Just in: UDSM wafukuzwa

Just in: UDSM wafukuzwa

Mzee ES anasema wanafunzi kwenye vyuo vya serikali hawaruhusiwi kugoma. Hakuna kitu kama kuruhusiwa kugoma. By definition, kugoma ni kitu kinafanywa bila ruhusa. Kikipata tu ruhusa kinaacha kuwa mgomo.

Kugoma, kufanya vurugu, au kususia masomo, ni njia ya kawaida ya wanafunzi dunia nzima, ya kutaka haki itendeke. Binafsi, nilikuwa kwenye mgomo nikiwa mwaka wa pili UDSM, na nikawa kwenye makundi ya wanafunzi yaliyofanya vurugu kubwa kwenye vyuo vikuu Canada kudai disinvestment from the then Apertheid Regime in SA.

Waalimu wa vyuo vikuu Kenya waligoma siku za karibuni, na hata waalimu wa UDSM wangegoma kama serikali haingeboresha mishahara yao.

Wanafunzi wa UDSM walikuwa na haki ya kugoma kudai serikali iwape support 100% Wengi wao wanatoka kwenye familia masikini ambazo haziwezi kulipa malaki ambayo JK anataka walipe. Ni sawa wanavyogoma wote. Huyo anayesema ilibidi wale wasio na uwezo tu ndio wagome hajui asemalo. Nguvu ya mgomo inatokana na umoja.

Tatizo sio kukosekana fedha, ni fedha kutumika vibaya. Hatutaki elimu a vyuo vikuu iwe ni kwa ajili ya watoto wa matajiri tu.

Watu walioko kwenye disciplined forces peke yao ndio hawana haki kugoma. Wengine wote tuna hiyo haki. Mara nyingi, ndiyo namna pekee ya kuwashinikiza wakubwa.
 
philemon ndio maana uko hivyo kumbe migomo imo kwenye spiritual mood yako
 
Mimi nilisoma pale UDSM na baadaye kufundisha pale. Nikiwa mwanafunzi tuliendesha "KUNJI" kali sana dhidi ya utawala wa Kuhanga ("Octopus") hadi tuliposikilizwa na baadaye maombi yetu kutekelezwa. Mgomo ule ulilazimishwa na ahadi hewa tulizokuwa tumepewa kwa term mbili mfululizo bila utekelezaji wowote. Baada ya kuitisha kunji lile, tulifanikiwa kukutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu ya Juu ambaye aliahidi kuwa kama maombi yetu yasipoketekelezwa katika muda fulani tuitishe kunji tena na kumsuta. Nakumbuka kuwa tatizo lile lilitatuliwa mara moja.

Wakati nikiwa nafundisha pale, wanafunzi waliweka kunji lingine ambalo lilikuwa limesababishwa na bajeti ya wakati ule kutokuwa imeweka vitu ambavyo vilikuwa vimeahidiwa kwao ndani ya prospectus; nadhani serikali walitaka kubadilisha rules of the game on the fly. Nakumbuka kuwa Kunji lile lilikuwa la nguvu sana na ndilo lililosababashwa Chancellor wa wakati ule Rais Mwinyi ("Mzee Jangala") aamue kufunga chuo kwa mwaka mzima na kujivua Ukuu wa chuo kuanzia hapo.

Uzoefu wangu wa zaidi ya miaka kumi pale mlimani unaonyesha kuwa wanafunzi huwa wanasita sana kufanya migomo kwa vile wote huwa wamefokasi sana kwenye masomo yao kutokana na kuzungukwa na tishio kubwa la "kudisko." Migomo yote ya pale chuo Kikuu husababishwa na ama uongozi wa chuo au serikali kutotimiza ahadi zake kwa wanafunzi, na mara zote huwa ni ahadi ambazo zinaweza kusabababisha mazingira ya kujifunza kuwa magumu kwa wanafunzi, jambo ambalo linatishia sana uhai wa wanafunzi hao kutokana na zimwi la "disko."

