DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mtia nia wa nafasi ya ubunge katika Jimbo la Pangani mkoani Tanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumaa Aweso, ameibuka mshindi kwa kishindo katika kura za maoni zilizofanyika jimboni humo baada ya kupata kura zote za ndiyo katika kata zote zilizopiga kura.
Aweso amepitishwa na wajumbe wote wa CCM kwa kupata asilimia 100 ya kura dhidi ya wapinzani wake wawili waliokuwa wakichuana naye katika mchakato huo wa ndani ya chama, ambao hata hivyo hawakuambulia kura hata moja. Katika taarifa aliyoiweka kupitia ukurasa wake wa Instagram, Aweso amewashukuru wajumbe kwa imani waliyoionyesha kwake akisema: “Asanteni Wajumbe wa CCM Pangani kwa kura zote za ndiyo... Imani hii mlionipa nitailipa kwa matendo.
” Matokeo ya awali ya kura za maoni katika kata zote 14 zilizoshiriki yanaonesha kuwa Jumaa Aweso alipata kura zote, huku wapinzani wake Ramadhan Zuberi na Mariam Abdallah wakitoka kapa kata hadi kata. Kata kama Pangani Magharibi, Kipumbwi, Mikinguni, Mkwaja, Mwera na nyinginezo zilionesha uungwaji mkono wa hali ya juu kwa Aweso, ambaye ni Waziri wa Maji katika serikali ya awamu ya sita.
Aweso amepitishwa na wajumbe wote wa CCM kwa kupata asilimia 100 ya kura dhidi ya wapinzani wake wawili waliokuwa wakichuana naye katika mchakato huo wa ndani ya chama, ambao hata hivyo hawakuambulia kura hata moja. Katika taarifa aliyoiweka kupitia ukurasa wake wa Instagram, Aweso amewashukuru wajumbe kwa imani waliyoionyesha kwake akisema: “Asanteni Wajumbe wa CCM Pangani kwa kura zote za ndiyo... Imani hii mlionipa nitailipa kwa matendo.
” Matokeo ya awali ya kura za maoni katika kata zote 14 zilizoshiriki yanaonesha kuwa Jumaa Aweso alipata kura zote, huku wapinzani wake Ramadhan Zuberi na Mariam Abdallah wakitoka kapa kata hadi kata. Kata kama Pangani Magharibi, Kipumbwi, Mikinguni, Mkwaja, Mwera na nyinginezo zilionesha uungwaji mkono wa hali ya juu kwa Aweso, ambaye ni Waziri wa Maji katika serikali ya awamu ya sita.