Mdondoaji, Labda nianze na hii Quote yako:
Sheria ya mirathi ya Tanzania inayotambuliwa na serikali inaruhusu watoto wote (ndani ya ndoa na nje ya ndoa) wapewe urithi sawa. Kigezo kinachotumika ni kwamba hao watoto wanatambulika kuwa watoto wa marehemu (mzazi wa kiume) asili ya sheria hii ni ukristo
Unaposema asili ya sheria hii ni ukristo una maana gani? Kwani wakristo wanaruhusu watoto nje ya ndoa? Mkristo anatakiwa awe na mke mmoja na definetelty watoto wa ndani ya ndoa tu. Kama sheria hii ina mapungufu usisingizie wakristo. Dini ya kikristo hairuhusu watoto nje ya ndoa, hata Isack hakurithi pamoja na Ishmael!
Na sasa hii:
Tatu tunapogusia Common Law na Canon Law kuna sheria mama zinazodaiwa ni secular laws na sheria akisi zinazoendana na huduma ya kiroho. Hizo unazizungumzia ni sheria akisi zinazoshabihiana na huduma ya kiroho nitakupa mfano wa sheria za kikristo zinazojumuishwa katika kile kinachodaiwa ati sheria za secular mfano sheria ya ndoa mke anayetambulika kiofficial ni mke mmoja
Ninavyofahamu cheti cha ndoa cha serikali kinatambua ndoa ya wake wengi na kuna 'Provision ya kujaza kama ndoa ni ya wake wengi au mke mmoja. Usichanganye suala hili na zile stahili za mfanyakazi, maana hata watoto wanaostahili huduma za mwajili ni wanne tu, tena ambao hawajazidi 18yrs. AU watoto 4 ni huduma ya kiroho ya wakristo? Hii haimaanishi watoto zaidi ya wanne hawatambuliwi na sheria za Tanzania. La hasha, ni policy za bajeti tu. Yaani unapewa safari ya kikazi ya wiki 3 unende na wake 4? Gharama hizi alipe nani? Wewe chagua yeyote na mwingine zamu ijayo kama mnavyofanya kwenye unyumba.
Na isue ya mwisho ni kwamba kuna makundi ya watu wengi wanashugulika sana kutatua migogoro mbalimabi katika jamii kama ya ardhi, mirathi, ndoa n.k mfano, mabaraza ya ya wazee wa kijiji, watumishi mbalimbali wa kiroho n.k sasa tukisema hawa wote nao walipwe sababu nao wameamua kesi mbalimbali tutakuwa na mfumo gani wa serikali? Naamini mashehe au Wachungaji wanapoamua kesi, hawafanyi hivyo kama sehemu ya ajira bali bali kama sehemu yao ya kumtumikia Mungu
Ndugu,
Kwanza naanza kukujibu watoto wa nje ya ndoa tunakubaliana kwamba sheria ya mirathi ya serikali na sheria ya mirathi ya kiislamu zinatofautiana? Kama ni hivyo basi kwanini sheria ya mirathi ya serikali inatumika kuhukumu waislamu even though mhusika mwenyewe hakupewa ruhusa ya kuchagua. Pili hata anapochagua hakuna wa kuhukumu zaidi ya jalada kupelekwa store mpaka baada ya mashauriano. Wanaotoa ushauri ni masheikh ambao hawalipwi kitu na hivyo hiyo sio huduma ya kiroho bali NI HUDUMA YA KISHERIA!!!!.
Pili tukirudi kwenye huduma za kiroho kama ni hivyo pia wachungaji wanapotoa huduma ya elimu na afya kwanini isiwe ni sehemu yao ya kutumikia mungu. Badala yake wanasubiria cheki ya Billioni 600 walipwe kwa kuisaidia serikali kutoa huduma mbali mbali za jamii. Billioni hizo zinatoka katika jasho langu ambapo mimi muislamu sifaidiki na chembe moja ya the so called huduma ya jamii. Kutoa elimu na afya ni sehemu ya kumtumikia mungu. Au kwa wakristo ni wajibu serikali kutoa pesa kwa waislamu sio wajibu bali ni sehemu ya ruzuku.
