Joshua Nassari MB.

Joshua Nassari MB.

Na wale wa zanzibari
wanaotaka kujitenga vp?
Tena wanaendesha miha
dhara kila siku nao vp?

mkuu umenena, yaani akifanya mwananchama wa Chadema inakua noma, kule Znz wale wanaoendesha mihadhara wanamwaga matusi mazito ambayo hayavumiliki kwa kua ni CUF, polisi na majeshi yote pamoja na usalama wa taifa hawasemi kitu...
Wakina JK, Sitta, Pinda, JK Nyerere kule Zanzibar kwenye mihadhara wanatukanwa vibaya na Polisi,TISS;FFU wanakua wapo pale pale wanakenua meno..
Kauli ya Nassry imeonekana ni threat kwa serikali???
 
Nassari anataka huruma kama Lulu kutokana na kifo cha kanumba?au?Yeye ni Mbunge anayetokana na Nguvu ya Umma alikuwa akiwaambia Umma sasa huo udogo wake unatoka wapi?Haya maneno aliye yatamka alikuwa peke yake chumbani?Mpaka polisi wamwite kumhoji?Akiri ilikuwa jazba anedelee na shughuli zake za kibunge!

hapa nawaona na nyie mnakurupuka kwa jazba zisizo na msingi!...hivi yeye alivyosema ni mdogo kwani ni lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri?....inawezekana yeye alimaanisha ni "mdogo" kwa wadhifa katika "game" la siasa na si lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri!
 
Nassari anataka huruma kama Lulu kutokana na kifo cha kanumba?au?Yeye ni Mbunge anayetokana na Nguvu ya Umma alikuwa akiwaambia Umma sasa huo udogo wake unatoka wapi?Haya maneno aliye yatamka alikuwa peke yake chumbani?Mpaka polisi wamwite kumhoji?Akiri ilikuwa jazba anedelee na shughuli zake za kibunge!
hapa nawaona na nyie mnakurupuka kwa jazba zisizo na msingi!...hivi yeye alivyosema ni mdogo kwani ni lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri?....inawezekana yeye alimaanisha ni "mdogo" kwa wadhifa katika "game" la siasa na si lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri!
 
POLISI mkoani Arusha jana lilimhoji Mbunge waArumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari kwa zaidi ya saa saba baada yakujisalimisha katika Kituo Kikuu cha jeshi hilo.

Nassari ambaye anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Serikali katikamkutano wa hadhara wa Chadema uliofanyika Mei 5, mwaka huu katika Uwanja chaNMC, alishikiliwa kituoni hapo kuanzia 6:12 mchana hadi saa 12 jioni kishakuruhusiwa kuondoka na kutakiwa kuripoti kituoni hapo leo.

Alifika hapo akiwa na Wakili wake, Arbert Msando bila ya kuwakuta viongozi wajeshi hilo hivyo wakaamua kuondoka.

Lakini nusu sasa baadaye, Naibu Kamishna, Isaya Mungulu na Kaimu Kamanda waPolisi Mkoa wa Arusha, Akilimali Mpwapwa walifika na kuwataka viongozi waChadema, waliokuwa kituoni hapo kuwasiliana na Nassari ili arejee.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Godbless Lema aliyekuwapo aliwasiliana naNassari ambaye alirejea saa 7:20 akiwa na Wakili Msando na alichukuliwa naKamanda Mpwapwa ambaye alimwelekeza kuelekea Ofisi ya Mkuu wa
Upelelezi Mkoa (RCO) kwa mahojiano.

Baada ya kumfikisha Mbunge huyo katika ofisi za mahojiano, Kamanda Mpwapwaalisema kulingana na uzito wa shauri lake atalazimika kutafuta watu wa kumwekeadhamana mara baada ya kuhojiwa.

“Hapa yupo mikononi mwa polisi, atahojiwa na baadaye atapewa dhamana,” alisemaMpwapwa.

Kamishna Msaidizi wa Polisi, Salum Msangi kutoka Makao Makuu ya Idaya yaUpelelezi wa Makosa ya Jinai (CID), ndiye alikuwa akiongoza kikosi maalumukilichokuwa kikimhoji Nassari.

Msangi ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa mpya waSimiyu, alikuwa akisaidiana na Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Hamisi Wariobakutoka ofisi ya upelelezi Mkoa wa Arusha.

ASP Warioba ndiye aliyewahoji watuhumiwa wengine, John Heche na Ally Banangajuzi kwa zaidi ya saa tisa kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku,walipoachiwa kwa dhamana na kutakiwa kurejea jana asubuhi.

