Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu

Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu

Ukitoa maoni uwe na uwakika nayo sio kujisemea semea tu, nakukumbusha kidogo, Sugu alichangia sana kuhusu Twiga na wanyama pori waliotoroshwa kutoka nchini kwenda nchi za watu, amechangia sana kuhusu wizara ya mambo ya ndani na kumuhasa Nchimbi kuhusu wizara hiyo, Wizara ya Uchukuzi kuhusu uwanja wa ndege wa Songwe na mengine mengi saaaaaaaaaaana ya Jimbo lake. Kaa sikiliza bunge wewe kilaza ndo ulete hoja
 
You can't expect more from him. He's Form 4 leaver.

hata kama ni form 4 ila utendaji wake ni zaidi ya akina magembe na ma dr. Kibao cjui niwa kupewa waliojaa ccm na maelimu yao pasipo na utendaji unaoridhisha kama elimu yao ilivyo ya hali ya juu!
 
Mbeya walichagua aina ya Mbunge na si Mbunge. Hata Masela wake hapa mwanjelwa saivi hawamtaki.
 
Ila hayupo peke yake wapo kina Lema, Mnyika....ndani ya chama wana manufaa kweli, wao wanaagizwa tu wewe mtukane raisi, wewe mtukane waziri mkuu.....

Ndio maana wale wanaojitambua kama Zito, Baregu, Shibuda hawana mvuto sana kwenye uongozi.

Mtukane tu ila ipo siku utajikuta upo man to man na mzee Mizengo, ametinga uzi wa taikwondo ndio utaanza kulia kuomba msaada......dokta Wily............Freeeman........Babu Eduuuuuu, saizo wapo kirima juu wanaria mbeke.

Unapewa Takwondo za kijapani ukitoka hapo viungo vyote vimekuwa displaced...miguu ipo mikononi...mikono miguuni...pua ipo kisogoni....

Ukikutana na dokta Wiliburodi lazima atoke nduki, na hivi tu gari yake ikifuatwa nyuma na gari nyingine anatamani ageuke Filbert Bayi ateremke akimbie kwa miguu (ila watu wa kule nawaaminia kwa nduki)....
breki ya kwanza karatu.......kurudi mjini majaliwa......chezea viumbe kutoka sayari ya Mars.

Na huyo ndio mgombea wenu wa kudumu, Itawabidi mtafute mgombea mwingine...ndio itakuwa imekula kwenu.
 
Mbona mimi nimewahi kumsikia akiwatetea machinga bungeni, au wewe ulikuwa Malawi?
 
Mleta uzi kachukuwe biku 7 yako.wana mbeya ndio wanamaamuzi kama sugu anafaa au hawafai..mpumbavu mkubwa na mchonganishi...gamba mkubwa wewe.chadema hakuna waropokaji kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mambo ya chama.huwa wanavikao vya cha ma vinavyoongelea matatizo yao.wewe kalia biku 7 mjinga wewe kama mwigulu.


Du sasa wewe na mleta mada nani ni mropokaji kwenyecmitandao ya jamii? Au stahili yako ya uropokaji ndiyo inaruhusiwa na chama chenu cha Chadema?

Mkiambiwa ukweli mnatokwa na povu. Mleta hoja anawashauri kuhusu mwenendo wa Sugu kwa maoni yake, kumbuka siovwana chadema wote wenye nafasi ya kushiriki na kuongea kwenye hivyo "vikao vyenu" unavyovisema. Maendeleo ya teknolojia yamewezesha mtu yeyote kufikisha mawazo yake kwa njia kama hizi, ni juu yenu "ninyi" wafanya maamuzi kuchuja zipi pumba na upi ni mchele.

Nimepata nafasi mara kadhaa kuongea na wana Mbeya Mjini, na wao wanamuona Sugu kama mzigo kwao. Kazi yake kubwa anayofanya akiwa jimboni ni kuandaa maandamano tu, hana kitu kingine anachofanya. Wana Mbeya wamewahi kumwambia kuwa abadili timu yake ya wasaidizi/washauri lakini alidharau na kuendelea nao hao hao kina Mkoloni na Dani Msimamo (wasanii wa bongo flava).

Kumbuka gari bovu halivutwi na gari bovu.

Come 2015, chama chochote cha siasa kitakachosimamisha mgombea smart, na chadema wakamng'ang'ania Sugu basi chadema wawe tayari kuachia jimbo.
 
Mkuu Ritz mbona hata wewe kwenye mijadala ya Kiingereza humu ndani huwa unaingia mitini?
huyo ni Emirates gold member wasafiri wote wakimjua, uingereza huwa anaenda kama anavyoenda Kariakoo... Kwa hiyo acha kumwaibisha Abu Jahl..
 
Last edited by a moderator:
Kwanza nadeclare interest me ni CHADEMA.
Huyu mkuu huwa hachangii chochote akiwa bungeni, labda ishu ihusu bongo fleva au Ruge.
Ameshindwa hata na Maji marefu ambaye huuliza maswali ya nyongeza na ya msingi kuhusu wapiga kura wake.
Ivi Mbeya mjini hamna matatizo ya maji, barabara , shule na clinic kweli?

Anadhani alichaguliwa kwa ajili ya kuongelea hati miliki za wasanii?

naona bangi ya leo ulichanganya na kinyec cha nguruwe jombaa!
 
Mkuu kitendo cha wewe kusema "uliwahi kumsikia" tayari ni uthibitisho tosha.
Hayo maneno usingeweza kuyatamka kwa Mnyika.
Afu hiyo wizara haihusu bongo fleva tu, kuna netball,bao etc.

Jambazi funguka mkuu inawezekana mna ugomvi binafsi na hapa hakuna atakaendekeza hayo. Yule Mbunge wa Rorya aliyewahi changia mara moja tu na wengine wengi unasemaje au wewe umemwona tu Sugu ambaye hata hotuba anasoma?
 
But very JEMBE

Hawa wanataka kusifiwa kila wakati na ukiwasema tu mitusi lukuki. Hata akiwa form four anaweza toa maoni mazuri ya kujenga kuliko hata graduate....education doesn't make some one intelligent but sees the world differently......
 
Mbona anatimiza wajibu wake ! Au mpaka wewe uone?
 
Jamaa jembe huyo,wala huwezi Tia mguu hapo.ila kwa sababu tu democracy tumbukia tu utimize ndoto yako kuwa na ww uligombea

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Sugu Hana chake Mbeya......kila mtu anajua Hilo na hata mwenyewe analifahamu Hilo....alichoweza kufanya katika miaka miwili na nusu ni kuwananga Clouds na kusambaza album yake ya Ant-virus
 
Mzee wa Ant-virus Hana chake Mbeya maneno mengi na kuwashambulia clouds
 
Back
Top Bottom