Jamani tunapo jadili jambo hili naomba tuelewe kuwa hakuna anaye kataa mahakama ya kadhi isiwepo hata mmoja,
Kinacho leta utata ni ile waislamu kutaka mahakama hii iendeshwe na serikali kwasababu tu eti Kenya na Uganda zipo na sijui kuna ubalozi wa Vatican nchini na hoja zingine zisizo na mashiko
Hoja ya Vatican ina mashiko kama iliyo hoja ya mahakama ya kadhi kwasababu kigezo mnachojidai kukileta ni kwamba serikali haina dini. Hebu soma habari hii na ujiulize maswali niliyoyaweka katika mabano kwa rangi ya bluu.
Vatican yamvua jimbo Askofu
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 5th June 2009 @ 16:00 Imesomwa na watu: 23173; Jumla ya maoni: 54
[TABLE="width: 310, align: right"]
[TR]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 98%, align: right"]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]Habari Zaidi:[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: Marquee"]Mpangaji NHC 'aingia mitini' na deni la mil. 42/-
Maghembe apigia debe kilimo cha muhogo
Jaji- Serikali inapendelea Bunge, haijali Mahakama
Kikwete ateua wakuu wa mikoa wapya 15
Waliokufa Zanzibar wafikia 203
Kortini kwa kumkeketa bintiye mwenye mwaka 1
Wavamia kampuni ya ujenzi, wapora mali
Kijana auawa akituhumiwa kuiba baiskeli
NHC yakanusha tuhuma za kuwabagua wapangaji
Mbowe kusomewa shitaka la shambulio
KKKT yasaidia waathirika wa meli iliyozama
NHC yawatimua Bob Makani, Tughe
Ndege yaanguka shambani
Wakimbizi waliotolewa rumande wachunguzwa
Barrick Canada yatoa mil. 37/- za karo ya wasiojiweza
Waliodakwa na bangi wafungwa jela miaka 10
Bilal achangisha mil.158/- kujenga maabara Duce
Japan yatoa mbolea ya bilioni 8/-
Maiti ajali ya meli waonekana ufukweni Mombasa
Vyama vya waandishi vyapata bilioni 8/-
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]
[TABLE="width: 98%, align: right"]
[TR]
[TD="class: kaziBody"]Habari zinazosomwa zaidi:[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: Marquee"]Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Balaa lingine kwa Chenge
‘Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Vatican yamvua jimbo Askofu
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Vatican nchini Italia yamemnyang'anya Jimbo, Askofu wa Same, Jacob Koda, baada ya kubainika kukiuka mafundisho ya imani ya kanisa hilo ( Kumbe Vatican ndio wanaajiri maaskofu wa waumnini kanisani??? Sasa inakuwaje nchi nyengine iajiri watumishi wa kiroho nchini kwetu? Mbona waislamu hujasikia sheikh ameletwa kutoka Saudi Arabia au ameajiriwa na serikali ya saudi arabia?). Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Joseph Chennoth alithibitisha Dar es Salaam jana kuwa Askofu Koda ametakiwa na kanisa kuacha utume huo mara moja na kupumzika ama kufanya shughuli binafsi za mafunzo.
Hata hivyo, Balozi huyo wa Papa hakufafanua zaidi kiini cha kuondolewa kwa Askofu Koda na ni mafundisho gani ya kanisa aliyokiuka, ingawa taarifa kutoka Same zilizolifikia gazeti hili jana zilidai kuwa amejiingiza katika mafundisho yaliyo kinyume cha imani ya Kikristo na ya Kanisa Katoliki.
Sambamba na kuondolewa Askofu Koda katika jimbo hilo lililoko mkoani Kilimanjaro, pia taarifa ya Askofu Mkuu Chennoth kwa vyombo vya habari jana ilieleza kuwa Baba Mtakatifu Benedicto wa XVI amemteua Padri Rogath Kimaryo kuwa Msimamizi wa Kitume wa jimbo hilo hadi hapo litakapopata askofu mwingine. (This is the argument of Professor Geoffrey Robertson how can a head of state of one nation appoint a religious leader of a constituent in another country??? Inakuwaje rais wa nchi au kiongozi wa nchi anateua kiongozi wa kiroho katika kijisehemu cha nchi nyengine??)
Padri Kimaryo kabla ya uteuzi huo alikuwa Paroko wa Parokia ya Kipawa, Jimbo Kuu la Dar es Salaam. "Tumemshauri kuondoka jimboni na Padri Kimaryo ataongoza jimbo hilo kwa muda mpaka hapo Baba Mtakatifu atakapomteua askofu mpya," alisema Askofu Mkuu Chennoth.