Awali, Nassari alieleza alikuwa hana taarifa za kuitwa polisi kwa shtaka lolotebali, mara baada ya mkutano huo wa Mei 5, alipokea ujumbe wa simu kutoka OfisaUpelelezi Mkoa wa Arusha, Faustine Mafwere kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha,Thobias Andengenye alikuwa anamtafuta ili waagane baada ya kuhamishiwa makaomakuu.

“Mimi nimeshangaa leo kusoma katika vyombo vya habari kuwa nasakwa na polisi nandiyo sababu nimekuja kwani awali, nilijua rafiki yangu Andengenye anatakatuagane na nilipanga siku nyingine,” alisema Nassari.


Nassari pamoja na viongozi wengine wa Chadema wanatuhumiwa kutoa kaulimbalimbali za uchochezi ikiwamo, kutishia kujitangazia uhuru wa
Arusha na kanda ya ziwa kama polisi haitawakamata waliohusika na mauaji yamwenyekiti wa chama hicho Kata ya Usa River, Msafiri Mbwambo.

Pia alimtuhumu mtoto wa Rais, Ridhiwan Kikwete kushinikiza uteuzi wa baadhi yaviongozi serikalini.

Bananga ambaye pamoja na Heche pia walikuwa wakisubiri kuhojiwa zaidi janaalisema juzi aliulizwa juu ya kauli zao kwenye mkutano huo, dhidi ya RaisKikwete na mtoto wake Ridhiwan. Huku Heche akisema kwamba aliulizwa juu kauliza Nassari katika mkutano huo.
 
Unajua kwa nn watu wanawadoubt vijana? Ni kwa sababu baadhi yao wanaweza fanya jambo bila impact analysis!
 
Ndiyo maana nilisema haikuwa kauli njema, ila kwanini watu wasijiulize nini kilisababisha atamke kauli ile!
Ukitaka kuuondoa mti mbaya usiendelee kuota unatakiwa ung'oe mizizi yake.
Watu wanapofanya mediation na wanatafuta muafaka huwa wanauliza hivi chanzo ilikuwa nini
Mungi,
Two wrongs doesn't make one right. UVCCM walikosea, je unataka Nassari (au CDM) asawazishe kwa njia alotumia?
 
Kama kijana or rathr mtu yeyote you need to think before yuo speak or do something!
 
sikutegemea kama Nasari ambaye tulimwamini hivi ayafanye haya..ni aibu kwake na wanachadema wenye akili timamu
 
Wewe sio mdogo tena, Umeshapakwa mafuta kuwa mwakilishi wa wameru mashariki wote, Chochote utakachofanya kwa sasa ni msimamo wa jimbo lako chini ya mwavuli wa CHADEMA, kwa hiyo nakuomba umwombe MUNGU akuongezee hekima zaidi, kama mfalme Suleman, Kwa kuwa ameshakupa nguvu kama DAUDI, sasa hivi kwa mkono wa MUNGU unao uwezo wa kumuua GOLIATHI, Kwa hiyo jitahidi usimdhuru SAULI kwa kuwa ni Mpakwa mafuta wa Mungu hata kama anakusudia kumwacha.
 
nasari amepatwa na kichaa au ni ulevi wa madaraka????????????????????????????????
 
Wakuu ile hotuba ya Kamanda Nassari NMC haikuwa imekaa vizuri.
Magamba wataitumia kuishambulia CDM kuwa tunataka kigawa nchi, na itatu cost sana chaguzi zijazo. Pamoja na Kamanda mkuu kuirekebisha Siku ile ni vyema Nassari mwenyewe airekebishe hili swala.
 
Ngoja niweke wazi kabisa; sina tatizo na kauli ya 'kujitenga'. Ni kauli ya kisiasa na imeshawahi kutolewa mara nyingi na watu wa Kigoma, watu wa Mtwara/Lindi, na hata watu wa Pemba.Binafsi hilo halinisumbui sana. Na mtu yeyote anajua aliitoa kauli hiyo kwa maana ya kuweka point ya utani ndio maana alisema "kama Sudan". Haina maana nzito ya kihivyo kwani na wengine wameshatoa kauli kama hizo.

Lakini huwezi kutoa kauli yenye kumtishia Rais na ukabakia hivihivi. Mtagundua kwamba kauli zenye kutishia maisha au usalama wa kiongozi yeyote wa umma huwa hatuzivumilii hapa kwa sababu moja kubwa - siyo watu wote wana akili zilizotulia na huwezi kujua nani akisikia anasukumwa vipi.

Nassari ni kiongozi maarufu sana sasa hivi na ameshinda kwa kishindo kikubwa sana. Kule Arusha ana mvuto mkubwa sana na ni mvuto wa watu kukesha na kumlinda hadi dakika ya mwisho. Chuki dhidi ya CCM ni chuki ya kweli (real hate) na siyo watu wote wanaweza kudumu kwenye chuki hiyo na wakiacha kwenye mambo ya kisiasa tu. Sasa, mbunge maarufu, tena kijana anaposimama na kusema anaweza kumpiga mkwara rais asikanyage Arusha siyo jambo dogo kwa sababu siyo wasikilizaji wake wote wanamuona 'mdogo hivyo'. Nassari ana ushawishi na anamvuto.

