JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

wanagoma. si walikuwa wanawazomea wa chadema. utoto huo wanaona aibu maana walishindwa kujadili mswada wakawa wanaimba taarabu ya mipasho. shame on ... walimlead vibaya jk kashtuliwa na watu makini aibu imewajaa. poleni waungwana
 
You missed my point pale niliposema kwamba nime zero down katika sakata hili tu kuanzia pale Chadema walivyopata baraka za JK ikulu kwamba muswada ule ubadilike, mpaka kufikia hali hii ya leo. Otherwise sikatai kwamba Ofisi ya Rais ina mapungufu, yapo mengi tu. Kuhusu wabunge, hoja yangu ya msingi ni kwamba wana kigeu geu, hawana msimamo unaoeleweka hasa kuhusu maslahi ya taifa hili. Na hilo ndio linapelekea wengio tuhoji, why this time around? Kwani matatizo nchi hii yameanza end of January 2012?? Walikuwa wapi muda wote, only to rush to the dance floor pale mziki wa posho ulivyowashwa na pia pale ile zomea zomea yao kwa chadema ilivyogeuzwa na rais.

Na kuhusu hiyo quote hapo juu kuhusu Mh. Beatrice, my point was - kuna wabunge wapo tayari kumuondoa Kikwete hata sasa kwa njia za ovyo ovyo tu. Kumuondoa Rais wa nchi madarakani sio suala dogo, nchi itatikisika hasa, hapo ndio watu watajua nini nguvu na umuhimu wa Rais. Kama wana nia ya kumwondoa Kikwete kwa justifications wanazojua wenyewe, wapeleke hizo efforts kwenye kofia yake ya Chama kwani yeye ni kiongozi wa CCM lakini ni Rais wa CCM, Chadema, NCCR, CUF, CCK, Jahazi Asilia, hata watanzania wasio kuwa na vyama, na hata watanzania ambao hawana umri wa kupiga kura bado.

Kwa mtazamo wako, kwanini nchi inayumba na solution yake ni nini?

Kwanini nchi inayumba? -- "In my view, source of problem remains entirely in himself JK for lacking leadership qualities and missing demanded intelligence necessary for his duty." By Radhia Sweety.
Solution yake ni nini? - Kumuondoa madarakani kwa njia zilizo halali kwa ajili ya maslahi ya nchi. Hatuwezi kuendelea hivi mpaka 2015 huku watu wakipewa sumu kutaka kuuawa, ufisadi uliokomaa, impunity yaani rule of law haipo. Sasa hatuwezi kujenga/kuendelea kama utawala bora haupo nasi kukaa pembeni kuacha kufanya maamuzi magumu kisa nchi itayumba. Nchi zote zinazoheshimu sheria ujue miaka ya nyuma walishawekana sawa kati ya watawala na watawaliwa. Mifano ni mingi: France, Russia, China na latest ni Egypt. Yaani Tz inavyoenda ni kama ndege iliyopo kwenye autopilot huku navigation instruments hazifanyi kazi. Tunahitaji extra effort and skills za rubani to navigate through safely unfortunately wewe na mie tunakubaliana kuwa Pilot mwenyewe hana ujuzi na ufundi huo. Je,utapendelea kuiacha hewani mpaka iishe mafuta ianguke au utatafuta namna ya kuishusha?
 
Wakulaumiwa ni hao walosema jk kasaini wakati ajasaini .walitaka rais akubari utumbo kweli sisiemu inawenye na wenyewe ni wabunge
 
Avatar yako inanikumbusha Tin tin na mbwa wake.
Nina collection ya nguvu.... pia ninazo za Asterik na Obelix.
Kama ni mshabiki, naishi jirani na comic bookstore, I can hook u up.
 
