Kwanza natoa shukurani zangu kwa wana Jambo kwa maoni yao . Kuhusu swala la kadhi maoni yangu ni kua katika haki za raia moja wapo ni haki ya Imani yake, sasa Serikali ina wajibu wa kuheshimu haki hiyo kwa raia zake na huku ikihakikisha kua haki hiyo haitumiwi vibaya, sasa mimi naona sio haki wala jambo la busara kuhukumu jambo kabla hata hilo jambo halijafanya kazi zake , la muhimu ni kua Serikali itafakari na kulitazama kwa kina na kuweka sheria ambazo zitakua na manufaa kwa wenye Imani hiyo BILA kuhatarisha au kuharibu haki za wenye Imani tofauti, maana haki ya kuabudu ni ya kila raia bila kuhatarisha haki za wengine, na katika kila Imani kuna sheria zake sasa kuamini bila kufuata sheria zake inakua Imani haijakamilika .
No one is above the law😕
Ni ushauri mzuri sana Sindbad. Mimi nakumbuka katika hotuba ya Rais wetu Kikwete kule Dodoma, hakukataa kuwepo kwa mahakama ya Kadhi kwa ajili ya Waislamu, alichokisema ni kwamba inakuwa vigumu mahakama hiyo kusajiriwa na Serikali. Aliwashauri Waislam kuianzisha mahakama hiyo wao wenyewe kama Waislam na siyo kupitia Serikali ya Tanzania.
Tatizo kwa Waislamu ni kwamba, taratibu za mahakama hizo kisheria ya Kiislamu inatakiw kuwa ndani ya Serikari na isimamiwe pia na Serikari. Chanzo cha haya yote nadhani ni kwa sababu, nyakati za Mtume Mohamad dola karibu zote ulimwengu alizozishika zilikuwa chini ya utawala wa Kiislam. Kutokana na hali hiyo, ilikuwa ni rahisi Serikali kwa upande wake katika mahakama zake kuwepo pia na mahakama ya Kadhi. Kulikuwa hakuna mgogoro kwa sababu Taifa zima lilikuwa ni kama la Kiislam kama ilivyo kwa upande wa Unguja na nchi za Kiislam [Iran, Iraq, Yemen, Afghanistan, n.k.
Kenya, Afrika ya Kusini , na nchi kama hizo ambazo zina mahakama ya Kadhi, sidhani kama mahakama zake zinafanya kazi kama ambavyo Uislamu wenyewe unahitaji.
Nionavyo mimi ni kwamba, Waislamu wawe wavumilivu katika hili kwa sababu historia ya mahakama hii ya Kadhi haikuwa ivyo nyakati zake wkati ina-apply. Wakubali mabadiliko ya mazingira ya sas japo katika dini haikubaliki kuchakachua
ili kuondoa mingongano inayoweza kujitokeza ambayo ni hatari zaidi kuliko mahakama yenyewe.
Waislamu tukiwa na subira, hata hao tunaodhani kuwa ni makafiri wataweza kuupenda Uislam wetu
na pia hata mbele za Mungu tutakuwa tumefanya jambo jema.
Mazingira ya nyakati hizi za imani nyingi tofauti katika Taifa moja, yanalihukumu jambo hili la mahakama ya Kadhi.