Labda watu wengi hawajui historia. Martin Luther King hakuwa na cheo chochote cha kisiasa zaidi ya kuwa mhamasishi mwanaharakati. Lakini mauaji yake yalisababisha miji ya Wamarekani kuingia katika machafuko makali sana. Ni kwa sababu watu walijua ameuawa na mikono ya watu wenye nguvu. Hata Nassari pamoja na "udogo" wake wote hakuna mtu Arusha atapenda anatendewa vibaya au kuonewa na wapo watu wanaoweza kufanya lolote kwa ajili ya utii wao. Nadhani watu wengi wameshasahu kuwa mauaji ya Arusha ya 2011 kwa kiasi kikubwa yalisababishwa na polisi kutumia nguvu dhidi ya watu ambao waliona wanaonewa.

Sasa mbunge anaposimama na kutoa kauli ambayo vyombo vya usalama vinaiona ni ya vitisho dhidi ya Rais ni kutokuwa makini kudhania tu ni jambo dogo. Alichotakiwa kusema Nassari ni hiyo kauli yake ya kwanza tu kuwa hakumaanisha ubaya wowote na kama mtu yeyote amekwazwa anaomba radhi. Lakini siyo kusema kuwa ati yeye ni mtu mdogo na asingeweza kugawa nchi; well hilil ni zaidi ya kugawa nchi. Hivi akisema kuwa Rais asikanyage na Kikwete akaamua kukanyaga na mwehu mmoja akaamua kufanya kitu kibaya kwa msafara wa rais watu watamlaumu mwehu kwa vile ni mwehu siyo? Lakini, yule mwehu ukimuuliza atasema "rais wetu" alitoa amri Kikwete asikanyage Arusha na akakanyaga!

Hii ni sababu moja ambayo inanifanya miye nisiwe shabiki sana ya hoja ya 'uongozi bora ni ujana' kwani tayari tumeshaona mengi yasiyo ya lazima ambayo vijana wameyafanya na kuthibitisha ukosefu mkubwa wa hekima na utulivu unaotokana na busara. Siyo lazima useme kila kinachoingia kichwani hata kama unaamini ni sahiihi. Kuna vingine unaweza kuvisema ila kwa namna tofauti. Hili huwezi kufundishwa shuleni au chuoni!

Ni matumaini yangu Polisi hawatoliendeleza hili na Nassari atakuwa amegundua (sidhani kwa sababu arrogance ya madaraka nayo nimbaya sana!) makosa yake. Sitaki ajisikie ameonewa bali ajue genuinely hakupaswa kutoa kauli hiyo na ni unfortunate. Kwa mfano Lema angekuwa makini na kauli zake wala asingevuliwa Ubunge! HEKIMA, HEKIMA, HEKIMA!!

mfano wako kuhusu Martin Luther King ni mzuri, ila unapingana na point yako! Kilichosabisha mauaji siyo kauli au uana-harakati wake, ni uonevu na matumizi ya nguvu ya polisi! Kumbuka damu ya mwana cdm imemwagwa Usariver, na Nassari aliitoa kauli iyo alipokua akizungumzia umwagaji damu huo! CDM wanaongea, ccm wanaua, fanya uchambuzi wa kina mwanakijiji!
 
Wakuu ile hotuba ya Kamanda Nassari NMC haikuwa imekaa vizuri.
Magamba wataitumia kuishambulia CDM kuwa tunataka kigawa nchi, na itatu cost sana chaguzi zijazo. Pamoja na Kamanda mkuu kuirekebisha Siku ile ni vyema Nassari mwenyewe airekebishe hili swala.

Post nzuri ni ile inayoelezea kauli ilikuwaje iliyotolewa then ndo unatoa ushauri wako, na ambao hatukuisikia inakuwaje ukiandika kama ivyo kuwa ile kauli wengine hatujaisikia
 
Nassari ni mgodo kiumri lakini si mdogo kwa ushawishi wa kisiasa, simply kwasasa ndo mwanasiasa mwenye ushawishi sana nchini kutokana na ushindi wake wa kihistoria kwenye uchaguzi mdogo wa Arumeru! Kwahiyo anapaswa kuacha utoto na maneno ya kwenye campaign na awe kiongozi wa mfano ili vijana tuendelee kuaminiwa na wananchi!
 
ile kauli ya dogo janja isiporekebishwa mapema itaicost sana cdm,dogo janja ningemuona km mweledi sana angeomba radhi,n it was spoken unintentionally.
 
Back
Top Bottom