jumatatu.j'nne....hadi j'pili zilitungwa na nani?

elf miaka

Member
Aug 5, 2011
18
2
habari!hivi hizi j'tatu-j'pili zilitungwa na nani na zina maana gani?mana naona kama kuna majina ya watu kwenye hizo siku mfano juma,tatu,pili,ali,hamisi n.k.vile vile kwa kiingereza monday-sunday.
Vile vile hawa kina january-december walitokea wapi kwa ujumla?
Nisaidie unachofahamu kwa manufaa ya wengi.
 
habari!hivi hizi j'tatu-j'pili zilitungwa na nani na zina maana gani?mana naona kama kuna majina ya watu kwenye hizo siku mfano juma,tatu,pili,ali,hamisi n.k.vile vile kwa kiingereza monday-sunday.
Vile vile hawa kina january-december walitokea wapi kwa ujumla?
Nisaidie unachofahamu kwa manufaa ya wengi.


kwanza wewe utuambie, efumiaka ilitoka wapi?????????????
 
bijou elf miaka ilitokana na jamaa alinambia miaka elfu moja kwa Mungu ni siku moja.alinambia ataniambia imeandikwa wapi ila sjamfatilia.
 
Juma ni neno linalomaanisha kujumuika linalotokana na Kiarabu Juma'a ambayo ni siku ya Ijumaa (Ijmaa) kukusanyika, kumbuka Waislam hukusanyika (Ijmaa) miskitini siku moja kwa wiki ili kuelezana mambo yaliyojiri kwa juma zima katika jamii na baada ya Imamu kuelezea Khutba (Hotuba) ya Ijumaa humalizia kwa kuswali Rakaa mbili za pamoja. Kumbuka, siku zote zingine sala za mchana huswaliwa Rakaa nne lakini siku hii zile rakaa mbili hufidiwa na ile Khutba ya kukusanyika (Ijmaa).

Juma = wiki
Mosi = ni kiswahili safi kikimaanisha "first". Kwa hiyo Jumamosi ni siku ya kwanza baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Pili = ni kiswahili safi kikimaanisha "second" Kwa hiyo Jumapili ni siku ya pili baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Tatu = ni kiswahili safi kikimaanisha "third" Kwa hiyo Jumatatu ni siku ya tatu baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Nne = ni kiswahili safi kikimaanisha "fourth" Kwa hiyo Jumanne ni siku ya nne baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Tano = ni kiswahili safi kikimaanisha "fifth" Kwa hiyo Jumatanoi ni siku ya tano baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Alhamis = ni neno la kiarabu linalomaanisha "fifth day" (Al Khamis). Kumbuka siku za kiswahili mosi huanza Jumamosi, siku za Kiarabu Mosi huanza Jumapili (Youm 'l Ahad) Ahad ni "first" kwa Kiarabu ambayo tayari ni siku ya pili ya Kiswahili.

Neno au jina Ali halipo kabisa katika hizo siku kama uonavyo kwenye hizo siku kuna "Al" na si Ali.

Majina ya Juma kuwa jina la mtu inawezekama kabisa huyo mtu alizaliwa siku ya Ijumaa na Waarabu wanalo hilo jina wao huliita Juma'a kama ujuavyo Kiswahili kinafanyiwa kila njia kuzitowa zile lafdhi za Kiarabu na ndio linabaki kuwa Juma na si Juma'a ki uhalisia wake inatakiwa liwe Juma'a na si Juma.

Hayo majina ya Pili, Tatu na Khamis (linauliwa na Hamisi) ni kuwa huyo ni mtoto wa Pili (second), Tatu (Third) na wa Tano (Khamis). Lakini kwa kuwa yameshakuwa majina na pengine yawe yamerithiwa kwa babu au bibi au Mjomba au ndugu au rafiki na huwa hayafati sana kuzaliwa kwa mtu, yaani inawezekana kabisa kuwa Tatu si mtoto wa Tatu bali alipewa hilo jina kwa kuwa shangazi yake anaitwa Tatu.

Nadhani umeelewa haya ya Kiswahili kabla hatujaanza na hayo ya Kiingereza? kama una swali lolote kuhusu hayo usisite kuuliza.
 
Juma ni neno linalomaanimanisha kujumuika linalotokana na Kiarabu Juma'a ambayo ni siku ya Ijumaa (Ijmaa) kukusanyika, kumbuka Waislam hukusanyika (Ijmaa) miskitini siku moja kwa wiki ili kuelezana mambo yaliyojiri kwa juma zima katika jamii na baada ya Imamu kuelezea Khutba (Hotuba) ya Ijumaa humalizia kwa kuswali Rakaa mbili za pamoja. Kumbuka, siku zote zingine huswaliwi Rakaa nne lakini siku hii zile rakaa mbili hufidiwa na ile Khutba ya kukusanyika (Ijmaa).