Kwa hiyo watu wanaweza kuwapa majina mbalimbali hawa watoto, ukweli ni kuwa serikali inachangia sana kuweka fujo za aina hii vyuoni. Pamoja kuwa hawa wanafunzi ni watoto, siyo kweli kuwa huwa wanafanya migomo hiyo bila kujua hatima yake, la hasha: wanakuwa wamelazimika.
 
mzee kichuguu
nnaamini unahifadhi mchwa na nguchiro bila mkwaruzano
kuna hili jina la mzee mwinyi kuitwa jangala, kwangu ni jipya unaweza kunipa reason behind scene? mana nnajua anaitwa mzee rukhsa pale aliporuhusu watu waaabudu dini watakayo bila ya kuvunjas amani

kima sitokukwaza nnaomba elmu kidogo
 
Kama zilitolewa 111.3bn/= kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi, basi mahesabu yako hivi: Ukizigawa kwa wanafunzi elfu 40, kila mmoja anapata karibu shilingi milioni 3 (2,782,555/= to be exact). Kama unazigawa kwa wanafunzi elfu 30, kila mmoja anapata karibu shilingi milioni 4 (3,710,000/= to be exact).

Hii mikopo ni kwa ajili ya wanafunzi wangapi? Kila mmoja alipata kiasi gani? Au hizi fedha zinaliwa wizarani?

Augustine Moshi


mwalimu augustine,well said .maneno mazito haya..nilipoyasoma nimetafakari sana ,kweli kama BILLION 114 zimetolewa na wanafunzi wanolipiwa hawafiki au ni 30,000..na wengi hasa wale wa private univs wanalipiwa only part...na ukizingatia ada nyingi zinarange between 1.5 to3 million...nahisi kwamba kuna uchunguzi unahitajika...sijui kama CAG [MR UTTOUH] alipita huko ,BUT WE NEED THE ACCOUNTS AUDITED tena haraka sana,yawezekana mikopo mingi itakuja shindikana kurudishwa kwa kuwa panaweza kuwa na uwezekano wa kutoa mikopo kwa wanafunzi hewa....au mkopo ukawa zaidi ya kiwango anachostahili mwanafunzi kwa wakati huo.

nimesoma jana [guardian/nipashe] taarifa ambazo zitamsikitisha mzazi yeyote kuhusu baadhi ya wanavyuo waliokosa pesa za kujikimu au kurudi makwao kuripotiwa kuuza baadhi ya personal effect zao na vifaa vingine ,la kusikitisha mabinti zetu wanaingia viwanja [wanakula vichwa]...sasa kweli mnaweka mazingira ya kumfanya maskini huyu ajitahidi kumsomesha mwanaye aje kufa na UKIMWI mara tu baada ya kupata degree yake ,kutokana na ukata aliosababishiwa na serikali!!!!??? tuwe na hurumu...kuna baadhi ya watu kama kulikoni inanibidi nifikiri mara mbili ninaposoma tafakari zao ,ni kama vile hawajui taifa hili MASIKINI WANAFIKIA 80%.
 
mzee kichuguu
nnaamini unahifadhi mchwa na nguchiro bila mkwaruzano
kuna hili jina la mzee mwinyi kuitwa jangala, kwangu ni jipya unaweza kunipa reason behind scene? mana nnajua anaitwa mzee rukhsa pale aliporuhusu watu waaabudu dini watakayo bila ya kuvunjas amani

kima sitokukwaza nnaomba elmu kidogo


Mtumwitu,

Kwa vile sijalala, nitakujibu swali lako kwa hatua tatu kama ifutavyo:

(a) Pale Chuo Kikuu kulikuwa na Zimwi fulani linaitwa "PUNCH" lililokuwa linatundika victms wake ukutani. Hili Zimwi lilikuwa linawapachika majina ya ajabu ajabu victims wake. Kati ya majina hayo ni kama: Poacher, Octopus, Kuku wa Kishenzi, Mama Kijaluba, Mpingo, Hailali, Gigolo, Akili Hana, Makali Hodari, Mzee Jangala, na majina mengine ya ajabu ajabu.


