Joshua Nassari MB.

Nasari aliwakilisha kile ambacho viongozi wa Chadema hukisema hasa wanapokuwa wenyewe tu. Kwa hiyo kile alichosema Nasari ni kile hasa Chadema wanaplan kwa nchi yetu nzuri Tanzania.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".

Kadakabikile

Unalipatia hili suala mwelekeo unaoutaka wewe na watu wengine wanaofanana na mawazo kama yako. Msimamo wa CHADEMA katika suala hili uko wazi tangu siku ya kwanza pale pale NMC.

Usiingize maneno yasiyokuwepo kwenye vinywa vya viongozi wa CHADEMA ambao wamedhihirisha pasi na shaka nia na dhamira zao katika kupigania maslahi (haki) ya Watanzania wote, wakiunganisha kila nguvu ya Mtanzania yeyote, wa mahali popote, aliye tayari kujiunga na siasa za vuguvugu kusaka mabadiliko na uhuru wa kweli, hasa mabadiliko ya kiutawala na kimfumo.
 
GRRRRRRRRRRRRRR!!! Wewe ni nani kutoa maelekezo kwa CDM. close your masaburi!! please. Ndiyo JK anaweza kuzuiwa na UMMA wa Atown au popote pale. Si wao ndio waajiri wake. Mnakaa kuanza kutoa woga na kulamba miguu ya waajiriwa wenu BUUREEE! Crazy! Ni wapi umesikia CCM wakiomba radhi kwa niaba ya watu kama LUSINDE aliyekunya kwa mdomo Arumeru!! Ni wapi umesikia CCM ikimkemea NAPE alipowaambia wafuasi wa CDM Mwanza wanashikishwa UKUTA!! Samahani nimetumia maneno kamili ili uelewe.
Wengine JK (mwajiriwa wetu wote) akiguswa mnatepeta ovyooo!!!! Plain stupidity!!
 
Mbona LUSINDE wa CCM alitoa matusi waziwazi na mbele ya kundi kubwa la polisi na hawakumchukulia hatua yeyote hata ya kumwonya tu badala yake alipongezwa na Katibu mkuu wa CCM. Haiwezekani mtu moja afanye kosa hilo hilo au kosa linalofanana na hilo awe hana kosa la kuhojiwa na polisi ila kwa mwingine iwe kosa na polisi wapoteze muda wa masaa sita kuhoji. Nadhani polisi wanatakiwa sasa wabadilike na wasifanye kazi zao kwa shinikizo la kisiasa
 
Mie nada I sio sahihi kuanzia kumpa mheshimiwa rais eti asifike Arusha labda Kama Arusha sio Tanzania kwahiyo dogo umekimbia bungeni endeleza harakati za kuendeleza jumbo Lako usitake kujiingiza ktk mambo ukajivunjia heshima ktk jamii
 


Kitenuly umenena haswaaa! Hawataweza kuzuia nguvu ya mabadiliko ambayo kwa sasa iko wazi sana karibu nchi nzima. Watanzania wameamua kufanya mabadiliko ndani ya nchi hii kupitia CHADEMA. That is their only hope they have to lean on. Hakuna jingine.

Ukitaka kuwaumiza na kuwakasirisha zaidi Watanzania na actually kuwachochea wafanye lolote baya ambalo halijawahi kutokea au kufikiriwa kutokea ni, fanya au onesha mbinu za kutaka kuiua CHADEMA. They are not ready for that...nimeiona hali hiyo Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kusini.

Nikiwa Kanda ya Ziwa juzi juzi, Kamanda Lema alisema wazi kuwa Lake zone si so hot...so hotter than even Kanda ya Kaskazini, tofauti tu ni kwamba Kaskazini inapata publicity sana.
 
Ukweli utabaki pale pale CDM ni wabiga dege wa siasa za kanda

Mmhhh !!



Ila mathalani ukiambiwa uchague 'siasa za kanda' na siasa za 'kudadadeki !!!' utachagua nini ???
Oooops !! Nilitaka kusahau ... Hiyo 'Kudadadeki' ni kwa hisani ya huyo jamaa hapo kwenye picha !!!
 
