John Heche: CHADEMA haiko tayari kwa Maridhiano

John Heche: CHADEMA haiko tayari kwa Maridhiano

Huu ndio msimamo makini sana. Najivunia sana kushabikia chama kinachojitambua. Kuna wajinga wanadhani bado cdm ni chama kinachotetemekea ruzuku. Cdm imeshavuka hatua ya kutegemea ruzuku, maana hiyo ilitumika kuvuruga vyama vya upinzani. Msimamo ni huo huo. Bigup cdm.
stakehigh ERTUGRUL BEY HAYA LAND HOV THE BIG SHOW
Huu si msimamo wa Chadema ni msimamo wa wananchi wote. Heko CDM
 
Hakuna maridhiano na wauaji.

Wauaji wakaridhiane na maiti walizozifukia katika makaburi ya halaiki.
 
Mimi zitto kabwe na ndugu yangu salumu mwalimu tutaenda mapema sanaaaa kuridhiana na CCM
 
Nilishashauri hakuna haja ya maridhiano na hawa wahuni. Serikali isonge mbele kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kwa sababu miaka 5 ni michache mno. Tusipoteze kuridhiana na wahuni aina ya Heche.
Mkiendelea na huu utaratibu wenu wa kuwatawala wananchi kwa nguvu, huku mkitegemea nguvu ya vyombo vyenu vya dola (na hasa policcm) kuwalinda; mtegemee majanga zaidi siku zijazo.

CHADEMA walihitaji uwepo wa tume huru ya uchaguzi! Nyinyi mkaamua kubadilisha tu jina, ila tume ya uchaguzi imebakia kuwa ile ile ya mwenyekiti wa ccm kuwateua makada wenzake wa ccm kuwa wasimamizi wa uchaguzi! Huu ujinga haukubaliki.

Wananchi wengi tumeamua kususia zoezi la uchaguzi kwa sababu tu ya ubinafsi wenu! Kama kweli mnapendwa na kukubalika, kwa nini msiruhusu uwepo wa tume huru ya uchaguzi! Tume ambayo haifungamani na mgombea wa chama chochote cha siasa, ili wananchi wawachague wagombea wanao wapenda kwa uhuru na uwazi?
 
Jamaa wanabeba iman ya watanzania hawana ndumi mbil
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema hakitakuwa tayari kwa maridhiano yenye kupumbaza, kuhadaa, yenye ulaghai na yenye kuliondoa Taifa kwenye ukweli, haki na kile ambacho Taifa inataka na kusisitiza kuwa kamwe CHADEMA haitowasiliti Watanzania.

Akiongea leo January 03,2026, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche amesema “CHADEMA, Chama chenu hakitakuwa tayari kwa maridhiano yenye kupumbaza, kuhadaa, yenye ulaghai na yenye kuliondoa Taifa kwenye ukweli, haki na kile ambacho Taifa inataka, kamwe hatuwasaliti Watanzania”

“Ni ubatili na dharau kubwa kwa Watanzania kuyaita maridhiano sasa katika mazingira ambapo Serikali iliamua kwa makusudi kuwapuuza Wananchi, Vyama vya siasa na Wadau wa demokrasia juu ya hitaji la nchi kuhusu mabadiliko (reforms) ya mifumo ya uchaguzi nchini, uchaguzi batili hauishii kwenye siasa pekee, huingia moja kwa moja kwenye tumbo la mwananchi na heshima ya maisha yake ya kila siku”

“Leo ninapotoa salamu hizi ni siku ya 269, tangu Mwenyekiti wetu, Tundu Lissu alipokamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kesi ya uongo, batili na yenye uonevu wa makusudi wakidhani atapiga magoti kusujudia sanamu”.
Asante kwa bandiko hili, kwa ruhusa yako naomba kulitumia hili bandiko kama mbegu ya kuoteshea bandiko langu fulani.

P
 
Huu ndio msimamo makini sana. Najivunia sana kushabikia chama kinachojitambua. Kuna wajinga wanadhani bado cdm ni chama kinachotetemekea ruzuku. Cdm imeshavuka hatua ya kutegemea ruzuku, maana hiyo ilitumika kuvuruga vyama vya upinzani. Msimamo ni huo huo. Bigup cdm.
stakehigh ERTUGRUL BEY HAYA LAND HOV THE BIG SHOW
kwan kaitwa kwenye maridhiano? hajashiriki uchaguzi maridhiano hayamhusu
 
Asante kwa bandiko hili, kwa ruhusa yako naomba kulitumia hili bandiko kama mbegu ya kuoteshea bandiko langu fulani.

P
Weka utakavyo, uje na zile porojo zako kwamba cdm wanakosea kutoshiriki maridhiano, wakati ACT walijipendekeza kwenye tume ya professor Mkandala na bado wampiga kidole cha kati. Kwenye uzi wako usisahau Samia aliingia na hadaa ya 4r's lakini zimebaki kulazimishwa kisiasa zaidi na wanaccm, wakati uhalisia unakataa na kinachohubiriwa.
 
kwan kaitwa kwenye maridhiano? hajashiriki uchaguzi maridhiano hayamhusu
Ameweka record sawa tu, maana tapeli anahadaa kuwa atashirikisha makundi yote. Ashirikishe makundi ambayo bado hayajamstukia kuwa ni tapeli.
 
Ameweka record sawa tu, maana tapeli anahadaa kuwa atashirikisha makundi yote. Ashirikishe makundi ambayo bado hayajamstukia kuwa ni tapeli.
huyo hausiki anatafuta tu kiki
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema hakitakuwa tayari kwa maridhiano yenye kupumbaza, kuhadaa, yenye ulaghai na yenye kuliondoa Taifa kwenye ukweli, haki na kile ambacho Taifa inataka na kusisitiza kuwa kamwe CHADEMA haitowasiliti Watanzania.

Akiongea leo January 03,2026, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche amesema “CHADEMA, Chama chenu hakitakuwa tayari kwa maridhiano yenye kupumbaza, kuhadaa, yenye ulaghai na yenye kuliondoa Taifa kwenye ukweli, haki na kile ambacho Taifa inataka, kamwe hatuwasaliti Watanzania”

“Ni ubatili na dharau kubwa kwa Watanzania kuyaita maridhiano sasa katika mazingira ambapo Serikali iliamua kwa makusudi kuwapuuza Wananchi, Vyama vya siasa na Wadau wa demokrasia juu ya hitaji la nchi kuhusu mabadiliko (reforms) ya mifumo ya uchaguzi nchini, uchaguzi batili hauishii kwenye siasa pekee, huingia moja kwa moja kwenye tumbo la mwananchi na heshima ya maisha yake ya kila siku”

“Leo ninapotoa salamu hizi ni siku ya 269, tangu Mwenyekiti wetu, Tundu Lissu alipokamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kesi ya uongo, batili na yenye uonevu wa makusudi wakidhani atapiga magoti kusujudia sanamu”.
Leo ninapotoa salamu hizi ni siku ya 269, tangu Mwenyekiti wetu, Tundu Lissu alipokamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kesi ya uongo, batili na yenye uonevu wa makusudi wakidhani atapiga magoti kusujudia sanamu”. 📌🔨✌🏿💪🏿☄⚡
 
Hakuna Maridhiano na Shetani
IMG-20260102-WA0049.jpg
 
Back
Top Bottom