Wakati fulani nadhani kijana yuko sahihi sana, nchi inatafunywa eti kanda kati, mashariki, kusini kabisa (Mbeya na Iringa) magharibi wanabweteka na CCM, yuko sahihi kutoa mawazo yake. Alichofanya shujaa huyu kinyume na wewe ni kusema anachodhani kifanyike, wewe ni uoga unakusumbua. Inafikia wakati unafikiri tugawanye nchi kwa faida ya kila kundi; Kama Kanda ya ziwa, Kaskazini wamechoka kuibiwa na nyinyi bado mnafurahi kuibiwa kwa faida ya wote si tuachane kwa mtiririko huo? anakosa gani sasa kusema mawazo yake???
Kwa mwenye akili kama kasikazin na kanda ya ziwa, kijana alimanisha tunachoka kusubiri watu ambao hawaji huku nchi inaisha kwa wizi wa kila siku. tunachoka kusubiri TABORA waamuke, Tunachoka kusubiri Pwani, Mtwara na Lindi, Ruvuma, Dodoma tumechoka; Inawezekana tunasubiri mtu mfu aamke, tutasubiri mpaka tufe!!!
Kama nchi ni moja mbona wenzetu mko kimya na wizi huu, mtasababisha tufe masikini nchi nzima eti tunawasubiri muamke, huenda mmelizika sasa tunafanyaje? ni haki yenu kulizika lakini ni haki yetu kusema endeleni na sisi tuendeleee kivyetu. au kuna ubaya???
Tunaipenda TZ moja lakini kwa usaliti huu, Tabora, Pwani, Dodoma, Ruvuma, Mtwara, Lindi, pengine na Dar TUMECHOKA, amkeni kelele ziishe la sivyo kijana kasema tu moja ya option.