Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 26...
Hakukumbuka chochote kuhusu mke wake, alimchukia, kila alichosema Juliet alimsapoti, hakukumbuka kwamba zamani hakuwa na pesa lakini msichana huyo alimpenda hivyohivyo, hakukumbuka kwamba utajiri aliokuwa nayo, chimbuko lake lilikuwa kwa wazazi wa mwanamke huyo huyo, hakukumbuka kitu chochote kile, kitu pekee alichokuwa na hamu nacho kwa wakati huo ni kumuua Juliana tu.
Akarudi nyumbani huku akiwa na muonekano mwingine kabisa. Akamkuta Juliana akiwa sebuleni amekaa akimsubiri. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake kila siku, hakukubali kulala na wakati mume wake hakuwa amerudi nyumbani.
Ilikuwa ni lazima kukaa sebuleni mpaka mwanaume huyo atakaporudi nyumbani hapo. Alipokuwa akija, hakuzungumza naye, alimsalimia mwanaume huyo lakini alikuwa kimya, hata salamu hakutaka kabisa.
Siku hiyo Gideon alipoingia, alionekana kuwa tofauti, alipoufungua mlango na kumwangalia mke wake, tabasamu pana likaonekana usoni mwake.
Juliana akashangaa, hakuamini alichokuwa akikiona, hakuwahi kuliona tabasamu la mume wake tangu alipoanza kuugua, leo iweje mwanaume huyo atoe tabasamu pana kiasi hicho?
Kwa tabu sana akasimama na kumfuata mume wake, alipomfikia, akamkumbatia, kwa furaha aliyokuwa nayo moyoni, Juliana akaanza kulia, hatimaye mume wake wa zamani, mume wake yule aliyekuwa kipindi cha nyuma alikuwa amerudi pasipo kugundua kwamba mwanaume huyo alikuwa na jambo lake moyoni mwake.
“Nimekukumbuka mke wangu,” alisema Gideon huku akimwangalia Juliana.
“Nimekukumbuka pia,” alisema Juliana huku akilia kwa furaha.
Wakaongea mengi kama wanandoa, wakaondoka na kuelekea chumbani.
Kila kitu alichokuwa akikifanya, moyo wake ulimuuma mno, hakutaka kumshika mkono Juliana lakini kwa kuwa alitaka kumuua, ilikuwa ni lazima kufanya hivyo.
Akamuacha chumbani na kumwambia kwamba aende jikoni kuchukua chakula na kula. Akaondoka na kuelekea huko ambapo kitu cha kwanza kabisa ni kuchukua simu na kumpigia Juliet.
“Vipi? Umemuua?” alisikika Juliet kwenye simu.
“Bado!”
“Acha ujinga. Unasubiri nini sasa?” aliuliza msichana huyo.
“Ndiyo naandaa mazingira!”
“Au bado unampenda?”
“Walaaa!”
Itaendelea
Hakukumbuka chochote kuhusu mke wake, alimchukia, kila alichosema Juliet alimsapoti, hakukumbuka kwamba zamani hakuwa na pesa lakini msichana huyo alimpenda hivyohivyo, hakukumbuka kwamba utajiri aliokuwa nayo, chimbuko lake lilikuwa kwa wazazi wa mwanamke huyo huyo, hakukumbuka kitu chochote kile, kitu pekee alichokuwa na hamu nacho kwa wakati huo ni kumuua Juliana tu.
Akarudi nyumbani huku akiwa na muonekano mwingine kabisa. Akamkuta Juliana akiwa sebuleni amekaa akimsubiri. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake kila siku, hakukubali kulala na wakati mume wake hakuwa amerudi nyumbani.
Ilikuwa ni lazima kukaa sebuleni mpaka mwanaume huyo atakaporudi nyumbani hapo. Alipokuwa akija, hakuzungumza naye, alimsalimia mwanaume huyo lakini alikuwa kimya, hata salamu hakutaka kabisa.
Siku hiyo Gideon alipoingia, alionekana kuwa tofauti, alipoufungua mlango na kumwangalia mke wake, tabasamu pana likaonekana usoni mwake.
Juliana akashangaa, hakuamini alichokuwa akikiona, hakuwahi kuliona tabasamu la mume wake tangu alipoanza kuugua, leo iweje mwanaume huyo atoe tabasamu pana kiasi hicho?
Kwa tabu sana akasimama na kumfuata mume wake, alipomfikia, akamkumbatia, kwa furaha aliyokuwa nayo moyoni, Juliana akaanza kulia, hatimaye mume wake wa zamani, mume wake yule aliyekuwa kipindi cha nyuma alikuwa amerudi pasipo kugundua kwamba mwanaume huyo alikuwa na jambo lake moyoni mwake.
“Nimekukumbuka mke wangu,” alisema Gideon huku akimwangalia Juliana.
“Nimekukumbuka pia,” alisema Juliana huku akilia kwa furaha.
Wakaongea mengi kama wanandoa, wakaondoka na kuelekea chumbani.
Kila kitu alichokuwa akikifanya, moyo wake ulimuuma mno, hakutaka kumshika mkono Juliana lakini kwa kuwa alitaka kumuua, ilikuwa ni lazima kufanya hivyo.
Akamuacha chumbani na kumwambia kwamba aende jikoni kuchukua chakula na kula. Akaondoka na kuelekea huko ambapo kitu cha kwanza kabisa ni kuchukua simu na kumpigia Juliet.
“Vipi? Umemuua?” alisikika Juliet kwenye simu.
“Bado!”
“Acha ujinga. Unasubiri nini sasa?” aliuliza msichana huyo.
“Ndiyo naandaa mazingira!”
“Au bado unampenda?”
“Walaaa!”
Itaendelea