Joshua Nassari MB.

Huenda hamkumuelewa Nassari kuhusu "udogo" wake. Amesema yeye ni mdogo, hajafafanua udogo katika umri, umbile au ushawishi. Kwa kauli ya kusema "basi hiyo nchi haipaswi kuwapo", mimi nimemuelewa kwamba alikuwa anazungumzia udogo wa ushawishi!
 
Nassari kakosea na kama ndivyo wote tunakubaliana hivyo basi hana budi kuwajibika kwa makosa yake kwa kukiri kwa maandishi amekosa kisha turuhusu utaratibu mwingine uendele, hata tukisema maneno billion mia ya kujaribu kumdis credit Dogo bado haitoshi kumhukumu kwamba mtazamo wake ni mfupi. Hivyo basi tukubali kosa lime kwisha tendeka kilicho baki ni kusonga mbele katika kulijenga taifa...!
 

Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Lakini nadhani nchi hii inahitaji watu watakaotibua hali ili watawala wetu wapate akili. Nakumbuka kuna wakati Mh Mbowe alisema inabidi wakati fulani pawe na Civil disobedience, je utasema Mbowe alikosea? Ni kwa sababu utawala uliopo hauwezi usikia vilio vya watu bila kauli kali kama hizi. Kwa nchi yenye demokrasia ya kweli na iliyotulia, na ambayo viongozi wake ni wasikivu kwa matakwa ya raia wake, kauli ya Nassari ingekuwa mbaya sana, lakini si kwa serikali kama yetu, ambayo kwa kutumia jeshi la polisi wanaifichia CCM ukweli wa mauaji wanayoyafanya kwa viongozi na makada wa vyama vya upinzani.

Natamani kauli kama hizi ziwe nyingi ili kuwaamusha wananchi na kuifanya serikali hii izinduke. Msimamo wangu siku zote ni kuwa CCM haindoki kwa lugha laini laini, lazima iambiwe maneno magumu ambayo hata wakiyasikia masikio yawe yawashwe.

Wito kwa Polisi wetu; acheni kufuatilia mambo yasiyo na umuhimu na kujaribu kuyakuuuuuza; kumbuka walivyomkamata Mbowe kule Dar na kumpeleka Arusha, nguvu kubwa inatumika kwa mambo madogo sana. Wao wanajua kuwa pamoja na Nassari kutamka yale maneno, hana uwezo wa kufanya lolote, ama wananchi wa Arusha hawawezi kufanya chochote kwa kauli ile; kwa nini msifanye mambo muhimu kwa nchi hii?
 

Kwa mtazamo huo wako, hapo ndipo unapo gundua uogaa na uchanga wa siasa ulio gubikwa na unywaji wa juice ya maji ya bendera ya jembe na nyundo.... hili linatosha kuonyesha jinsi gani mabadiliko kwa CCM ni sawa na mtu kukalia mafiga ya moto... lazima muogope....!
 
Kumbe ni kweli Chadema mnataka kujitenga...

CDM itajitenga vipi wakati wimbi la mageuzi sio la Arusha tena. Nenda Bukoba, mpaka Songea; anzia Musoma mpaka Tunduma, kote huko CDM inapaa kwa kasi, sasa CDM itajitengaje? Tumia akili ndogo tu. Lililo wazi ni kuwa CCM bye bye
 
[h=3][/h]
POLISI mkoani Arusha jana lilimhoji Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari kwa zaidi ya saa saba baada ya kujisalimisha katika Kituo Kikuu cha jeshi hilo.

Nassari ambaye anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Serikali katika mkutano wa hadhara wa Chadema uliofanyika Mei 5, mwaka huu katika Uwanja cha NMC, alishikiliwa kituoni hapo kuanzia 6:12 mchana hadi saa 12 jioni kisha kuruhusiwa kuondoka na kutakiwa kuripoti kituoni hapo leo.

Alifika hapo akiwa na Wakili wake, Arbert Msando bila ya kuwakuta viongozi wa jeshi hilo hivyo wakaamua kuondoka.

Lakini nusu sasa baadaye, Naibu Kamishna, Isaya Mungulu na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Akilimali Mpwapwa walifika na kuwataka viongozi wa Chadema, waliokuwa kituoni hapo kuwasiliana na Nassari ili arejee.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Godbless Lema aliyekuwapo aliwasiliana na Nassari ambaye alirejea saa 7:20 akiwa na Wakili Msando na alichukuliwa na Kamanda Mpwapwa ambaye alimwelekeza kuelekea Ofisi ya Mkuu wa
Upelelezi Mkoa (RCO) kwa mahojiano.

Baada ya kumfikisha Mbunge huyo katika ofisi za mahojiano, Kamanda Mpwapwa alisema kulingana na uzito wa shauri lake atalazimika kutafuta watu wa kumwekea dhamana mara baada ya kuhojiwa.

“Hapa yupo mikononi mwa polisi, atahojiwa na baadaye atapewa dhamana,” alisema Mpwapwa.

Kamishna Msaidizi wa Polisi, Salum Msangi kutoka Makao Makuu ya Idaya ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CID), ndiye alikuwa akiongoza kikosi maalumu kilichokuwa kikimhoji Nassari.

Msangi ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa mpya wa Simiyu, alikuwa akisaidiana na Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Hamisi Warioba kutoka ofisi ya upelelezi Mkoa wa Arusha.

