vipengele vilivyomo katika hotuba yake kuhusu kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

“Moja ya vipengele vilikuwamo katika hotuba yake (Rais Kikwete) ni kwamba Serikali haitaanzisha Mahakama ya Kadhi na kwamba badala yake Waislamu wenyewe ndiyo waanzishe mahakama hiyo. Hii moja inonyesha kutokukubaliana juu ya kuanzishwa kwa mahakama hiyo,” alisema Shehe Ponda. Alisema hakuna mahakama yoyote inayoweza kuanzishwa ikiwa nje ya dola na kwamba vinginevyo mahakama hiyo haitakuwa na nguvu katika kutekeleza majukumu yake.

“Lakini pia Jumuiya ya Taasisi za Kislamu, inapingana na kifungu cha pili na cha tatu cha hotuba kwamba Mahakama ya Kadhi haitowekwa ndani ya katiba, jambo linalomaanisha kwamba haitakuwa na nguvu kama ilivyo kwa mabaraza ya Kiisilamu ambayo yamesajiliwa kwa utaratibu wa kawaida lakini hayana uwezo wa kisheria,”alisema Shekhe.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Jumuiya za Taasisi za Kiislamu, Ramadhani Sanze, alisema njia pekee ya kudai haki ya kutaka kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi hapa nchini ni kufanya maandamano ya usiku na mchana ili kilio cha Waislamu kiweze kusikilizwa. “Wasilamu hawawezi kukubali kuona haki yao ya msingi ya kutaka kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi haipatiwi majibu sahihi, Kumekuwa na maneno mengi ya kuzungushwa kuhusu undwaji wa chombo hiki muhimu ambacho tunaamini kitasaidia kupunguza matatizo ya Waislamu,” alisema Shehe Sanze.

Alielezea kushangazwa kwake na kauli ya Rais Kikwete kwamba mahakama hiyo, itanzishwa na Wasilamu wenyewe.Alisisitiza kuwa waumini wa dini hiyo, wanaamini kuwa hakuna mahakama yoyote inayoweza kuwa na nguvu kama itakuwa nje ya dola. “Kauli ya Rais Kikwete inaashiria kwamba hakuna uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, mahakama yoyote haiwezi kuwa nje ya chombo cha dola vinginevyo, haitakuwa na nguvu za kisheria,” alisema Sanze.


Source: Mwananchi
 
bahati nzzuri sisi waislam linapokuja swala la kudai haki zetu za msingi hatuogopi kupigwa , wala kufa ikibidi... kitaeleweka tu,
U r warmly welcome! Hivi mkiwa mnaandamana mnafanya uhalifu? Kama ni kupita tu barabarani, be our guests!
 
Hatujakataliwa tumeambiwa tuanzishe... Kwa hio tuipe kazi kamati ..KUANZISHA..Serikali haiwezianzisha maana haina dini...
 
kwa kijana uliechangia hapa ikishaanzishwa hiyo mahakama then what? unahisi kunaulazima wakushinikizwa kwenda kuandamana? je ikiwa chini ya dola wewe inakusaidia nini? ANGAZA NJIA PANGA SAFARI ZAKO KATAFUTE MKATE WAKO WA KILASIKU.
Nawasilisha
 
andamaneni mkimaliza mtatuambia, mi nashangaa sana huyo anaepgania mahakama ya kadhi hata iliyopo hajawah kuitumia,
Hii ni tatizo la matumizi mabaya ya iman za dini,
Mkisha andamana mna mlazimisha nani kuwapa mahakama kadhi?
Mkisha andamana usiku na mchana viduka vye2 vibakie vizima wala hamtazinguliwa na m2,
Serikali iliweka wazi,swala hlo ni kidini zaidi serikali haitahusika zaidi ya kutoa ushirikiano ili kujiridhisha uundwaji wake.
 
Back
Top Bottom