Juliana - Erick Shigongo

Juliana - Erick Shigongo

Je Gideon atamuuwa mkewe Juliana tutaonana kesho kwenye mwisho wa simulizi hii nzuri ya kusisimua.....
Sente Shunie.....
Najua hii ni hadithi, ina maana wazazi wa Juliana hawapo tena hadi binti yao anaumwa kiasi cha kuteseka ndani bila msaada?
 
Sente Shunie.....
Najua hii ni hadithi, ina maana wazazi wa Juliana hawapo tena hadi binti yao anaumwa kiasi cha kuteseka ndani bila msaada?
Ngoja nimuulize shigongo hili swali my dear
 
  • Thanks
Reactions: ram
SEHEMU YA 33...

“We wanted to surprise you!” (tulitaka tukusapraizi) alisema Juliana huku akimwangalia mume wake.
“Well, you succeeded,” (Vizuri, mmefanikiwa) alisema Gideon huku akiwafuata.

Tangu mke wake alipoanza kuumwa, siku hiyo alimuona mke wake kuwa tofauti kabisa, tabasamu alilokuwa akilionyesha usoni mwake lilionyesha kabisa kwamba mwanamke huyo alikuwa na penzi la kweli kwake.

Akabaki akiwa amesimama huku macho yake yakiwaangalia wote wawili. Wakati akiwa anaendelea kufikiria mambo mengi kuhusu mke wake, Jesca akasimama, akamfuata na kumkumbatia.
“Dad! Come back to us pleseee,” (baba! Turudie tafadhali) alisema Jesca huku akianza kulia.

Hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, hakujua kama mtoto wake huyo alijua kilichokuwa kikiendelea au la. Ghafla, katika hali ambayo hata yeye mwenyewe aliishangaa, mwili wake ukaanza kutetemeka na kijasho chembamba kuanza kumtoka.

Aliguswa moyoni mwake, alimshika mtoto wake huku akimwangalia mke wake aliyekuwa kochini, bado tabasamu pana lilikuwa likionekana usoni mwake.
Hapo ndipo akaanza kujiuliza juu ya kile kilichokuwa kimetokea, kwa nini alitaka kumuua Juliana? Kulikuwa na ubaya wowoote aliomtendea mpaka kutaka kuchukua hatua ngumu kiasi hicho.

Wakati akijiuliza hivyo, kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma kabisa tangu siku ambayo alikutana na msichana huyo, alivyokuwa akimuhitaji na mwisho wa siku kufanikiwa kuwa naye na kumuoa.
Upendo wote ulikwenda wapi? Yaani kipi kilimfanya mpaka kuchukua uamuzi wa kukubaliana na Juliet kumuua mke wake? Kuna baya alilomtendea? Kama hakuna, kwa nini aliamua kukubaliana na msichana huyo?

Wakati akijiuliza yote hayo, akaanza kumfikiria mtoto wake. Hii ilimaanisha kwamba kama angemuua Juliana mtoto Jesca angebaki akiwa hana mama. Nani angempa mapenzi yale aliyokuwa akiyapata kutoka kwa mama yake? Juliet angeweza? Msichana huyo alikuwa na umri mdogo, binti mbichi, je, angeweza kuishi na Jesca na kumpa mapenzi yote ambayo mke wake alikuwa akimpa?

Itaendelea.
 
SEHEMU YA 34...

Miguu yake ikaanza kuishiwa nguvu, akakaa kwenye kochi, mashavu yake yalilowanishwa na machozi, aliumia, alijiona kuwa mkosaji kwani mke wake huyo hakuwa amemkosea kitu chochote kile zaidi ya kumwambia kwamba kila siku alitamani kumuona akiwa na furaha tele.
“Nisamehe mke wangu!” alisema Gideon huku akisimama na kumfuata mke wake.
Juliana hakujua kilichokuwa kikiendelea, alimwangalia mume wake huku akiwa na maswali mengi juu ya sababuu iliyomfanya kulia namna ile.


Alipomfikia, wakakumbatiana.
“Nilitaka kukuua!” alisema Gideon, hakuwa na jinsi, alimwambia ukweli mke wake kwamba alitaka kumuua kwa kuwa tu alikuwa na tamaa ya kuwa na mwanamke mwingine.
Juliana ilimuuma lakini hakuwa na la kufanya, alifurahi kwa sababu tu mume wake alijiweka wazi, kwa jinsi alivyokuwa akilia ilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa ameumia kwa kile kilichokuwa kimetokea.

Akamuomba msamaha mke wake, alimwambia kwamba shetani alikuwa amemuingia na ndiyo maana alifanya maamuzi ya kijinga ya kutaka kumuacha na kumchukua mwanamke mwingine.
“Nimekusamehe mume wangu kama tu umeligundua kosa lako,” alisema Juliana huku akimwangalia mume wake huyo aliyekuwa akibubujikwa na machozi.

Akasimama na kumkumbatia, moyo wake ukaridhika, akajisikia amani, hakutaka kachana na Juliet hivihivi, alichokifanya ni kumpigia simu na kumwambia kwamba aliifanya kazi aliyokuwa amempa na hivyo alitaka kuonana naye katika Hoteli ya Lion kwa ajili ya kuzungumzia maisha yao ambayo yangeendelea baada ya kumuua mke wake.

