Joshua Nassari MB.

Joshua Nassari MB.

Uongozi si akili au uwezo wa kuzungumza mtu, kuna vitu vingi vinavyoweza kumpamba au kumbomoa kiongozi.
Vitu hivyo ndivyo vyenye nguvu ya ushawishi. Moja ya kitu hicho ni 'Charisma'- compelling attractiveness or charm that
can inspire devotion in others' ikimaanisha mvuto wenye ushawishi kwa wengine.

Mh Nasari kwa umri wake na CV yake kuwa katika hadhi aliyo nayo ni wazi ana Charisma ya aina fulani.
Charisma hiyo ndiyo inampatia wafuasi waliojitoa(devotion) kwa ajili yake. Hawa watamsikiliza kwa kila jambo na baadhi yao wataziweka fikra zao rehani ili mradi tu kumsikiliza na kumtii kiongozi wao kwa heri au kwa shari.

Hoja ya udogo wa umri na akili haina mantiki hasa tukijua uwezo wake wa kushawishi wana Arumeru kumchagua, pamoja hadhi anaopewa bungeni kama alivyo mzee Samuel Sitta n.k.

Nasari si mbunge mtoto au kijana ni mbunge na kwa taratibu za nchi yetu ni kiongozi wa umma katika hadhi ile ile ya mbunge mwingine. Ni ujuha kudhani kuwa hoja zake zinatapewa hadhi ya utoto.

Tuache ushabiki na tuangalie ukweli. Kauli aliyotoa inamtia yeye mwenyewe doa, CDM na wanananchi anaowawakilisha.
Leo hii akitokea kiongozi kupopolewa mawe au kudhurika kwa namna yoyote kule Arumeru Nasari hatakwepa tuhuma.
Huu ni ukweli hata kama watu hawaukubali. Ni kauli aliyoitoa ima kwa kutojua au kwa bahati mbaya lakini ina madhara

Ukiachilia mbali kauli yake, Nasari anakijengea chama taswira ile ile inayopigwa vita au kushadidiwa na watu kuhusu Ukanda. Ndiyo maana mwenyekiti Mbowe hakusubiri kuikana.

Busara zinasema kuwa, na nimewahi kuandika, ilibidi Nasari aitishe mkutano wa vyombo vya habari na kusema samahani.
Mwendelezo wa malumbano haukitendei chama chake haki na unazidi kutia shaka juu yake na uwakilishi wake.
CDM walipaswa kumshinikiza aombe radhi kama sehemu ya kumlea. Nashangaa anaendelea kutoa kauli tata, hili linammaliza kisiasa na kukiumiza chama chake.

Jambo la kushangaza ni kuwa yapo mengi ya kuongelea katika mikutano, kauli zenye utata ni uchanga wa kisiasa au ukosefu wa malezi ya kisiasa.

Nasari wewe ni kiongozi wa taifa na siku zote fikra na kauli zako zilenge kuleta utangamano kitaifa.
Wewe ni kiongozi kauli zako ni tofauti na kauli za Nasari wa mwaka 2010.
Tumia ushawishi wako, karama na haiba yako katika kufikiria namna ya kuwakomboa Watanzania kutoka katika lindi lenye kina kirefu la umasikini.

Nasari, wewe bado ni mchanga kisiasa, jitokeze na useme neno moja 'Samahani'. Samahani si neno la udhaifu ni dalili ya kukua kifikra, busara na utimilifu wa hekima.
Hiki ni kidonda utakachoishi nacho, dawa si kukifunika ni kukitafutia dawa.
Mdogo wangu dawa ni moja tu na unayo, ulimi wako na kinywa chako
 
Hivi Tanzania yetu hii kuna kitu gani kilicho cha hatari hakijawahi kusemwa au kufanywa?

Wanchi wanapiga kura kumchagua kiongozi wao wanaye mpenda kwa uroho wa madaraka nguvu ya JWTZ UWT na POLISI inatumika kumnyang'anya mtu ushindi.

