Just in: UDSM wafukuzwa

Wadanganyika wameanza amka, tusichoke kupiga kelele[hata msolla akin'oka], JF imekuwa ni kisima, watu wengi wanachota humu na kuamsha isiha mitaani, mfano mzuri ni suala la Richmond hakuna magazeti yaliyochambua kama JF na watu wengi wamesoma humu.

Tuendelee kupiga kelele, huku tukiweka mkakati wa kelele hizi kusikiwa na watu wengi zaidi
 
We have to set standard! na sio fedha kuweka standard!..[/QUOTE]

Its so unfortunate but thats the case! Iam not sure how we can reverse this!
 
Mikuki,
Very unfortunate indeed!..
Yet, it is possible...'cause ignorance and selfishness has always been ahead of traits of an effective leadership. I sometimes wonder if we do have good leaders at all...
Our leaders do not have vision, structure or values and they are not accountable for anything!. They can't communicate, see forces and ecosystem, sythesize viewpoints e.t.c on the other hand we do have the society which is driven by the force of evil.... MONEY! - Again, always wonder if we were/are fit to have Independence!...

Where to start - At those schools!... next time around thing will be different. Not this generation but self-fulfilling prophesy will come from these schools. A new generation of leadership...2nd time around Independence.
I do hope this is a lesson learned!
 

....its true kwamba....chungwa huzaa chungwa!

hao watoto watakaosomeshwa...kwa pesa zipi...hizi za rushwa?,halafu wanajuwa wanasomeshwa nazo....hapo ilimu yake ni kuwa nao kesho wale hiyo ili wawasomeshe wa kwao!

barabara wanazopita ni zipi?hizi mbovu,tena kwa magari ya kifahari...kwahiyo deal hapo ni lipi?...kujenga barabara akishika madaraka au kununua gari kama hilo ili atese kwenye barabara mbovu?

babaye halimi vya kutosha hilo shamba...halafu anashinda klabuni,lakini chakula kinapatikana[subsistence],sasa...deal lipi, kuchoshwa na jembe au plau...au kuburudika komoni baada ya kazi ya kivivu?

babaye hakusoma...eti aliishia la pili....ila pesa anazo,si ana biashara ya ng'ombe....sasa,deal lipi....kwenda shule au kukuza mifugo na kuiuza na bado ukawa na fedha kuliko profesa!

mamaye alikuwa akiwafahamu wazungu ma-tx,yeye anakawaita uncle...amejenga,anakausafiri kazuri...pesa hazipigi chenga.....yeye kasomeshwa lakini uzalendo ukamshinda...kitabu hakilipi ka pale jolly's!

sasa,mi ntakwambia...tukifanyakazi tulizopewa[kwani,kusawazisha barabara za udongo tunahitaji grants toka china?]au kuziomba,tena kwa ufanisi na kama za kwetu binafsi[utamshangaa mtu akiwa na chake,cha wenzake aagh!]maendeleo yatapatikana.

ndio nakubali...tuache UBINAFSI!
 
DAR si LAMU,
nadhani tunachosema ni kwamba mabadiliko yanaweza kuanzisha ktk hizi shule!...hapa hatutaki kufuga kizazi hiki ambacho kinaweza leta matokeo kama uliyoyasema. Ni kizazi ambacho wewe na mimi tumekulia.. Kwa hiyo kama kuna mabadiliko basi yaanzie katika shule zetu.... ndiko iwe mlengwa wa somo lolote tunalojadili humu.
Hao ndio watakuwa viongozi bora zaidi ikiwa mabadiliko yameanza kwao wao!
 

maana yangu ni kuwa,tutawapeleka shule nzuri,lakini kama sisi wenyewe hatujajirekebisha na kuwajibika....watatufata nyayo zetu hawa!...na ndo litakalotokea....ilimu vitendo, maalim wangu.

kama unafundishwa halafu matendo hayo hayapo,haisaidii.