RAIS Jakaya Kikwete amefanikiwa kuzima uasi uliotaka kufanywa na wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), waliopanga kukwamisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Katiba ya mwaka 2011.
Baada ya kushindwa kukutana wabunge wote wa chama hicho, Kamati ya Uongozi ya Bunge imeteua wawakilishi watano kutoka miongoni mwa wabunge wake ambao wameunda kamati maalumu ya kukutana na Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM.
Kilichoibua mawazo ya uasi miongoni mwa wabunge wa CCM kinatokana na hatua ya serikali kuamua kuwasilisha mabadiliko katika sheria hiyo siku chache baada ya Rais Kikwete kukutana kwa nyakati tofauti na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na wadau mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Kikwete aliwasili Dodoma jana akitokea mkoani Mwanza alikokwenda kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM, kisha akaanza kukutana na wawakilishi watano wa wabunge wa chama hicho.
Awali, Rais Kikwete alipanga kukutana na wabunge wote wa CCM, alilazimika kukutana na wawakilishi watano wa chama hicho kutokana na msimamo wa wabunge hao kukataa kuonana naye kwa madai kuwa hawana cha kujadiliana naye.
Mbali ya kukutana na wawakilishi wa wabunge hao mjini Dodoma, Rais Kikwete alibadili upepo wa kisiasa katika viunga vya Bunge kwa hotuba yake aliyoitoa juzi mjini Mwanza kwamba katika marekebisho hayo, CCM nayo ilileta mapendekezo ya marekebisho manane ya sheria hiyo.
Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa wakati kuna wabunge bado wameshikilia msimamo wa kuukwamisha muswada huo, lakini pia wapo wanaokubaliana na Rais Kikwete.
Habari ambazo gazeti hili imezipata kutoka ndani ya kikao hicho cha rais na wabunge hao zilisema kuwa rais alifafanua kwa kina sababu ya kukubadili marekebisho aliyopokea kutoka kwa ujumbe wa CHADEMA na ule wa vyama vingine kutokana na uzito wa jambo lenyewe.
Habari zinasema kuwa Rais Kikwete mbali ya kuwalainisha wabunge kuhusiana na muswada huo, pia aliweka wazi msimamo wake wa kuwataka wawakilishi hao wa wananchi kuachana na suala la posho kwa sasa kwani linawajengea taswira mbaya.
Ujumbe huo wa wabunge, ulitarajiwa kukutana na wabunge wote jana baada ya kikao chake na rais ili kuwajulisha yaliyojiri katika mazungumzo yao na kama kuna haja ya kukutana nao wote kwa pamoja kabla ya muswada huo kuwasilishwa bungeni.
Awali muswada huo wa marekebisho ya sheria ya Katiba ya mwaka 2011, ulitarajiwa kuwasilishwa bungeni jana, lakini haukuwamo katika orodha ya shughuli za Bunge jana.
Akizungumza wakati wa kuahirisha kikao cha Bunge jana, Naibu Spika, Job Ndugai, aliwataka wabunge wa CCM kuwasha simu zao muda wote kwani Mwenyekiti wao, Jenister Mhagama (Peramiho), angewapigia simu wakati wowote kwa ajili ya kikao.
Wiki iliyopita, upepo wa kisiasa kwa wabunge wa CCM ulibadilika na kusababisha kutoa kauli nzito ndani ya vikao vya ndani, wakimlaumu Rais Kikwete kwa kile walichokiita kuwageuka.
Mambo ambayo yamewakera wabunge wa CCM katika siku za hivi karibuni ni pamoja na hatua ya Rais Kikwete kukana kubariki posho mpya za wabunge wakati Waziri Mkuu Pinda na Spika Makinda, tayari walishautangazia umma kwamba rais amebariki posho hizo.
Jingine ni la marekebisho ya sheria ya Katiba ya mwaka 2011, iliyofanyiwa marekebisho baada ya Rais Kikwete kukutana na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Wakati serikali iko mbioni kuwasilisha bungeni marekebisho ya sheria ya Katiba ya mwaka 2011, kama ambavyo Rais Kikwete amekubaliana na viongozi wa CHADEMA, wabunge wa CCM, walipitisha azimo la kukataa marekebisho hayo

SOURCE:TANZANIA DAIMA

Mm sijaelewa mantiki ya kchwa cha habari na habari yenyewe.
 
Hahahahaahaahah JF siku hizi unaweza post chochote kutoka chanzo chochote! Home of Great thinker
Mchungaji umeuza ID yako? Unataka invisible a post uamini! Get tym to think then muda utaongea! Tunavunja moyo informer wetu.taarifa hii hapo juu ni ngumu kuikanusha au kuikubali kwa haraka mkuu.
 
Ukiwa rais na ukafikia hali kama hiii ya JK inanidi uwe makini sana aidha ufanye maamuzi magumu au uukabidhi urais wako kwa kigroup cha watu ambao watakuwa wanakudrive.
 
awali JK alishauriwa aundee baraza dogo la mawaziri yeye kende kinyume kabisaaa amekuwa na baraza kubwa mno haya ndiyo madhara yake badala ya kufanya kaazi tulizo tarajia wao wanaendesha ajungu

sasa reshuffle ifanyike ili tuwe na baraza dogo sana la watu wenye kujituma sana. Wao wanadhani JK ndiye anayekosea kumbe ni wao hawatendi sawa na majukumu yao

ikilazimu ni bora tuingie kwenye uchaguzi mpya tu kieleweke kuwa awali tulikosea na sasa tunapaswa kurekebisha .......'' AMENI''
 
Mkuu,

Nimsafishe JK humu Jamiiforums kwa sababu gani, kwani ananilipia nauli ya daladala? Sina maslahi yoyote na JK zaidi ya yeye kuwa Rais wangu na Mwenyekiti wa Chama Changu, kama vile atakavyokuwa yeyote yule mwingine uchaguzi ujao 2015. Nachokieleza ni fikra zangu huru zinazotokana na kuchanganua pande zote mbili, na sio zaidi ya hapo. Unless wewe unalitazama suala hili kwa mapana, kwani kama unaenda nje ya mpaka wa sasa, upo sahihi - both bunge na Ofisi ya Rais wana mapungufu yao, mengi tu. Laini mimi nime zero down kwenye hili la:

sakata ya chadema kwenda ikulu;
JK kukubali hoja za Chadema kurekebisha muswada wa mchakato wa katiba;
JK kupinga ongezeko posho za wabunge;
Wabunge wa CCM kupinga miswaada miwili ya serikali bungeni;
Wabunge wa CCM kutishia kupiga kura ya kutokuwa na imani na JK
Na kuhusu taarifa kwamba JK kuwaambia wakitaka wapige hiyo kura.

Katika mlolongo huu, mtazamo wangu ni kwamba JK yupo correct, lakini vilevile nadhani huo pia ni mtazamo wa wananchi walio wengi.
Hehehehehe! Kizunguzungu! Sikuwahi ota kuna magamba mwenye upeo kama wako! Hehehe! Mchambuzi ni gambas!!
 
Mkuu,
hakuna mbunge aliye tayari kurudi jimboni kuanza kampeni upya dhidi ya Chadema, CUF, CCK, NCCR, kwa tiketi ya CCM ambayo imelemewa kwa hoja katika kila kitu cha msingi ndani ya nchi hii. Ikitokea uchaguzi mpya, sana sana wengi watagombea kupitia vyama vya upinzani. Vinginevyo, wabunge wengi sana kwa sasa wapo katika harakati za kulipa madeni yao kutokana na mikopo ya kampeni za 2010, ndio maana wanapigania sana posho. Kwa wastani, mbunge ambae hana kipato cha pembeni, huwa anabakia na shillingi zisizozidi laki mbili kwenye account baada ya makato ya madeni haya, pamoja na makato ya madeni ya magari yao (mashangingi), kwahiyo wana survive kwa posho na ndio maana wanakuwa wakali kama mbogo juu ya hilo.

Rais akiweka msimamo na kuwaambia wakitaka wapige kura ya kutokuwa na imani na Rais, wengi watasononeka chini kwa chini lakini hawata piga kura ya namna hiyo kutokana na sababu hizi. Lakini tujiandae kwa wao kufanya utawala wa Kikwete kuwa mgumu sana kuelekea 2015, hasa kuikwamisha serikali kwa makusudi katika mambo mbalimbali, bila ya wao kujua kwamba kufanya hivyo ndio kukimaliza CCM na kuvijenga Chadema, CCK, NCCR....

Huwa nakubali sana hoja zako kwa jinsi unavyochambua mambo kwa kina na siyo kishabiki.
 
ili kulinda heshima hata jk anapaswa kukaa pembeni........mtu mbishi sana huyu!!!!
 
Lakini kama tunakumbuka, kuna taarifa zilivuja kwamba katika mkutano wake wa kwanza na Chadema, Rais aliwaeleza kwamba analifahamu fika suala wanalolizungumza Chadema lakini akifanya tofauti na maamuzi ya wabunge wa CCM, wabunge wa CCM pamoja na CCM kwa ujumla hawatamwelewa. Kwahiyo sio kweli kwamba Rais hakuwa makini kujua kilichojiri ndani ya muswada. Nadhani ni sahihi zaidi kusema kwamba, awali Rais alitawaliwa na uwoga juu ya kukubaliana na hoja za Chadema, jambo ambalo katika kikao chake na Chadema cha mara ya pili, ameamua liwalo liwe.
Mcdm utawajua kwa dhana zao finyu.
 
adui yetu kama nchi ni kikwete........
 
Mchambuzi. Nakubaliana na msimamo wako. Kama kweli hicho kikao kilikuepo,JK awaache hao akina Shelukindo wapige kura,tuone mjaja nani. Hatuwezi endekeza ujinga na upumbavu eti kwa kuogopa kura ya kutokua na imani na Rais.

Mkuu unamsemea nani hapa!!! Naomba niwe nje ya hao unaowasemea!!!!

Tiba
 
Wapinzani wa kweli watatoka ndani ya CCM,nafikiri muda ni huu.
 
Back
Top Bottom