Nchi nyingine ni sababu tosha kuanzisha vita ya nchi nzima.

Watu wanachukua fedha za miradi ya serikali kama kuchukua fedha kwenye akaunti zao.
Hawaibi tena wameigeuza serikali kuwa PIG BANK

Hivi hili si jambo hatari?

Kauri ya dogo siiungi mkono hata kidogo lakini nafurahi kwamba amesema jambo ili tupime ujinga wa POLISI na viongozi wakuu serikalini. Dogo anatakiwa kujifunza kuunda tungo, aseme jambo hilohilo kwa mpangilio tofauti wa maneno.

Mijitu inaua watu na kutaifisha mali zao haijawahi kuchukuliwa hatua bado inabupumua hewa bure huku inatamba kwa matusi mazito kama kimbuga cha Gafu ya Mexico, sasa mtu kajikwaa ulimi kuongea,mfukoni hana hata kisu cha kukunja anaoneka jasusi muuaji. TOBA!


Dogo usipunguze kasi
 
Amesema jambo ambalo kwa haraka linaonekana lina mantiki lakini linapuuzia uzito wa alichokisema. Kama ni mtu mdogo hivyo aligombea ubunge wa nini? Kama anakosa hekima ya kupima madhara ya maneno yake - watu wanaweza kuumia kwa kauli moja tu ya mtu mwenye ushawishi - kwa sababu yeye ni 'mtu mdogo' ananitisha. Yeye anaweza kuwa na umri mdogo lakini nguvu ya ushawishi wake inashinda baruti na siyo watu wote wanaomsikiiliza wanamchukulia kuwa ni mtu 'mdogo'. grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr

Aliteleza vibaya sana. Huo ndo ukweli. Je, afanye nini sasa? MM hebu tuambie baada ya kufanya kosa lile afanye nini sasa kusawazisha mambo? Najua kuwa Mbowe alilitolea ufafanuzi suala lile haraka sana.
 
CDM wanatakiwa kujua kwamba "mateso yakizidi ujue neema i-karibu
 
Kama huyo mtoto( kwa kauli yake) atakuwa anapata sapoti ya wameru kujitenga basi watanzania wengine tutakuwa hatuna jinsi ila kulikomboa jimbo hill
Uwezo upo, nia ipo, ni wakati tu ukiwadia.
Kama ni noma na iwe noma.
Wengi wenu ham kiwepo 1979 wakati wa Nduli Idi Amin,tunakumbuka kuwa kuna waliomsapoti.
 
Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"
Source;ITV News 2000hrs*

:biggrin1: point well taken
 
Tusiwe na mapenzi kwa chama kiasi kwamba tunatafuta udhuru wa tabia mbovu. Kuna mambo ambayo sasa CDM inapaswa ikemewe na wale wanaoipenda pasi ya kusita. Mambo mengine yakiachwa yaendelee yana matokeo mabovu huko mbeleni.

Mkuu sikufuatilia hotuba yake, lakini kwa hii kauli Nasari akubali kwamba aliteleza kama binadamu, anaposema yeye ni mtu mdogo sana kuigawa nchi ndiyo kanivuruga kabisa, mwanzoni nilimuelewa vizuri kwamba polisi wawatafute haraka hao wauaji wa wanasiasa, hivyo Kikwete kama mwanasiasa na mkuu wa nchi itakuwa ni hatari sana kutembelea eneo lenye mauaji ya wanasiasa ambao hawajatiwa mikononi mwa polisi hivyo asikanyage ARUSHA.
 
.

Sasa mbunge anaposimama na kutoa kauli ambayo vyombo vya usalama vinaiona ni ya vitisho dhidi ya Rais ni kutokuwa makini kudhania tu ni jambo dogo. Alichotakiwa kusema Nassari ni hiyo kauli yake ya kwanza tu kuwa hakumaanisha ubaya wowote na kama mtu yeyote amekwazwa anaomba radhi. Lakini siyo kusema kuwa ati yeye ni mtu mdogo na asingeweza kugawa nchi; well hilil ni zaidi ya kugawa nchi. Hivi akisema kuwa Rais asikanyage na Kikwete akaamua kukanyaga na mwehu mmoja akaamua kufanya kitu kibaya kwa msafara wa rais watu watamlaumu mwehu kwa vile ni mwehu siyo? Lakini, yule mwehu ukimuuliza atasema "rais wetu" alitoa amri Kikwete asikanyage Arusha na akakanyaga!