tutawaze kwanza,tujiondoe hii najsi halafu ndo tusonge mbele...itakuwa vicious circle tusiporekebisha.

ushan'fahamu maalim wangu?
 
tatizo moja ni hii imani tuliyonayo kuwa kwenda shule peke yake ni suluhisho la matatizo yetu. Hivi katika serikali yetu ya sasa ni mawaziri wangapi wana shahada ya kwanza na zile za juu (kina Nchimbi et al tusiwahesabu). Je ni vitengo vingapi vinaongozwa na "wasomi"? Mwenye kusimamia Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu si Profesa? Je dili ni kusoma sana halafu kufuja sana au kutosoma sana lakini kuwa mwaminifu kwa mali ya umma? Au kusoma na kuwa mwaminifu? Inaonekana mara nyingi wale "tuliosoma" tukipewa nafasi ya kura na kula, basi tunakula kisomi zaidi!!
 
i) Sasa wanafunzi wazuiwa hata kukusanyika na kufanya mkutano. Wakati huohuo walimu wataenda madarasani kuhubiri uhuru wa watu kukutana na kutoa mawazo.

ii) Kituko kingine eti wanafunzi wamepewa masharti ya kutokugoma tena!

Yaani unaweza kuwa na mamlaka na moyo wa kupora haki na uhuru wa watu kwa kiasi hiki

iii) Halafu wanafunzi waliosimamishwa wamepewa barua za 2004! They couldn't be more reckless

Haya yote yanatokea katika kisima cha elimu nchini mwetu na kinafanywa na maprofesa! Wakati mwingine Nungwi yuko sawa, bora kuwa na uprofesa wa Waryoba ukafanya mambo sawa kuliko hawa jamaa zetu wa mlimani! very disgusting

Soma hapa chini-Mwananchi
________________________________

 
Dar Si Lamu,
Hawa vijana waliopo Vyuoni wanalazimishwa ibada!... wanafahamu vizuri haki zao na wimbi lao la kuikataa dini hii linaanza kujitokeza tofauti na wakati mwingine wowote. Kutawadha kwetu hakuondoi ubovu wa imani yetu ambayo kila siku ndio adhana. Hawa vijana bado ni bikra wa maisha kama yetu na ndio maana nakubali kwamba fedha itaendelea kuweka standard zetu badala ya sisi watu kuweka standard.... Hili ni somo pana zaidi ya kutawadha na kutoa najisi ikiwa ndani ya ibada zetu shetani katawala mafundisho...
Sisi ambao tayari tumeisha toa bikra tunachoweza kufanya ni kuwapa moyo hawa vijana na imani zao, hatuwezi kurudisha bikra zetu wala kuwaacha wake zetu...Mmoja mmoja anaweza kuwa anasali nyumbani mwake lakini ukweli ni kwamba dini nzima ni mbovu. Ibada haikomei msikitini ama kanisani.

Mzee Mwanakijiji,
Siku zote elimu inatanguliwa na IMANI....hata katika dini zetu kwanza unatakiwa Kuamini ambayo ina misingi yake kisha Elimu ambayop inakuonyesha jinsi ya kufanya Ibada. Tupo wengi sana wenye elimu hiyo iwe ya dini ama elimu dunia isipokuwa tumekosa Imani. Katika dini hawamwogopi MUNGU na katika serikali zetu hawaogopi SHERIA...

NI bora sana kuwa na waumini wasiokuwa na elimu lakini wana imani kuliko kuwa na wasomi wasiokuwa na imani. Hii ndiyo Tanzania ya leo, Tanzania ambayo inatanguliza mahitaji yake mbele ya imani.
Kwa hiyo labda wapo waliokwisha kata tamaa ya pepo na hivyo the ONLY way for them (ubinafsi huo) ni pepo ya hapa duniani... FEDHA!
 
soko lenye deal ni mabibo hostel....upo hapo!