Tatu umezungumzia kuhusu cheti cha ndoa kaisome sheria ya ndoa ya mwaka 1970 inasema hivi nanukuu :-
Section 10 par 2 ,
A marriage contracted in Tanganyika, whether contracted
before or after the commencement of this Act, shall-
(a) if contracted in Islamic form or according to rites recognized by
customary law in Tanganyika, be presumed, unless the contrary is
proved, to be polygamous or potentially polygamous; and
(b
) in any other case, be presumed to be monogamous, unless the
contrary is proved.
Why should the law assume my marriage is monogamous while I am a muslim irrespective whether I have declare it in marriage or not na kama tumeoana kiserikali. (what is the right of justice to a muslim who is a Tanganyikan). Huu ni ukristo kulazimishana ndoa isiyonihusu. Pili why is Islamic Laws are grouped together with customary laws while Christianity laws are incorporated in a secular Laws???
Pia ndani ya Marriage Act of 1970 wanasema hivi nanukuu:-
32. It shall be the duty kadhis and registration (a) of every kadhi or registration officer to whom notice has been
officers given that a marriage is intended to be contracted in Islamic form; and to attend marriages
(b) of every registration officer to whom notice has been given that
a marriage is intended to be contracted according to rites
recognized by customary law,
so far as is reasonably practicable, to attend that marriage.
33.-(1) When a marriage has been contracted in the presence of
a district registrar or kadhi or celebrated by a minister of religion, the
Issue of
marriage
certificate or
transmission
of
statement of
particulars
district registrar, kadhi or minister, as the case may be, shall forthwith
complete in duplicate a marriage certificate in the prescribed form
and sign the same and cause it to be signed by the parties and by two
witnesses to the marriage and shall hand one part to the parties and
retain the other.
(2) When a marriage has been contracted in the presence of a
registration officer, he shall forthwith complete a statement of particulars
relating to the marriage in the prescribed form and shall sign the same
and cause it to be signed by the parties and by two witnesses and
shall send the same to the district registrar, if the marriage was contracted
according to rites recognized by customary law, or to the kadhi, if the
marriage was contracted in Islamic form.
Section 32, 33 inaonyesha kuna registration officer na kadhi (whom kwa mujibu islamic sharia hayupo anakuwa replaced na sheikh wa mtaani). Registration officer wa ndoa analipwa mshahara na serikali ila sheikh wa mtaani hiyo ni huduma ya kijamii hebu nifafanulie haki iko wapi?
Pia ukiendelea ndani ya marriage act hiyo hiyo Divorce section 99 inasema hivi nanukuu:-
"99. Subject to the provisions of sections 77, 100 and 101, any
petition for
separation or married person
may petition the court for a decree of separation or
divorce on the ground that his or her marriage has broken down.
but no decree of divorce shall be granted unless the court is satisfied
that the breakdown is irreparable."
Nikuulize court gani itaamua kesi ya marriage ya muislamu??? Islamic laws zinasemaje kuhusu separation of marriages, reconciliation, dispute. Wanandoa wakienda mahakamani wanahudumiwa na mahakama kuhusu ndoa zao je nikuulize waislamu sio walipa kodi nchi hii na kama ni walipa kodi basi kwanini watu wanaoshughulikia ndoa zao, mirathi na HUDUMA ZENGINEZO ZA KIJAMII (kama wanavyodai maaskofu) wasilipwe??? Namalizia na speech aliitoa JK alipokuwa akifungua usharika mmoja Mwanza huko alisema hivi namnukuu:-
"Serikali itaendelea kutoa ruzuku kwa hospitali na zahanati za Kanisa lenu ambazo tuna Mkataba wa Huduma (Service Agreement)"
Swali ni Kanisa linataka nini ruzuku from the Government wakati ni sehemu ya huduma yao ya kiroho??? Kama ni kwasababu wanaisaidia serikali kutoa huduma katika jamii basi Mahakama ya kadhi nayo itagharamiwa na serikali kwasababu kodi yangu wanayoichukua kila mwezi,kodi ya muislamu mwengine au akina Bakhressa, Manji na wengineo ziende kuhudumia huduma ya kisheria kwa waislamu huu si udini mkuu ni haki ya msingi ya waislamu nchini Tanzania as simple as that. Mahakama ya kadhi inatoa huduma ya kisheria kwa wananchi hivyo wanahitaji kodi zetu waislamu.