Hii ni sababu moja ambayo inanifanya miye nisiwe shabiki sana ya hoja ya 'uongozi bora ni ujana' kwani tayari tumeshaona mengi yasiyo ya lazima ambayo vijana wameyafanya na kuthibitisha ukosefu mkubwa wa hekima na utulivu unaotokana na busara. Siyo lazima useme kila kinachoingia kichwani hata kama unaamini ni sahiihi. Kuna vingine unaweza kuvisema ila kwa namna tofauti. Hili huwezi kufundishwa shuleni au chuoni!

Ni matumaini yangu Polisi hawatoliendeleza hili na Nassari atakuwa amegundua (sidhani kwa sababu arrogance ya madaraka nayo nimbaya sana!) makosa yake. Sitaki ajisikie ameonewa bali ajue genuinely hakupaswa kutoa kauli hiyo na ni unfortunate. Kwa mfano Lema angekuwa makini na kauli zake wala asingevuliwa Ubunge! HEKIMA, HEKIMA, HEKIMA!!

Very well said MM.
Ushabiki pembeni, Nassari alikosea na hata sasa hajataka kukubali kosa. Attitude kama hii haiwezi kumfanya kuwa kiongozi bora....time will tell.

Ifahamike kuwa kuna watu wengi sana waliokuwa na superior talents ktk fani mbalimbali lakini hawakufikia kilele cha uwezo wao. Mara nyingi moja ya sababu ni wrong attitude (both mentally and physically).
 
Hapa mimi sikubaliani na wewe kabisa. Udogo anaomaanisha Nassari ni wa yeye kuigawa nchi. Najua hata wewe unajua Nassari hana uwezo wa kuigawa nchi kwa sasa. Na hana maana kwamba kila siku atakuwa mdogo. Haya maneno kayatamka leo lakini haina maana kwamba atakuwa mdogo na kesho pia
Udogo kwa mtazamo wangu mimi ni wa kimamlaka sio wa kiumri. Inawezekanaje kauli yake ionekane tishio kwa kiwongo cha kuifanya jamii iamini kuwa ni ya hatari sana? Ni kweli kwamba hakuna wanasiasa ambao wameshawahi kutoa kauli kali kama au kuliko hiyo? Wamefanywa nini? Nahisi jeshi la polisi haliko makini! Nashwaishika kuamini kuwa wanapokea maagizo katika kushughulikia baadhi ya mambo, hususani yanayowahusu wanasiasa wa upinzani!
 
Ha Ha HA!!! Haya polisi kazi kwenu!
Leo baada ya mahojiano na polisi Arusha mjini zaidi ya masaa sita,Nassari akiongea na waandishi wa habari alisema "Mimi ni mdogo,kama ninauwezo wa kuigawa nchi hii basi nchi hii haikupaswa kuwepo"
Source;ITV News 2000hrs*
 
Nassari anataka huruma kama Lulu kutokana na kifo cha kanumba?au?Yeye ni Mbunge anayetokana na Nguvu ya Umma alikuwa akiwaambia Umma sasa huo udogo wake unatoka wapi?Haya maneno aliye yatamka alikuwa peke yake chumbani?Mpaka polisi wamwite kumhoji?Akiri ilikuwa jazba anedelee na shughuli zake za kibunge!
 
Nchi nyingine wanawatukana maraisi waziwazi hata juwachora cartoon kwenye Tshirts lakini sijasikia kama wanakamatwa mfano raisi Obama. But this is Tanzania beware of what you speak to the public!!!
 
