Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 18...
Gideon akatoka kuoga, akalivua taulo lake na kukaa kitandani. Alimwangalia mpenzi wake, Juliana, kwa jinsi alivyoonekana, hakuonekana kama alivyokuwa ameelekea bafuni, alibadilika na kwa jinsi uso wake ulivyokuwa, ilionyesha kabisa kwamba kulikuwa na kitu.
Hakujua ni kitu gani kilitokea, ila cha kwanza kabisa akaiangalia simu yake, alitaka kujua kama ilikuwa salama. Akatoa password na kuingia huku akizuga kuangalia kama kuna ujumbe au kupigiwa simu.
Akaenda kotekote, hakukuta ujumbe wowote wala simu iliyopigwa kwani wakati Juliana ametuma ujumbe kwa Halima, aliufuta ujumbe wake. Gideon akajiridhisha kwamba hakukuwa na kitu kibaya, sasa kwa nini mpenzi wake alibadilika hivyo?
“Kuna nini? Mbona upo hivyo?” aliuliza Gideon huku akimwangalia Juliana.
“Hakuna kitu! Kichwa kinaniuma sana, kimeanza ghafla, yaani sina raha mpenzi,” alisema Juliana huku akikishika kichwa chake.
“Pole sana jamani! Hebu sogea huku kwanza,” alisema Gideon, Juliana akasogea na kisha kumkumbatia.
Alilihisi joto la mwili wa msichana huyo, lilikuwa kali lililomfanya kujisikia vizuri kabisa kutokana na uwepo wa mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha. Walikumbatiana kwa dakika kadhaa na msichana huyo kuaga, siku hiyo hata kusindikizwa hakutaka.
Njiani alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma, kitu kilichokuwa akilini mwake ni kwamba Gideon alikuwa akitoka kimapenzi na Halima. Kwa nini amsaliti? Kwa nini mchukue msichana huyo na wakati alikuwa naye kipindi hicho.
Akafungua WhatsApp kupitia kwa namba yake nyingine ambayo alimpa Halima. Alitaka kuangalia kama kungekuwa na ujumbe wowote ule, kabla ya kufanya chochote akabadilisha picha na kuweka ya Gideon.
Alikaa na kuangalia huko, hakukuwa na ujumbe wowote ule lakini baada ya dakika chache akapokea ujumbe kutoka kwa msichana huyo ambaye alikuwa akilalamika.
“Kwa nini umenifanyia hivi?” aliuliza Halima kwa kupitia ujumbe mfupi WhatsApp, tena aliweka na emoj ya kulia.
“Nimekufanyaje jamani?” aliuliza Juliana kwa namba ile aliyojifanya Gideon.
“Hebu niambie kitu kimoja! Unanipenda?” aliuliza Halima.
Itaendelea.
Gideon akatoka kuoga, akalivua taulo lake na kukaa kitandani. Alimwangalia mpenzi wake, Juliana, kwa jinsi alivyoonekana, hakuonekana kama alivyokuwa ameelekea bafuni, alibadilika na kwa jinsi uso wake ulivyokuwa, ilionyesha kabisa kwamba kulikuwa na kitu.
Hakujua ni kitu gani kilitokea, ila cha kwanza kabisa akaiangalia simu yake, alitaka kujua kama ilikuwa salama. Akatoa password na kuingia huku akizuga kuangalia kama kuna ujumbe au kupigiwa simu.
Akaenda kotekote, hakukuta ujumbe wowote wala simu iliyopigwa kwani wakati Juliana ametuma ujumbe kwa Halima, aliufuta ujumbe wake. Gideon akajiridhisha kwamba hakukuwa na kitu kibaya, sasa kwa nini mpenzi wake alibadilika hivyo?
“Kuna nini? Mbona upo hivyo?” aliuliza Gideon huku akimwangalia Juliana.
“Hakuna kitu! Kichwa kinaniuma sana, kimeanza ghafla, yaani sina raha mpenzi,” alisema Juliana huku akikishika kichwa chake.
“Pole sana jamani! Hebu sogea huku kwanza,” alisema Gideon, Juliana akasogea na kisha kumkumbatia.
Alilihisi joto la mwili wa msichana huyo, lilikuwa kali lililomfanya kujisikia vizuri kabisa kutokana na uwepo wa mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha. Walikumbatiana kwa dakika kadhaa na msichana huyo kuaga, siku hiyo hata kusindikizwa hakutaka.
Njiani alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma, kitu kilichokuwa akilini mwake ni kwamba Gideon alikuwa akitoka kimapenzi na Halima. Kwa nini amsaliti? Kwa nini mchukue msichana huyo na wakati alikuwa naye kipindi hicho.
Akafungua WhatsApp kupitia kwa namba yake nyingine ambayo alimpa Halima. Alitaka kuangalia kama kungekuwa na ujumbe wowote ule, kabla ya kufanya chochote akabadilisha picha na kuweka ya Gideon.
Alikaa na kuangalia huko, hakukuwa na ujumbe wowote ule lakini baada ya dakika chache akapokea ujumbe kutoka kwa msichana huyo ambaye alikuwa akilalamika.
“Kwa nini umenifanyia hivi?” aliuliza Halima kwa kupitia ujumbe mfupi WhatsApp, tena aliweka na emoj ya kulia.
“Nimekufanyaje jamani?” aliuliza Juliana kwa namba ile aliyojifanya Gideon.
“Hebu niambie kitu kimoja! Unanipenda?” aliuliza Halima.
Itaendelea.