(b) Miaka ya themanini kulikuwa na mchezo wa kuigiza redioni (RTD) uliokuwa unadhaminiwa na kiwanda cha pombe cha Kibuku. Mmoja wa characters wakuu katika mchezo ule alikuwa akiitwa "Mzee Jangala." Huyu mzee alikuwa mtu wa kubababsiha kila kitu akiwa hana uhakika na matokeo yake.

(c) Mwaka 1990 wakati watoto wale wa UDSM wanagoma, mzee Punch alimtundika rais Mwinyi ukutani na kumpachika jina na "Mzee Jangala." Wachunguzi wa mambo wanasema kuwa yule Panchi ndiye hasa aliyesababisha Mzee Mwinyi kufunga chuo kile indefinitely.

Nadhani sasa umeelewa.
 
mwalimu augustine,well said .maneno mazito haya..nilipoyasoma nimetafakari sana ,kweli kama BILLION 114 zimetolewa na wanafunzi wanolipiwa hawafiki au ni 30,000..na wengi hasa wale wa private univs wanalipiwa only part...na ukizingatia ada nyingi zinarange between 1.5 to3 million...nahisi kwamba kuna uchunguzi unahitajika...sijui kama CAG [MR UTTOUH] alipita huko ,BUT WE NEED THE ACCOUNTS AUDITED tena haraka sana,yawezekana mikopo mingi itakuja shindikana kurudishwa kwa kuwa panaweza kuwa na uwezekano wa kutoa mikopo kwa wanafunzi hewa....au mkopo ukawa zaidi ya kiwango anachostahili mwanafunzi kwa wakati huo.

nimesoma jana [guardian/nipashe] taarifa ambazo zitamsikitisha mzazi yeyote kuhusu baadhi ya wanavyuo waliokosa pesa za kujikimu au kurudi makwao kuripotiwa kuuza baadhi ya personal effect zao na vifaa vingine ,la kusikitisha mabinti zetu wanaingia viwanja [wanakula vichwa]...sasa kweli mnaweka mazingira ya kumfanya maskini huyu ajitahidi kumsomesha mwanaye aje kufa na UKIMWI mara tu baada ya kupata degree yake ,kutokana na ukata aliosababishiwa na serikali!!!!??? tuwe na hurumu...kuna baadhi ya watu kama kulikoni inanibidi nifikiri mara mbili ninaposoma tafakari zao ,ni kama vile hawajui taifa hili MASIKINI WANAFIKIA 80%.

Mwalimu (mtaalamu wa mahesabu) Moshi alitoa hesabu nzuri sana zinazoonyesha kuwa pesa ile inaliwa na watu wengine, halafu wanalaumiwa watoto wale. Kwa kweli imenisononesha sana kusikia kuwa mabinti wetu wamelazimika kutumiwa miili yao hovyo ili waondoke pale chuoni kwa muda mfupi ule. Hivi kweli nchi hii ni yetu?

Utashangaa kuwa wazazi wengi wa vijijini hawana watoto pale chuo kikuu kwa hiyo hawaoni wala kujua tatizo hili. Wakati wa kupiga kura utaona watavyopiga kura zao: 90%
 
Yes, serikali inawajibika moja kwa moja juu ya matatizo ya hao wanafunzi kwani wengi wao hawana uwezo na tukisema wafanyekazi wajisomeshe Kazi zenyewe ziko wapi? ikiwa wahitimu tu hawanakazi au vibarua je hao wanafunzi ndiyo watazitoa wapi hizo kazi au vibarua?Tusiseme tu kwasababu wengi wanaosoma nje ya nchi wanauwezo wa kujisomesha wanachopaswa kukumbuka uwezo huo umetokana na mazingira mazuri ya hizo nchi wanazosoma ya kuweza kuzalisha nafasi za kazi hivyo kutoa nafasi kwa mwenye shida ya kupata kazi kuipata.
 