Hakuna chembe ya mantiki hapo hata kidogo ndugu yangu! Amefanya kosa then analeta mzaha. CHE GUEVARA alikufa akiwa na miaka 38, ndani ya muda huo mfupi akawaadabisha mabepari wakubwa kama Marekani.
Kwanza ni kujidharirisha mwenyewe, anajifananisha na mtoto asiyejua jema na baya, hali lukuki ya wana-arumeru wana tumaini naye? Anataka waamini wamekosea kumchagua?
1. Akiri kuteleza ulimi, na kuomba radhi, ni jambo la kawaida sana, sisi kama watz tuko tayari kumsamehe, na ajipange upya, tuko nyuma yake.
2. Chadema itoe tamko la kulaani, na kutoa karipio kwa maneno hayo. Na sio kuishia kusema "hayo sio maneno ya chadema", kwani ametoa nani na wapi?
3. Asipokubaliana na yote hayo, basi chdma kama chama makini, kisisite kumuwajibisha. Lakini sitegemei kufikia huko!
Mungu wetu anaita?

tatizo la msingi kwenye hii habari ni kuwa nje ya "context" kwa makusudi. Nassari amesema maneno mengi lakini watu wana"donoa" maneno machache ili kuharibu maana halisi ya alichosema. Kwa mfano hapa unashupalia yeye kusema ni mdogo tu, lakini pia amesema ilikua kauli ya kuhamasisha mikoa mingine. Pia udogo aliosemea siyo umri, ni cheo chake cha ubunge katika chama chake cdm. Tukitaka kutendea maneno haki, tuyachambue kwa ujumla wake, (katika context) tuache "udonoaji"
 
Acha kujikomba kwa Mzee Mwanakiji amechemka sana. Sidhani kama ni yeye ama kaibiwa password.
Siungi na sikubaliani na kauli ya Dogo Janja, lakini pia sikubaliani na pumba alizoongea MMK. Suala la msingi ni kwamba ile kauli haikuwa kauli ya chama, ndiyo maana ilikanushwa pale pale uwanjani na Mbowe, na hili Mzee Mwanakijiji alijua mapema siku hiyo. Jambo alilotakiwa kulijadili Mzee Mwanakijiji kama nguli humu Jf ilitakiwa iwe ni nini kilisababisha Dogo Janja afikie hatua ya kutamka yale manen, nini kiliwaudhi au kilimuudhi. Hii ndiyo ilitakiwa iwe pakuanzia.
Tusiwe kama wapumbavu wanaopiga vita uvutaji wa sigara wakati huo huo wanasimamia uzalishaji wa sigara.
Hii kauli ya Kaskazini kujitenga mnaona kama kauli mbaya ya kibaguzi kuliko kauli ya uvccm mkoa wa pwani ambayo hadi leo hakuna kiongozi wa ccm aliyethubutu kanusha kwa kumwogopa Riz1! Shame on you guys!
Ni afadhali ya CHADEMA waliothubutu kukanusha kauli ya Dogo Janja pale pale.

Mungi,
Two wrongs doesn't make one right. UVCCM walikosea, je unataka Nassari (au CDM) asawazishe kwa njia alotumia?
 
Hawa mbwa wa ccm (polisi-ccm) wamechoka akili kabisa, mbona hawakumhoji mzee wa matusi, Lusinde?mbona hawakumhoji ridhiwani aliposema rais wa Tanzania hawezi toka Kaskazini?

watanzania tusiendelee kudanganyika na haya magamba tuikomboe nchi yetu toka mikononi mwao!!!!!!!!!!


Peoooooples!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 
Mwanakijiji ameongea vema kuhusu kauli za baadhi ya viongozi wa Chadema akitolea mfano wa Lema kupoteza ubunge ni sababu ya kauli si vitendo. Hali kadhalika Slaa baadhi ya kesi ni lugha si vitendo. Kinachomsumbua leo Nasari ni lugha si vitendo. Nimeongea hili jana hapa jf lakini mdau mmoja alivyoniporomoshea matusi namsamehe kwa kuwa hajui kuwa najua hajui alitetealo.