Poleni makamanda hii ndiyo Tanzania inayoubiliwa na watawala wetu kuwa ina amani na utulivu wakati watu wake wanachinjwa kama wanyama na jeshi la polisi linashangilia kisa CDM.NAKWAMBIA WAKATI HAUWASUBIRI MAGAMBA WATAJUTA.MUNGU YUPO NA KATU HAWEZI KUSHINDWA NA MAGAMBA.MUNGU IBARKI TANZANIA USIKIE KILIO CHETU NA UWAAIBISHI WOTE WANAOWATESA WATU WAKO.
 
Naona watu wengi sana hapa wanataja 'Maslahi ya Taifa'. Hivi maslahi ya Taifa ni yapi hayo ???

Labda mimi nianze kwa kuweka orodha ya maslahi ya Taifa kama ifuatavyo:-
1. Usalama wa nchi na mali zake zote (nchi isije kuvamiwa na kuporwa mali zake)
2. Usalama wa wananchi wake (wananchi wakae kwa usalama na amani)
3. Ustawi wa wananchi (wananchi wastawi kwa kupata huduma nzuri za kijamii na maisha bora)
.
.
n.k.........

Baada ya kuyajua haya na mengine, ndio tunaweza kuzihusisha kauli za wanasiasa na maslahi ya Taifa.
 

I can't believe this. Kwamba Polisi wamemhoji Nassari for 6 hours! Walikuwa wanamhoji kitu gani hasa WASICHOKIJUA????
Hakika HATUNA POLISI NCHI HII! Hivi huyu dogo na MANENO ALIYOTAMKA KUWA ANAWEZA KUMZUIA RAIS WA NCHI JAKAYA KIWETE ASIKANYAGE ARUSHA YANA UKWELI WOWOTE HAPO????Kwa ujinga wa Polisi wetu wanayaona haya maneno kama DEAL na issue nzito ya kupotezea muda!!!!

Nassari ki ukweli HAWEZI KUMZUIA RAIS WA NCHI ASIKANYAGE ARUSHA.Siyo kweli kabisa labda JESHI LA POLISI WATUAMBIE KUWA WATAKUWA WAMESHINDWA KAZI YAO!!!Hivi kama WANAWEZA KUZUIA,KUSAMBARATISHA NA KUUA WAFUASI WA CHADEMA WAKIZUIA MAANDAMANO,WATASHINDWA VIPI KUMSAMBARATISHA JOSHUA NASSARI KWA MABOMU,MAJI YA WASHAWASHA NA RISASI ZA MOTO???

Hapa Polisi na Serikali yao ya CCM hawasemi ukweli. Wanatukumbusha yale maneno ya kipindi cha Uchaguzi POLISI WALIPOSEMA KUWA CHADEMA WALIKUWA WAMEKODI MAKOMANDOO TOKA NJE YA NCHI KUVURUGA UCHAGUZI!!!. Nakumbuka Mhe. Mbowe na Dr. Slaa waliiambia Serikali kuwa KAMA KWELI KUNA MAKOMANDOO WALIINGIZWA NA CDM TOKA NJE BASI HATUNA SERIKALI.

Kwa hiyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa KAMA JOSHUA NASSARI NA WAFUASI WA CDM ATAWEZA KUMZUIA KIWETE ASIKANYAGE 'A' TOWN,THEN HATUNA JESHI LA POLISI,HATUNA UWT,HATUNA JWTZ NA KWA MAANA HIYO HATUNA SERIKALI. MAANA YAKE NI NINI??NI WAKTI WA CHADEMA KUCHUKUA NCHI. Pambaf!

 

Well said my brother,

Niliandika pia siku ya kwanza kabisa kuwa nasary bado mdogo na ni mchanga sana katika siasa. Pia nilisema kuwa nafasi

Ubunge aliyoyano imemzidi umri na uwezo i mean sio saizi yake.

At least umenena kweli.

Ni kwa watu kama wewe pekee ndio jamii hupata manufaa ya kweli.

Well done my brother.
 
Hilo la kugawa nchi ni sera ya Chadema Nassari katumwa tu kusema.

Hiyo ni theory, maana ukiwaza hiyo katika kila eneo, unaweza kukwama.