Juma = wiki
Mosi = ni kiswahili safi kikimaanisha "first". Kwa hiyo Jumamosi ni siku ya kwanza baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Pili = ni kiswahili safi kikimaanisha "second" Kwa hiyo Jumapili ni siku ya pili baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Tatu = ni kiswahili safi kikimaanisha "third" Kwa hiyo Jumatatu ni siku ya tatu baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Nne = ni kiswahili safi kikimaanisha "fourth" Kwa hiyo Jumanne ni siku ya nne baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Tano = ni kiswahili safi kikimaanisha "fifth" Kwa hiyo Jumatanoi ni siku ya tano baada ya Ijmaa (Ijumaa).
Alhamis = ni neno la kiarabu linalomaanisha "fifth day" (Al Khamis). Kumbuka siku za kiswahili mosi huanza Jumamosi, siku za Kiarabu Mosi huanza Jumapili (Youm 'l Ahad) Ahad ni "first" kwa Kiarabu ambayo tayari ni siku ya pili ya Kiswahili.

Neno au jina Ali halipo kabisa katika hizo siku kama uonavyo kwenye hizo siku kuna "Al" na si Ali.

Majina ya Juma kuwa jina la mtu inawezekama kabisa huyo mtu alizaliwa siku ya Ijumaa na Waarabu wanalo hilo jina wao huliita Juma'a kama ujuavyo Kiswahili kinafanyiwa kila njia kuzitowa zile lafdhi za Kiarabu na ndio linabaki kuwa Juma na si Juma'a ki uhalisia wake inatakiwa liwe Juma'a na si Juma.

Hayo majina ya Pili, Tatu na Khamis (linauliwa na Hamisi) ni kuwa huyo ni mtoto wa Pili (second), Tatu (Third) na wa Tano (Khamis). Lakini kwa kuwa yameshakuwa majina na pengine yawe yamerithiwa kwa babu au bibi au Mjomba au ndugu au rafiki na huwa hayafati sana kuzaliwa kwa mtu, yaani inawezekana kabisa kuwa Tatu si mtoto wa Tatu bali alipewa hilo jina kwa kuwa shangazi yake anaitwa tatu.

Nadhani umeelewa haya ya Kiswahili kabla hatujaanza na hayo ya Kiingereza? kama una swali lolote kuhusu hayo usisite kuuliza.

FaizaFoxy, nimekusoma!
 
bibie Faiza Foxy umenilog in na hayo mafundisho yako hapo juu,ubarikiwe sana. Nalog off
 
asante faiza,kwa kifupi nmeelewa kwamba hizi siku mizizi yake iko kwenye kiarabu au yako kiislamu zaidi.nmeona kwenye kitabu cha neno la Mungu cha kikrsto kimeandika siku ya kwanza,ya pili...mpaka ya saba sasa nkapata wasiwasi kuhusu uwepo wa jumatatu hadi jumapili.vilevile kwenye miezi nikajitahidi kutizama januari mpaka desemba sikuona ndiko maswali yakaanza kuja kichwani.haya mambo si ya kudharau kwasababu ukiambiwa ndege yako inaondoka saa nane mchana ukafika saa nane usiku hujaachwa?so tunapozungumzia majira ambazo ndo izi siku na miezi iliyopewa majina tuwe na taadhari ya kujifunza.faiza endelea kutujuza zaidi kama kwenye quraan labda wameandikaje na mengineyo.
 
kongosho ingia kwa kweli mana kuna dakika,saa,siku,mwezi hadi mwaka wa kila tukio iwe nila kufa au kuzaliwa au kupata pesa.sasa tusipojua haya majina majina chimbuko lake nahisi ndo tunadondokea kwenye majira ya mitego mibaya.yani unakuwa km umewekewa fence flani.information is power.elimu haina mwisho si unajua.
 
asante faiza,kwa kifupi nmeelewa kwamba hizi siku mizizi yake iko kwenye kiarabu au yako kiislamu zaidi.nmeona kwenye kitabu cha neno la Mungu cha kikrsto kimeandika siku ya kwanza,ya pili...mpaka ya saba sasa nkapata wasiwasi kuhusu uwepo wa jumatatu hadi jumapili.vilevile kwenye miezi nikajitahidi kutizama januari mpaka desemba sikuona ndiko maswali yakaanza kuja kichwani.haya mambo si ya kudharau kwasababu ukiambiwa ndege yako inaondoka saa nane mchana ukafika saa nane usiku hujaachwa?so tunapozungumzia majira ambazo ndo izi siku na miezi iliyopewa majina tuwe na taadhari ya kujifunza.faiza endelea kutujuza zaidi kama kwenye quraan labda wameandikaje na mengineyo.

Miezi kwenye bible;
Abibu,zivu,siwan,tamuz,abu,eluli,ethanim,buli,kisleu,thebet,shebath,Adari
 
mh marejesho naomba reference ya hayo majina nikajisomee.kwa hiyo kwenye hicho kitabu hakuna januari mpaka desemba?unafahamu zilitoka wapi na maana zake?

JF elimu tosha kwa kweli
 
Elf Miaka,nakumbuka ni kitabu cha Mwanzo mistari ntakupatia baadae kwani bible iko mbali kidogo!Hakuna January to December bali ni aina ya wazungu tu kutuweka sawa!!Kwa wanaosali kanisa la Siloam,wamekuwa wakifundisha sana kuhusu siku na miezi!
 
asante faiza,kwa kifupi nmeelewa kwamba hizi siku mizizi yake iko kwenye kiarabu au yako kiislamu zaidi.nmeona kwenye kitabu cha neno la Mungu cha kikrsto kimeandika siku ya kwanza,ya pili...mpaka ya saba sasa nkapata wasiwasi kuhusu uwepo wa jumatatu hadi jumapili.vilevile kwenye miezi nikajitahidi kutizama januari mpaka desemba sikuona ndiko maswali yakaanza kuja kichwani.haya mambo si ya kudharau kwasababu ukiambiwa ndege yako inaondoka saa nane mchana ukafika saa nane usiku hujaachwa?so tunapozungumzia majira ambazo ndo izi siku na miezi iliyopewa majina tuwe na taadhari ya kujifunza.faiza endelea kutujuza zaidi kama kwenye quraan labda wameandikaje na mengineyo.

Kumbuka kwanza wakurusedi wa mwanzo (Vasco Da Gama na wenzake) walipoingia pwani ya bahari ya hindi walikuta kuna mji (Kilwa uliyo kuwa umeendelea kwa wakati huo kuliko hata miji ya kwao walikotoka, walikuta watu wanavaa mpaka hariri wakati kwao walikuwa hawaijuwi, walikuta watu wanapaka rangi za nyumba wakati kwao walikuwa hawazijuwi, walikuta watu wanatumia kauri za Kichina (China ware) wakati kwao walikuwa hawazijuwi, walikuta watu wanatumia sarafu za dhahabu kwa biashara zao na pia wakakuta watu hao ni Waislaam na wanaendesha mji wao Kiislaam.

Kwa hiyo usishangae hizi siku zimekaa Kiislaam sana kwani hapa kwetu Uislaam ulikuwepo kabla ya Ukristo na pia Uswahili unahusishwa na Uislaam, maneno mengi ya Kiswahili yanatokana na Kiarabu ambacho ni lugha ya Qur'an kwa hiyo usishangae ukiyakuta ya Kiislam mengi kwenye Kiswahili.
 
asante faiza,kwa kifupi nmeelewa kwamba hizi siku mizizi yake iko kwenye kiarabu au yako kiislamu zaidi.nmeona kwenye kitabu cha neno la Mungu cha kikrsto kimeandika siku ya kwanza,ya pili...mpaka ya saba sasa nkapata wasiwasi kuhusu uwepo wa jumatatu hadi jumapili.vilevile kwenye miezi nikajitahidi kutizama januari mpaka desemba sikuona ndiko maswali yakaanza kuja kichwani.haya mambo si ya kudharau kwasababu ukiambiwa ndege yako inaondoka saa nane mchana ukafika saa nane usiku hujaachwa?so tunapozungumzia majira ambazo ndo izi siku na miezi iliyopewa majina tuwe na taadhari ya kujifunza.faiza endelea kutujuza zaidi kama kwenye quraan labda wameandikaje na mengineyo.

Kwanza nikupe huu muujiza wa hizi siku, miezi, na juma kwenye Qur'an, halafu mengine tutaendelea:

  • Neno Mwezi "month" (shahr) linatajwa mara 12.
  • Neno Siku (uwingi wa Siku au Kipindi) "days" (ayyam,yawmayn) linatajwa mara 30.
  • Neno Siku "day" (yawm) linatajwa mara 365.
  • Neno Sabbath (Siku ya Saba ya Juma) linatajwa mara 7.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom