Mahakama ya juu zaidi Marekani yapiga marufuku jimbo lolote kumzuia Trump sanduku la kura, Wasiempenda anazidi kung'aa, Biden kaiharibu nchi

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,080
wabunge na vyombo vya sheria vya majimbo yaliyoshikiliwa na chama cha Democrats anachotokea Rais Biden yamekuwa yakifanya michezo michafu kukwamisha jitihada za Trump kugombea uraisi 2024.

Jimbo la Colorado lilimumuondoa Donald Trump kwenye sanduku la kura na majimbo mengine yalikuwa kwenye mchakato huo.

Leo hii mipango yao imefeli, Mahakama ya juu zaidi Marekani yaamuru Donald Trump anaweza kubaki kwenye kinyang'anyiro cha Urais, imepiga marufuku jimbo lolote kumzuia.

Kwa sasa wananchi wengi wanatamani Trump Arudi kwa jinsi uongozi wa Biden ulivyoiharibu nchi, Vitu vimepanda sana bei, Raia wa nchi nyingine wanaingia Marekani bila vibali huku serikali ikiwajali kuzidi wamarekani wanaoishi mitaani, Biden ana matatizo ya memory, n.k
 
wabunge na vyombo vya sheria vya majimbo yaliyoshikiliwa na chama cha Democrats anachotokea Rais Biden yamekuwa yakifanya michezo michafu kukwamisha jitihada za Trump kugombea uraisi 2024...

Mkuu Mbona umeandika kama chawa wa CCM? Au wewe unatumia id ya Lucas mwashambwa?

Kwa akili kama hii sidhani kama Unaishi huko unyamwezini. Kule chawa ni marufuku…
 
Back
Top Bottom