ASP Warioba ndiye aliyewahoji watuhumiwa wengine, John Heche na Ally Bananga juzi kwa zaidi ya saa tisa kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku, walipoachiwa kwa dhamana na kutakiwa kurejea jana asubuhi.

Awali, Nassari alieleza alikuwa hana taarifa za kuitwa polisi kwa shtaka lolote bali, mara baada ya mkutano huo wa Mei 5, alipokea ujumbe wa simu kutoka Ofisa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Faustine Mafwere kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa Arusha, Thobias Andengenye alikuwa anamtafuta ili waagane baada ya kuhamishiwa makao makuu.

“Mimi nimeshangaa leo kusoma katika vyombo vya habari kuwa nasakwa na polisi na ndiyo sababu nimekuja kwani awali, nilijua rafiki yangu Andengenye anataka tuagane na nilipanga siku nyingine,” alisema Nassari.

Nassari pamoja na viongozi wengine wa Chadema wanatuhumiwa kutoa kauli mbalimbali za uchochezi ikiwamo, kutishia kujitangazia uhuru wa
Arusha na kanda ya ziwa kama polisi haitawakamata waliohusika na mauaji ya mwenyekiti wa chama hicho Kata ya Usa River, Msafiri Mbwambo.

Pia alimtuhumu mtoto wa Rais, Ridhiwan Kikwete kushinikiza uteuzi wa baadhi ya viongozi serikalini.

Bananga ambaye pamoja na Heche pia walikuwa wakisubiri kuhojiwa zaidi jana alisema juzi aliulizwa juu ya kauli zao kwenye mkutano huo, dhidi ya Rais Kikwete na mtoto wake Ridhiwan. Huku Heche akisema kwamba aliulizwa juu kauli za Nassari katika mkutano huo.



CHANZO - Mwananchi
 

Nyie mtaendelea kulumbana kuhusu Nassari wakati wenzenu wako busy wanaiba mali za umma,mkikurupuka toka kwenye malumbano trivio haya mtakuta mabilioni yamevunwa kama mlivyofanywa kwa babu wa Loliondo.

DON'T SAY I DID'NT WARN YOU, au mmewasahau CCM nyie?
 
Sio udogo wa umri udogo wa mamlaka mbona hamfikirii mbali. Ni vizuri kutafakari habari ndio ujibu.
 
Habari ya KAULI ya NASSARI kijana mdogo asiyemiliki hata mgambo kumi, ni kukwepa majukumu na mambo ya msingi yanayotukabiri... tunataka Kusikia Nini hatima ya TANESCO,ATCL,EPA,KAGODA,DOWANS,...NK , Nini Hatima ya MAIGE na TWIGA wetu na MENGINE mengi yanayofanana na HAYA.
 
We pia pata moja kwa bili yangu
 
jmushi1 Verbatim? Tangu lini tukaanza kudaiana ushahidi wa namna hiyo?Hebu tujadili hoja hapa.Kama Nassari alikuwa sahihi ni kwa nini Mbowe alimkanusha on the spot??
Kigarama,unafahamu maana ya verbatim?Huoni mjadala ungekuwa vyema baina yetu kama ungeweka hayo maneno kama alivyoyasema?
 
Last edited by a moderator:
Watanzania si wapumbavu kiasi hichu, kumsikiliza mtu mmoja na kufanya maamuzi, na wala Mh. Nasari hana uwezo wowote kushindana na dora, wananchi wanasikiliza wanatafakari na mwisho wanafanya maamuzi. Serikali itambue hilo na polisi walijue hilo, hatutarajii kumsikiliza mtuu kwa jambo la kipuuuzi hivyo kukusanya watu zaidi ya 1000 wakakusikiliza ujue unajambo la msingi na si uchochezi! Mahakama, polisi muda wa kutetea maovu umekwisha umebaki tu muda wa kuadhibu mafisadi only.
work up my people, our country has been destroyed, where shall we get it once again?:baby::baby:
 
Nadhani Nassari sasa anona jinsi alivyo na nguvu katika jamii, ili suala bado linajadiliwa tu!!

Dogo jirekebishe, wewe una nguvu kubwa sana kwenye jamii tambua hilo kwanza halafu zingatia kuwa ulimi ni kiungo kidogo kinachoweza kuleta balaa katika jamii yetu!!

Kisiasa kuwa chonjo na kauli pia magamba yanatufuatilia nyendo zetu!!
 
Mwenyekiti wa CDM ambaye ndiye kiongozi wajuu kabisa wa chama kapinga vikali kauli za Huyo dogo Nassari sasa nashindwa kuwaelewa watu wanaounga mkono kauli ya Nassari,kwa maana nyingine wanampinga mwenyekiti wa CDM!Sitakosea nikiwaita washabiki uchwara wa CDM wanaokwenda kama ng'ombe kufuata miluzi ya mchungaji (Mchungaji wa ng'ombe)
 
We pia pata moja kwa bili yangu
 
Nimeipenda sana hii Comrade umetoa elimu ya juu sana,nchi tushaiweka mikononi mwetu sasa taratiiibu kuelekea Ikulu cha msingi tusiache majeruhi wengi sana

Ni kweli kabisa kwenye ndoto ukiwa umelala mchana linawezekana kabisa hata kuchukua serikali ya dunia
 


Mwanakijiji...no more to add on top of this.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…