philemon ndio maana uko hivyo kumbe migomo imo kwenye spiritual mood yako

moja ya njia ya mwisho rahisi kwa mtu yoyote kutetea kile anachoamini ni kugoma...na historia imeonesha kuwa hata viongozi wengi maarufu duniani,wamepata kuwa viongozi wa harakati mbalimbali ikiwemo mgomo

mwalimu nyerere alipata kushtakiwa ...mzee mandela alifungwa ...kenyatta na wengine ..migomo ,harakati, na maendamano ni jambo hatari kama serikali itakaa makusudi kusubiri migomo ndio wafanye kazi ...migomo / maandamano yameangusha dola zenye nguvu...kumbula ncholae chausesco na romani.kumbuka UKRAINE juzi..ets

tukirudi hapa kwetu migomo imekuwa kama kitendo cha kujihisi ushujaa kwa serikali yoyote ya wanafunzi inayoingia...uwezo wa kutatua matatizo ya wenzau ikibidi kwa migomo ni moja ya mafanikio ...ukiangalia nyuma utagundua migomo chuo kikuu imeanza tangu enzi ya kina JOSEPH WARIOBA ,PETER BAKILANA na wengine wengi,wote baadaye wamekuwa raia wema na wakutukuka tu,mgomo si uhaini...hawa walifikia kupigwa viboko na mwalimu na kurudishwa hadi vijijini walikotoka na kutakiwa kuripoti kwa wenyeviti wa vijiji WALISAFIRISHWA HADI VIJIJINI sio leo mnawaacha wanatangatanga MITAANI.pamoja na hayo nyerere alikuwa na ushujaa wa kujibizana kwa hoja na wanafunzi pale nkrumah[sio diamind] hadi wakamuelewa.

MIGOMO kipindi cha mwinyi iliandamana na dukuduku la kutaka mabadiliko ya vyama vingi ndo maana iliwazaa wanaharakati maarufu kama DR KIMARO[YUKO WAPI?},JAMES MBATIA , NAwengine wengi[kichuguu naomba tukumbushe viongozi wa ule mgomo maarufu]..huu ndio mgomo uliokomesha utaratibu wa rais wa nchi kama ilivyo kenya na uganda kuwa chancellor wa state university kwa hapa tanzania....mwiyi alishindwa kuwavumilia ...lakini kama sikosei na hawa walirudishwa kwa wazazi wao.hawakutelekezwa manzese wanye tapu tapu....

kwa hiyo tusiwahukumu vijana kwa kugoma hiyo ndio njia yao ya mwisho kama wanyonge kama wale mahabusu ets.. watu hugoma hadi kula..safari ijayo wagome kula[kiddin]
 
DR KIMARO[YUKO WAPI?},,


Huyu Kimaro sijui Kama alihitimu Udaktari wake Lakini alifukuzwa pale Muhimbili akiwa mwanafunzi wa mwaka wa nne alibakiza mwaka mmoja na miezi kadhaa kuhitimu Kama kumbu kumbu zangu ziko sawa kwani kichwa changu kinazunguka kati ya mwaka wa nne na watano.Na alikuwa na mke au Binti anaishi naye na alikuwa akisaidia ndugu zake kuwasomesha kwa kile kidogo alichokipata kupitia Allowance zake kadhaa kwa kweli ilkuwa pigo kwake na familia yake.Lakini Baadae nilipata tetesi kwamba Kina Mrema wakati huo akiwa NCCR mageuzi walimtafutia shule Zimbwabwe na kuendelea na masomo huko.Sasa sina uhakika alimaliza shule zimbwabwe au laah?Na kama alimaliza na baada ya kumaliza aliishia zimbwabwe au sehemu nyingine hili nalo sina uhakika nalo.Ila jamaa alikuwa mwana harakati mwenye msimamo wa hali ya juu na mweye uwezo wa kujenga hoja.
 
