Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,933
- 2,817
Wakuu nimekuwa nikifuatilia mtiririko wa matukio tangu kuibuliwa kwa hoja ya masalia hadi kufukuzwa na hatimaye kufikia hatua ya kuhamia chama tawala baadhi ya masalia akiwepo Juliana na Mwampamba.
Kuibuka kwa ile hoja ni jambo ambalo japo lilijadiliwa sana, chanzo chake ni tata. Waliohamia CCM ni wawili; Juliana na Mtela lakini anayesikika zaidi ni huyu dada. Awali alisema yeye bado ni BAVICHA na hautambui utenguzi uliofanyika. Mara tukasikia yuko CCM na kapokelewa na Rais! Akiwa yeye na mwenzake. Mara anatoa kauli kuwa yeye ni mzawa wa Ubungo na yuko tayari kupambana na Mnyika.
Niseme tu kwamba kazi aliyotumwa sio kwamba ameikamilisha. Ndio kwanza inaanza. Huyu ni Delila. Ni mzuri wa sura na umbo lakini ana akili ya nyoka.
CHADEMA itambue yafuatayo;
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya CHADEMA ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya CHADEMA na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka CCM kwa ajili ya kuikandamiza CHADEMA atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.
CHADEMA watambue sasa kuwa hawajaondoa tatizo bali wamezaa tatizo. Wamezaa si kwa kosa lao bali wakati mwingine inatokea tu. Wajipange katika kudhibiti athari zitakazotokana na kauli za huyu msichana.
Historia isijeandikwa kupitia sumu ya huyu mtoto na kamwe asipuuzwe. Harakati zake kipindi cha masalia na PM7 dhidi ya CHADEMA zinajulikana, nazo zilikuwa za faragha na ziliathiri chama. Sasa hizi za hadharani nazo zikipuuzwa si balaa?
Kuibuka kwa ile hoja ni jambo ambalo japo lilijadiliwa sana, chanzo chake ni tata. Waliohamia CCM ni wawili; Juliana na Mtela lakini anayesikika zaidi ni huyu dada. Awali alisema yeye bado ni BAVICHA na hautambui utenguzi uliofanyika. Mara tukasikia yuko CCM na kapokelewa na Rais! Akiwa yeye na mwenzake. Mara anatoa kauli kuwa yeye ni mzawa wa Ubungo na yuko tayari kupambana na Mnyika.
Niseme tu kwamba kazi aliyotumwa sio kwamba ameikamilisha. Ndio kwanza inaanza. Huyu ni Delila. Ni mzuri wa sura na umbo lakini ana akili ya nyoka.
CHADEMA itambue yafuatayo;
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya CHADEMA ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya CHADEMA na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka CCM kwa ajili ya kuikandamiza CHADEMA atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.
CHADEMA watambue sasa kuwa hawajaondoa tatizo bali wamezaa tatizo. Wamezaa si kwa kosa lao bali wakati mwingine inatokea tu. Wajipange katika kudhibiti athari zitakazotokana na kauli za huyu msichana.
Historia isijeandikwa kupitia sumu ya huyu mtoto na kamwe asipuuzwe. Harakati zake kipindi cha masalia na PM7 dhidi ya CHADEMA zinajulikana, nazo zilikuwa za faragha na ziliathiri chama. Sasa hizi za hadharani nazo zikipuuzwa si balaa?