Ebwana Mabibo hostel si mchezo lakini.
Mi napaita mbuga ya wanyama au serengeti....maana kuna wanyama wa kila aina i.e. twiga, pundamilia, ngedere, vicheche......n.k.

Bob Mkandara ulipitia hapo?
 

u don't know what u are talking about. Besides umesoma Detroit kijana, elimu ya juu ya bongo unaisoma kwenye IPP media tu.
 
Nyani Ngabu,
Hiyo ndio lugha ya mjini siku hizi... Ukipita sehemu utasikia Punda milia haoo!..eeh eeh bwana wee!..Twiga kakatisha.
Eeeh mwenzako mwenyeji sana mji ule!...Mabibo Hostel tena. Kumbuka nilikuwa Mtalii nimeongeza hesabu ya watalii nchini, usifanye mchezo.
 
barua za Mei 2004!!!!!

Mhh.. mlimani kuna vitukooooooo......lakini daima nitakupenda tu.

Yaani hizo barua ni zilezile walizotumia wakati wa ule mgomo wa 2004 ambao ulikuwa kuzuia kupitishwa kwa sheria ya mikopo ambayo ni mfululizo wa uchemshaji uligubika zoezi zima la utekelezaji wa dira ya elimu ya juu nchini. wakati ule mzee Luhanga alipopoa mahasira yake akayamaliza ki-aina.

Lakini hili linadhihirisha kuwa uongozi mpya mlimani ambao umejaa damu changa zenye upeo wa hali ya juu (ni vichwa kwelikweli) katika dunia yetu umerithi tabia ya kutumia mazoea badala ya mbinu endelevu kutatua matatizo lukuki yanayokikumba chuo chetu.

Well,angalao mwaka huu hawa vijana hawajabakishwa nje ya chuo hadi wakose wiki tatu ambazo zitawalazimisha kurudia mwaka hata kama watkutwa hawana hatia. Lakini kwa upande mwengine hii inaonyesha dalili ya kuwa chuo kinampango wa kuwaachia kama sio wote basi wengi wao lakini kinataka kutoka na sura kidogo.

Ni wazi kuwa kwa kutowapa muda wa kujiaanda kwa utetezi ambao huwa unahitaji si chini ya wiki mbili na pamoja na kuwapa vigezo vyote vilivyotumika kuwashitaki na kuwafikisha katika kamati hiyo ya nidhamu, basi wanafunzi wanakuwa na nafasi nzuri kisheria kuushitaki utawala wa chuo kwa kuwahukumu kinyume cha taratibu za kisheria. Hii inaweza kuwasaidia wanafunzi kwa kuwalazimisha utawala "kuwasamehe" wote watakao patikana na "hatia". Hata hivyo hali yote naweza sema ni mtego mkubwa ambao ni busara zaidi ya maguvu ndio inayohitajika.

Mkumbuke kuwa wengi wao ni wa mwaka wa tatu ambao ni wa mwisho kama sio wanafunzi wa sheria, ualimu, uhandisi na kozi zingine za miaka minne. Hivyo kupoteza mwaka mwengine mmoja ni adhabu kubwa mno kwao na kwa watanzania ambao wangelifaidika na usomi wao hata kiduchu tuu.

tanzanianjema
 
Kaka mkandara,

inaelekea upo katik stage ya kujichambua kimaisha na unajaribu kupata, kujenga ama kuimarisha dira ya maisha yako. Ama nakosea?

Ombi langu ni kuwa ujitahidi tu isije mwisho wa siku usije uka amua kujiunga na "timu ya ushindi" ili ujitengenezee "maisha yako kiulaini" kama watanzania tunavyodai. Huku nyumbani huwa tunasema kuwa "smart" ama "kukubali ukweli".

Nakutakia kila la heri kaka Tanzania yetu inahitaji sana kichwa chako.

Tanzanianjema
 

Kaka Mkandara,

Maneno mazito hayo ... heshima juu yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…