PM: MIGOMO kipindi cha mwinyi iliandamana na dukuduku la kutaka mabadiliko ya vyama vingi ndo maana iliwazaa wanaharakati maarufu kama DR KIMARO[YUKO WAPI?},JAMES MBATIA , NAwengine wengi[kichuguu naomba tukumbushe viongozi wa ule mgomo maarufu]..huu ndio mgomo uliokomesha utaratibu wa rais wa nchi kama ilivyo kenya na uganda kuwa chancellor wa state university kwa hapa tanzania....mwiyi alishindwa kuwavumilia ...lakini kama sikosei na hawa walirudishwa kwa wazazi wao.hawakutelekezwa manzese wanye tapu tapu....

Kimaro Alikuwa hapa UK na kupewa hifadhi ya kisiasa lakini aliamua kwenda kuishi Zimbabwe kwa Mugabe ambaye alimpa hifadhi na walinzi wa kumlinda pamoja na bastola Private hadi mwaka 2001. Alikuwa na contacts na wanasiasa wengi tu nchi za nje lakini baada ya hapo sina details. Kuna wakati wa BMW alipeleka maaskari kanzu kwenda kuchunguza alichokuwa anafanya. Alikuwa anaishi kwenye nyumba za madaktari wanafunzi Parirenyatwa Hospital kule Zimbabwe kutokana na reliable sources zangu. Walimchora Mzee Ruksa anabash*** (au kupigwa mti) na ba***.
 
Hatukatai wananchi kugoma, tunachokataa ni kugoma bila ya kuwa na sababu za msingi kisheria, na kutokuwa na justification mbele ya jamiii ya huo mgomo,

Tunasema kwanza zifuatiliwe njia zote za kisheria, ikiwa ni pamoja na kupitia ngazi zote zilizowekwa na taratibu za serikali, wanafunzi walitakiwa kwenda mkuuu wa chuo, kwa mkurugenzi wa elimu ya juu, naibu katibu mkuuu wa Wizara ya elimu, katibu mkuu, Waziri, waziri mkuu, makamu wa rais, then rais, baadaye mahakamani kuipinga hiyo sheria mpya, sasa ndio pafanyike mgomo maana njia zote za kisheria na hta kistaarabu zimeshindikana,

Mzee Moshi, hatuko kwenye business za ku-create taifa la wagomaji ndio maana kuwafukuza hawa wanafunzi ilikuwa ni sawa kabisaa, na pia hakuna elimu ya bure tena hapa duniani, no matter what somebody has to pay for kama ni serikali au wanafunzi, lakini one thing lazima ieleweke ni kuwa somebody has to pay for, no more free education, na wanafunzi wajifunze kutumia utaratibu wa kisheria,

No excuses, maana Mtikila alitumia njia hiyo hiyo ya sheria na kukubaliwa na mahakama ya ccm kuhusu wagombea binafsi kuwa srikali ina makosa kwa kuwakataa, na wanafunzi pia wanaweza kupitia njia hiyo ya sheria, badala ya migomo. Wakigoma watarudi nyumbani tu! Hatuwezi kamataifa kuwa-reward wagomaji!
 
kichuguu,
Matiko Matare, na James Bazigiza, waliishia wapi? Mzee Ruksa alitia aibu sana jinsi alivyoushughulikia mgogoro ule wa UDSM.
 
Mwalimu Wangu Kichuguu

Asieshukuru Wanaadamu Hawezi Kumshukuru Muumba Wake, Nnakushukuru Kwa Kunielimisha Kuhusu Jina La Jangala Lilipotokea.

Mzee Phile,
Nnategemea Mzee Es Amekutosheleza, Si Busara Kushabikia Kila Mgomo, Tushabikie Ile Migomo Ambayo Inastahiki Hasa Kufanyika, Hawa Watoto Wamechemsha Na Wala Haifanani Migomo Yao Na Ile Yenu Au Unasema Je Mzee Wangu Hapa?
 
hivi kama sikosei matiko alogombea ubunge mwaka 2000 kule kwao mara kwa tiketi ya upinzani,hata kama sio yeye kuna mmoja wa wale victims wa mzee rukhsa aligombea .... mtumwitu et al nimekusoma .....lakini kwani mkono wako ukishika mavi utaukata???? nini chanzo ,na nini suluhisho!? je tutaendelea kusubiri migomo kama ule wa mahabusu na huu wa vijana ndio tushtuke...
 