Aidha, taarifa hiyo ya Ubalozi wa Vatican hapa nchini kwa vyombo vya habari iliyotolewa kwa gazeti hili na Katibu Mtendaji wa Habari wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Revocatus Makonge, ilithibitisha uteuzi wa Padri Kimaryo katika jimbo hilo la Same.
"Mwakilishi wa Baba Mtakatifu hapa nchini anayo heshima kutangaza kuwa Baba Mtakatifu Benedicto wa XVI amemteua Padri Rogath Kimaryo (CSSP) (Nani mwakilishi Pope Benedict nchini Balozi wa Vatican City au Askofu mkuu wa kanisa katoliki nchini? Isitoshe inawezekana vp balozi wa nchi nyengine apewe power ya kuteua viongozi wa kiroho nchini kwetu? Ushasikia Saudi Arabia imetoa tamko kupitia balozi wake kuwa sheikh wa ilala hafai???? Hizi ndio arguments za maprofessor Robertson and Tiggs are asking na mie nawaulizeni wanazi wa Vatican nchi). ambaye ni Paroko wa Kipawa, Dar es Salaam kuwa Msimamizi wa Kitume mwenye mamlaka kamili na chini ya utii kwa kiti kitakatifu wa Jimbo Katoliki la Same," ilieleza taarifa hiyo iliyotolewa Mei 30, mwaka huu. Hata hivyo, Padri Makonge alisema TEC haina taarifa zozote za kina kuhusu suala hilo na kueleza kuwa wanachofahamu ni uteuzi wa Padri Kimaryo kupitia taarifa hiyo ya Mwakilishi wa Papa nchini.
Taarifa zaidi kutoka katika ofisi za Ubalozi wa Vatican Dar es Salaam zilieleza kuwa Padri Kimaryo atakabidhiwa jimbo hilo kwa usimamizi rasmi kesho katika Ibada ya Misa itakayoongozwa na Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo katika Kanisa Kuu la Same na kuhudhuriwa na viongozi kadhaa wa kanisa hilo akiwamo Askofu Mkuu Chennoth.
Bila kufafanua zaidi, Askofu Mkuu Chennoth alisema Kanisa Katoliki huwa lina utaratibu wa kumteua Msimamizi wa Jimbo linapotokea hitaji kama hilo hivyo ni kitu cha kawaida ndani ya kanisa pindi panapoonekana umuhimu wa kufanya hivyo.
Askofu Koda aliteuliwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II kuwa Askofu Mpya wa Same Septemba 1999 (Hivyo na sisi waislamu tuteuliwe Mufti kutoka Saudi Arabia) kuchukua nafasi ya Askofu Josephat Lebulu aliyehamishiwa katika Jimbo Kuu la Arusha.
Padri Kimaryo ambaye ni Padri wa Shirika la Roho Mtakatifu alitunukiwa Udaktari wa Sheria nchini Roma katika Chuo Kikuu cha Pontifical Gregorian na pia amefanya kazi ya kitume kama mshauri kwa miaka sita katika nyumba yao ya shirika nchini humo.
Kwa utaratibu wa Kanisa Katoliki, Papa humteua Msimamizi wa Jimbo ambaye kikanisa ni kama Mtawala ambaye hufanya kazi hiyo, mara kadhaa hutumikia katika eneo ambalo halijapewa hadhi ya Jimbo au katika Jimbo lisilo na Askofu au tatizo kama lililotokea. Katika sheria za kanisa (Canon Law), utawala wa aina hiyo unampa mamlaka mtawala kufanya kazi zote za kiaskofu isipokuwa kuuza mali yoyote ya jimbo na kutoa daraja la upadrisho.
Source: Habari Leo.
Kisomi na kitaaluma ya kisheria na kifalsafa haingii akilini kabisa hizi argument zenu kuwa serikali haina dini. Naomba mnijibu maswali hayo hapo juu tuone ni akina nani waropokaji na nani wako makini kihoja. Hivyo basi kumbe serikali inaweza ikapinda katiba kuruhusu ubalozi wa Vatican City uwepo nchini ila kuruhusu mahakama ya kadhi ambayo haina tatizo lolote kikatiba isiwepo nchini. Sitaki kusema zaidi nafikiri mwenye akili ataelewa asiye nazo ataendelea kuelewa anavyotaka mwenyewe.