Hebu check sera za jamaa huyu hapa chini kwenye picha, halafu utumie maoni yako uliyoyatoa hapo kuwa kila mbunge akiongea, basi 'ametumwa', na alichoongea ni 'sera' za chama chake. 'Kudadadeki !!!'

View attachment 53890
 

Mkuu, with all due respect, nadhani hujamuelewa huyu bwana mdogo Mhe. Nassari. Ninaamini hakuzungumzia udogo kwa maana ya umri wake, bali kwa mamlaka.
Hana hata chembe ya dola, huo uhaini ataufanyaje? Mambo mengine ni kutumia logic ndogo tu na si kama walivyolishupalia hao polisi na kulitangaza nchi nzima.
Mhe. kajieleza vizuri tu, kwamba kama kweli walimhitaji wangewasiliana na katibu (wa mbunge) wake, na si kupitia vyombo vya habari au viongozi wake wa kitaifa, kwa sababu hilo suala si la chama ni la kwake binafsi.
Nakuhakikishia hapo hakuna kesi ya maana.
 

Bila samahani ndugu yangu, nilishakusamehe kabla hujawaza kuandika post yako!
Ila tu nikukumbushe kuwa, Dr. Slaa na Chdm inaheshimu sana mawazo yako kama shabiki au mwanachama katika kuimarisha chama. Kudhania kuwa raia hana mchango wowote katka uwajibikaji wa viongozi ndiko kulipotufikisha hapa tunapopalalamikia leo.
Nakushauri, acha ushabiki tumia mantiki katika kuhoji mambo! Pole sana kwa kujidharirisha, ila usiumie sana bado una nafasi ya kuonesha kuwa unaakili, uliteleza tu na hukuanguka, kama alivyoteleza Nassari.
Mungu wetu anaita!
 
Bwana RAGE alipanda na bastola Igunga jeshi halikuona,bwana Mkama akatoa kauli nzito za makomando na walikopata mafunzo bila vielelezo polisi wakaishia kusema CDM iwashtaki kwani wao hawajui,leo kijana kasema hli neno wao wamelipandia juu.Ukweli ni kwamba CCM wanawatumia polisi kuwatishia watanzania wasifuate njia ya haki lakini hatuchoki kama GADDAF na wenzake walishindwa na utajili wao wote na nyie magamba mtashinwa tu.Ebu ona kesi za kupinga uchaguzi zlivyo kibao kwa USHINDI WA CDM alafu wanajitetea kutohuska na mauaji wakati mnakataa ushindi wa kweli.POLENI MAGAMBA MAANA HAMNA TENA JIPYA.WATU WANAJUA KUWA MNAWADANGANYA KWA VISINGIZIO VISIVYO NA MASHIKO.NA MKOME KUTUDHARAU WATANZANIA KANA KWAMBA HATUNA MACHO HATUONI!
 

Our system had detected that you are either nasari or close aide of him.

Automatic generated report, on wednesday 9th may 2012 at 2:40 GMT
 
mimi naipinga vikali kauli ya nassari.kwani ina weza kurudisha nyuma maendeleo ya chama!
 
Hebu tuache maskhara. Hili suala la Nassari limekuzwa kupita kiasi. Kwanza sio "tamko"; hiyo ni "kauli" tu! Halafu sitaki kuamini kwamba watanzania wengi tu wajinga kiasi cha kuweza kutetereshwa na kauli ya bahati mbaya ya mh. Nassari. Tunaelewa tofauti kati ya mizaha ya kisiasa na matishio ya kweli toka kwa wanasiasa. Pita mitaani hivi sasa uone wananchi wangapi wana hata hiyo habari ya alivyosema Nassari. Mh. Mbowe keshaweka mambo sawa na cha maana ni kumsaidia mh. Nassari aende taratibu na maneno. Naona kama hizi ni njama za kupunguza makali kwa wahujumu wa kweli wa nchi hii ambao ndio tishio kubwa sana la amani na utengamano wa taifa letu. Let's stop this misdirected non-issue!
 

Our system has detected that you are either nasari or close aide of him.

Automatic generated report, on wednesday 9th may 2012 at 2:40 GMT
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…