Joe Biden achaguliwa kuwa rais wa 46 wa Marekani

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Ushindi wake unakuja baada ya kushinda kwa kishindo jimbo la Pennsylvania.

Anakuwa Rais wa kwanza kuingia Madarakani akiwa na umri mkubwa (miaka 78). Pia, Marekani imepata Makamu wa Rais wa kwanza Mwanamke, Kamala Harris.



BIDEN: NITAWATUMIKIA WALIONIPIGIA NA WASIONIPIGIA KURA

Mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Marekani katika Nafasi ya Urais, Joe Biden amewashukuru wamarekani kwa kumpa dhamana ya kuongoza taifa hilo

Katika tweet yake amesema atawatumikia wote bila kujali kama walimpigia kura au ambao hawakumpigia kura

Ameahidi kutowaangusha kwa imani ya uongozi ambayo Wananchi wamempa kwa kipindi hiki

Rais Mteule wa Marekani Joe Biden

Kamala Harris Mwana Mama wa kwanza katika Historia ya Marekani kuwa Makamu wa Rais.

=====

 
Nimeumia mno, ila ndo hivyo tujipange 24
Mgombea wako alikuwa na character flaws nyingi mno!

Kapata kura zaidi ya milioni 70 na bado kashindwa!

Hakuna mgombea mwingine wa urais aliyewahi kupata kura nyingi namna hiyo na akashindwa.

Biden kapata kura milioni 74.

Nyingi ya hizo kura si za Biden. Ni kura dhidi ya Trump.

Trump angerekebisha tabia yake na kuachana na beef za Twitter na kuacha kutoa kauli za ajabu ajabu, naamini wananchi wangemsamehe licha hata ya janga Corona maana hakulisababisha yeye.

Watu walichoka na drama zake na tabia zake zisizo za ki presidential.
 
Bila shaka wapigakura wa US wanaongezeka kila baada ya miaka 4. Miaka ijayo kunaweza kuwa na mgombea ambaye atapata kura mil 100 na atashindwa, kulingana na population ya wapigakura ya mwaka huo.
Kapata kura zaidi ya milioni 70 na bado kashindwa!

Hakuna mgombea mwingine wa urais aliyewahi kupata kura nyingi namna hiyo na akashindwa.
 
Leo projections zinaonesha Joe Biden ni president Elect wa US

Kama tulivyomsikia na tulivyozoea sera za Democrats kwa mambo ya nje ni kuingilia au kujali sana mambo ya Africa tofauti na Trump alivyoyapa kisogo!!

Biden aliahidi ku deal na democrasia za Africa kama ilivyokua kwa Obama.

Afrika na mafashisti wake wajiandae maana huyu bwana na Chama chake watatuletea tena mambo ya Arab Spring!!
 
Nimeumia mno, ila ndo hivyo tujipange 24
24, mnataka Trump asimame tena, au someone else?!

Kama mnamtarajia Trump tena, then tell that old man to stop being too arrogant!! Arrogance yake towards anyone else imem-cost huku matokeo yake anaelekea kupoteza hata senate majority!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…