“Umemuua kweli?” aliuliza msichana huyo kwenye simu.
“Ndiyo! Tuonane tuzungumzie maisha yetu mapya,” alisema Gideon.
“Sawa. Nakupenda sana mume wangu! Nakupenda sana kwa kunisikiliza,” alisema Juliet na simu kukatwa.
Alipanga mipango na mke wake, japokuwa hakuwa katika hali nzuri lakini alimuomba kujikaza kwani alitaka kumpeleka huko hotelini kuonana na Juliet, msichana aliyetaka afe kwa gharama yoyote ile.

Je nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 35...

Kwa kuvumilia maumivu, Juliana akakubaliana na mumewe, wakaingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo. Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika hoteli hiyo ambapo akachukua chumba na kwenda na mkewe.
Wakatulia huko, muda mwingi alikuwa akimpigia simu Juliet kwa lengo la kumsisitiza kwamba alitakiwa kuonana naye haraka sana. Hilo halikuwa tatizo, baada ya dakika ishirini, msichana huyo akafika na kwenda ndani ya chumba hicho alichoambiwa kwamba Gideon alikuwepo akimsubiri.

Alipoingia na macho yake kutua kwa mwanaume huyo, akamfuata na kumkumbatia kwa furaha. Gideon hakuonyesha tofauti yoyote ile, naye akamkumbatia huku mke wake, Juliet akiwa bafuni akisubiri muda wa kuambiwa atoke.
“Hongera sana kwa kazi nzito!” alisema Juliet huku akiachia tabasamu.
“Nashukuru! Ila ningependa kwanza nikwambie kitu kimoja,” alisema Gideon.
“Kitu gani hubby?”

“Ninampenda mke wangu!” alisema Gideon.
“Unampenda mke wako? Kashakufa tayari! Tuanze maisha mapya hubby!” alisema Juliet.
“Hapana! Mke wangu hajafa.”
“Hajafa?”
“Juliet! Ninampenda mke wangu. Hujui tulipotoka, nilimpenda kwa kipindi kirefu sana, tangu tulipokuwa shuleni. Nilikuwa masikini, mwanamke yule alinipenda hivyo hivyo, sikuwa na kitu, alinionyeshea mapenzi ya dhati. Nilimthamini sana.

Uliponiambia nimuue, nilikubaliana nawe, sikukumbuka kitu chochote kile kuhusu mimi na yeye,” alisema Gideon na kuendelea:
“Ni mwanamke mzuri, hajawahi kunikosea, ananipenda. Juliet! Mke wangu ni mke mwema, sikuweza kumuua mwanamke yule, ni mzuri sana, mcha Mungu! Nitamuua vipi? Siwezi!

Nikwambie tu Juliet, ninampenda mke wangu, ninampenda sana, haijalishi ni mgonjwa, ninampenda mno, ninampenda kwa kiasi kwamba siwezi kuelezea. Kama ulitarajia nimuue, hicho ni kitu ambacho hakiwezi kutokea, siwezi kumuua mwanamke ninayempenda toka moyoni mwangu,” alisema Gideon huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.

Juliet alivimba kwa hasira, hakuamini kile alichokisikia, alimwamini Gideon na kuona kwamba angefanya kile alichomwambia akifanye lakini matokeo yake akamwambia kwamba hakukifanya kwa kuwa tu alikuwa akimpenda mke wake.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 36...

Hata kabla msichana huyo hajasema kitu chochote, Gideon akasimama na kwenda kuufungua mlango wa bafu na Juliana kutoka. Kama ilivyokuwa kwa mumewe, hata na yeye machozi yalikuwa yakimtiririka mashavuni mwake kwani alikuwa akisikia kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko.

“Juliet! Mwangalie mke wangu, angalia uzuri wake, huyu mwanamke ana moyo wa chuma, ni mwanamke ambaye kila mwanaume duniani anatamani kuwa naye. Unawezaje kumuua mwanamke kama huyu? Hakuna mwanaume kichaa wa kufanya hivyo, kila mmoja anatamani kuwa na mtu kama Juliana,” alisema Gideon na kuendelea:

“Juliet! Ninampenda mno mke wangu, ni mrembo, sikuwahi kuukupenda, sikuwahi kupenda mwanamke zaidi ya huyu, wewe nilikutamani tu, ukweli sikuwahi kukupenda hata siku moja moyoni mwangu! Nilikutamani tu Juliet,” alisema Gideon.

Juliet alishindwa kuvumilia, akasimama kutoka pale alipokuwa amekaa, akaufuata mlango, akaufungua na kutoka ndani ya chumba hicho.
Moyo wake ulisikia maumivu makali, hakuamini kama kwa kipindi chote hicho alichokuwa na mwanaume huyo kumbe hakuwahi kumpenda zaidi ya kumtamani tu.

Gideon hakujali, akamwangalia mke wake usoni na kumwambia kwa mara nyingine tena kwamba alikuwa akimpenda mno na kamwe asingeweza kufanya ujinga kama alioufanya kipindi hicho. Akamkumbatia na kumpiga mabusu mfululizo mashavuni mwake na baada ya dakika kadhaa, wakaondoka hotelini hapo.

Maisha yakabadilika, mapenzi yakarudi, wakapendana zaidi, Gideon akawa karibu na mkewe, akamfanyia mambo mengi kama mkewe mpaka pale miaka mitano ilipokatika na mwanamke huyo kufariki dunia kwa ugonjwa wa kansa iliyokuwa ikimtesa kwa miaka mingi.

Juliana akabaki kichwani mwa Gideon, alimthamini na kila wiki ilikuwa ni lazima kwenda katika kaburi la mke wake na kukaa pambeni kama kumuenzi.

MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom