loliondokwetu
JF-Expert Member
- Feb 21, 2018
- 1,376
- 1,767
,,
Umepotelea wapi lakini vipi mkanda wa siri season 2 si ulisema unayo tuwekee basi
Pamoja sana shunieJULIANA-03....
Moyo wa Juliana ukachoma, akahisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake, hakutegemea kusikia maneno kama hayo yakitoka mdomoni mwa mume wake. Alimkumbuka, alihitaji faraja, alijua kwamba alikuwa akipitia katika kipindi kigumu, alitakiwa kubembelezwa, alitakiwa kufarijiwa na kutiwa moyo sana lakini kwa mume wake huyo, hilo lilionekana kuwa kama ndoto. Angeanzaje kumkumbatia?
“Unalala sebuleni au chumbani?” aliuliza Gideon.
“Popote utakapolala! Siwezi kulala peke yangu tena! Gideon mume wangu! Kumbuka tulivyokuwa, kumbuka ulivyoahidi mbele ya kanisa, shida na raha, ugonjwa na afya! Umesahau yote hayo mume wangu?’ aliuliza Juliana huku akimwangalia Gideon.
“Clock is ticking…” (muda unakwenda tu)
“Gideon! Pleasee..” (tafadhali, Gideon..)
Gideon akasimama, kwake, maneno yote aliyokuwa akiambiwa na mkewe hayakuonekana kuwa na maana kabisa, hayakumuingia hata kidogo moyoni mwake. Alimchukia Juliana, hakumpenda, alikuwa radhi kulala na mbwa lakini si kulala na mtu kama Juliana.
Alibadilika, hakuwa mzuri, hakuwa na mvuto, kila alipomwangalia, alionekana kuwa kama kituko. Bosi yeye, milionea, eti alale na mtu kama Juliana! Ili iweje? Thamani ya mwanamke huyo ilipotea moyoni mwake, mapenzi yakapotea, chuki ikaingia moyoni mwake.
Kila alipomwangalia, alitamani kumuua, alitamani kumchukua na kwenda kumtelekeza mahali fulani lakini si kuendelea kukaa ndani ya nyumba yake, yaani kila alipokuwa akiamka, amkute chumbani humo. Alimchukia kupita kawaida.
“Kuna siku nitamuua tu! Nitakuja kumuwekea sumu kwenye maji,” alisema Gideon huku akipiga hatua kuelekea chumbani, hakuyajali machozi ya Juliana, jinsi alivyokuwa akilia, kwake alimuona kama muigizaji wa Bongo Muvi ambaye alikuwa kwenye filamu kali ya majonzi.
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, alimchukua mkewe, yuleyule mwanamke ambaye kipindi cha nyuma alimwambia kwamba alimpenda kwa moyo wote, alimpenda hata zaidi ya alivyokuwa akiwapenda wazazi wake.
Kansa ikabadilisha kila kitu, ikayaondoa mapenzi aliyokuwa nayo na kupandikiza chuki moyoni mwake. Hakukuwa na jingine alilokuwa akilifikiria zaidi ya kumuua mwanamke huyo ambaye bado alikuwa akiteseka kila siku.
Unajua nini kiliendelea?
Nakuaminia bibieItaendelea tena kesho......