Elimu ya usemaji ni muhimu sana katika majukwaa, si kupanda na kuropoka kikutokacho kichwani, licha ya kujiandaa namna gani uwepo jukwaani kama alivyotokea mbunge wa Tabora wakati wa Kampeni Igunga kupanda jukwaani na trigger. Profesa moja alituambia chuoni, kama huweze kuwa msetirivu katika mada yako na kushtukia unayumba kutoka nje ya mada jitahidi kuandika na uyasome uliyoyaandaa hadi utakakuwa mzoefu wa kudadafula dhamira inayokusudia bila kutoka nje ya dhamira.

Ni nadharia ya kawaida upandapo jukwaani utakuwa umejiandaa vya kutosha nini utaenda kuongea hadharani. Ni bora uandike na uanze kusoma tangu mwanzo mpaka mwishi kama unaona unashindwa kuzuia ulimi wako kuropoka kila kikutokacho kwani uliyojiandaa huwa umeshayachuja yapi yanafaa kwa watu utakaokutana nao badala ya kuongea tu kukujiacho uwapo jukwaani ndio matokeo yake mbunge anafikia hatua ya kumwekea mipaka Rais wa nchi asigusi ndani ya mipaka ya jimbo au ukanda wake, ni kitu kisichoingia akilini mwa wengi wenye upeo wa kuelewa nini dhamana ya viogozi wetu watarajiwa.

Uongozi bora haupimwi kwa usemaji mwingi jukwaani, bali busara hekima na maoni ya umoja kitaifa ndiyo kigezo cha kujenga nchi kwa amani na utulivu. Siasa inaweza kukugeukia upande mbaya mara moja kutokana na kosa moja tu hata kama umefanya mengi mazuri.

Kesi karibu zote zilizopo mahamakani ni za maneno ya uchochezi, hilo ni jambo ambalo Viongozi wa Chadema wanapaswa kuwa waangalifu sana. Viongozi wa Chadema wasidanganywe na uwingi wa watu kuona kwamba ndio kigezo cha kuongea watakavyo bila kupima nini kinatakiwa kuongelewa katika nafasi walizo nazo mikutanoni na kuonyesha umahiri wao wa kisiasa. Mvuto wa kisiasa ni uwezo wa kujenga hoja nzuri na kuzitetea na wala si kutukana au kusema kauli za kuashiria uchochezi.

Nassari hajagawa jimbo wala mkoa au kanda, pia hajampiga raisi marufuku kukanyaga Arusha! Ametishia kufanya hivyo, kachambue upya hotuba yake
 
Hakuna chembe ya mantiki hapo hata kidogo ndugu yangu! Amefanya kosa then analeta mzaha. CHE GUEVARA alikufa akiwa na miaka 38, ndani ya muda huo mfupi akawaadabisha mabepari wakubwa kama Marekani.
Kwanza ni kujidharirisha mwenyewe, anajifananisha na mtoto asiyejua jema na baya, hali lukuki ya wana-arumeru wana tumaini naye? Anataka waamini wamekosea kumchagua?
1. Akiri kuteleza ulimi, na kuomba radhi, ni jambo la kawaida sana, sisi kama watz tuko tayari kumsamehe, na ajipange upya, tuko nyuma yake.
2. Chadema itoe tamko la kulaani, na kutoa karipio kwa maneno hayo. Na sio kuishia kusema "hayo sio maneno ya chadema", kwani ametoa nani na wapi?
3. Asipokubaliana na yote hayo, basi chdma kama chama makini, kisisite kumuwajibisha. Lakini sitegemei kufikia huko!
Mungu wetu anaita?


hapa nawaona na nyie mnakurupuka kwa jazba zisizo na msingi!...hivi yeye alivyosema ni mdogo kwani ni lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri?....inawezekana yeye alimaanisha ni "mdogo" kwa wadhifa katika "game" la siasa na si lazima nyie m-conclude kuwa ni "udogo" wa umri!
 
Back
Top Bottom