Mgomo wa mahabusu umewasaidia nini ndugu zetu huko mahabusu? Mbona Ditopile bado yuko nje, na kesi haitajwi tena?

Migomo haiwezi kubadili ukweli kuwa hakuna elimu ya bure tena duniani!
 
Hivi katika Tanzania yetu hatuna watu wanaoweza kukaa chini, kukuna vichwa na kuja na suluhisho la suala la elimu ya juu nchini? Itatolewa vipi, ni haki ya nani, kwa gharama ipi, na nani atalipia gharama hiyo na kwa nini? Hivi, kweli tunaweza kukubali kuwa hakuna watu ambao wanaweza kulikabili tatizo la elimu ya juu na kulitatua once and for all haswa suala la "tutalipia vipi gharama ya elimu ya juu"? Kama kuna mtu anaweza kunisaidia kuelewa serikali ilifikia fikia vipi uamuzi wa wanafunzi kuchangia asilimia 40 na siyo 50/50 au 15/85? kwanini 40%?

Au ndio hili la "tumekosa wataalamu wenye uwezo" tuombe msaada. Kama hatuna watu wenye uwezo wa kukabili matatizo na kuyatatua tuombe "wafadhili" wetu wafikiri kwa niaba yetu, waje na mapendekezo ya elimu ya yetu, na ikibidi wasimamie utekelezaji wa masuluhisho watakayopendekeza! Haiwezekani kila baada ya miezi/miaka michache wanafunzi wawe wana goma goma, such an environment is not conducive for imparting higher education!

Prof. Msolla, kama hamuwezi kufikiri, tutawasaidia!! for free!!
 
Mzee ES,

Hatusemi Elimu iwe bure. Wanafunzi wanadai wapewe mikopo ya kutosha kudumu gharama za Elimu. Hawasemi kusiwe na ada. Si vema kupotosha mambo.

Umetoa hatua za kupitia kabla mgomo haujakubaliwa. Nakumbusha tena kwamba mgomo hauhitaji kukubaliwa. Wahusika wote uliowataja walifahamu matatizo ya wanafunzi kabla ya mgomo, na hawakuyatatua. Wanafunzi walishaeleza, juu kabisa, kutoweza kwao kumudu ada za elimu ya juu bila mkopo wa kutosha. Walipewa ahadi na Rais kwamba hakuna hata mmoja wao atashindwa kusoma kwa sababu ya kukosa ada. It was a lie.

Taarifa za serikali ni kwamba zimeolewa 111.3 bn/= kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi. Mahesabu yetu ni kwamba hizo fedha zingetosha kuwapa wanafunzi elfu 40 mkopo wa 2,782,500/= (karibu milioni 3) kila mmoja. Hizo fedha zimekwenda wapi? Au serikali imedanganya kwamba imetoa hizo fedha wakati haijafanya hivyo?

Ningekuwa bado nafundisha UDSM ningetoa pendekezo kwa UDASA kwamba tugome kuishinikiza serikali ifafanue hizo 111.3 bn/= zimetumikaje, na iwarudishe wanafunzi na kutoa fedha za kufidia kufundisha vipindi vilivyopotea.

Augustine Moshi
 
Kama kuna mtu anaweza kunisaidia kuelewa serikali ilifikia fikia vipi uamuzi wa wanafunzi kuchangia asilimia 40 na siyo 50/50 au 15/85? kwanini 40%?

Uamuzi ulitolewa na World Bank, serikali yetu ikaufuata bila kufanya mchanganuo wowote kuona kama ilikuwa ni feasible katika mazingira ya watanzania.
 
Back
Top Bottom