JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

Pro lowassa have really risen to this thread
 
Amfukuze Selina Kombani na Judge(?) Werema mimi hawa wawili ktk baraza la mawaziri la JK wani bore stiff
 
Wana jamvi
Hapa Dodoma kimenuka. JK kafika kutoka MWZ ili kuonana na wabunge. Wabunge wa CCM wakaitwa na kuingizwa ukumbini ili kumsubiri. Awali Katibu wao Jenester Mhagama alitoa tangazo kupitia Naibu Spika kuwa wabunge wote waache simu zao wazi ili kuitwa wakihitajika.
JK aliendelea kupata briefings na kuambiwa hali ni mbaya. Akashauriwa afanye reshuffle upesi ili kupoza moto. Kama kawaida akawa mbishi, lakini pia akasita kuingia ukumbini kuonana na wabunge. Mwishowe wabunge wameambiwa waende kulala kwa sababu JK bado ana kikao na watendaji.
Kuna hatari kesho ya reshufle. Mawaziri wote matumbo moto hususan Afya, Nishati, Fedha na Ujenzi. Vijana wa TISS wamemweleza kuwa baraza zima ni kama haliko kazini isipokuwa wizara moja tu- Ya Pombe Magufuli.
Vijana wa TISS wameingia kazini kwa kasi sana usiku huu kujaribu kubadili upepo miongoni mwa wabunge.

Chanzo: Mimi mwenyewe nikiwa Dodoma mjengoni.

Habari hii ingekuwa inawahusu CDM ungesikia vilio vya watu humu, ila kwa vile ni CCM wote kimya japokuwa ni habari ya uzushi. JF kwa nn tunakuwa na double standards, je watu wakisema huu mtandao ni wa CDM tutakataa? . JF imepoteza mwelekeo kabisa siku hizi .

 
Hayo marekebisho yatasomwa na kupitishwa bila shida. Utawasikia wabunge wa CCM wakiongozwa na Mama Kilango wakisema CCM kwa kuwa ni chama cha wananchi imesikia malalamiko yao na hivyo kuamua kuleta mabadiriko husika.
 
wabunge wa CCM, sijui wapo mjengoni kwa maslahi ya nani? Badala ya kusimamia mambo ya msingi wao wameng'angana na posho, hivi watakua na ujasiri tena wa kurudi majimboni kuomba kura kwa wapiga kura wao???
 
nipo nanoa mikuki na panga hapa. Nasubir watz waamke tukamtoe vasco dagama.
 
Kaka wanakosa msimamo kiivi hawawezi kutetea maslahi ya waTz
 
kuwa mbunge wa CCM unafungwa speed gavana, hupewi nafasi ya kupumua, mimi nisingeweza wakuu. bora nikalime matikiti rufiji ijulikane moja.
 
hao wabunge wa ccm ni wanafiki (ukimtoa january makamba) wangeni waliobaki hawana uwezo wa kupingana na serikali.

Nina wasiwasi na uhusiano wako na January , yawezekana anakufanyia kitu mbaya, huishi kumsifia humu ndani. Ukiisha ona mwanaume anamsifia mwanaume mwenzake ujue kuna walakini hapo

 
kuwa mbunge wa CCM unafungwa speed gavana, hupewi nafasi ya kupumua mimi nisingeweza wakuu. bora nikalime matikiti rufiji ijulikane moja.

Mbona Shibudi CDM wanamfunga gavana pia ?

 
wabunge wa CCM, sijui wapo mjengoni kwa maslahi ya nani? Badala ya kusimamia mambo ya msingi wao wameng'angana na posho, hivi watakua na ujasiri tena wa kurudi majimboni kuomba kura kwa wapiga kura wao???

Fedha Fedheha !

 
Mimi nadhani hii ni nafasi pengine ya mwisho kwa JK kurudisha hadhi yake na ya CCM mbele ya umma. Anahitaji kufanya mabadiliko makubwa na kuondoa mawaziri legelege wote; pia mwanasheria mkuu wa sasa hatoshi, huyu hafai katika mchakato wa kupata katiba mpya. Pia ni muhimu kwa rais kubadili mfumo wa serikali, hasa sekta ya elimu na afya. Pia apunguze ukubwa wa baraza la mawaziri kwa kufuta wizara nyingine au kuziunganisha ili iwe ishara kwa umma ya kuanza kubana matumizi tunapoelekea bajeti mpya mwezi juni. Na katika hotuba yake kuunda baraza jipya, awe mkali na awe tofauti kabisa, na ashike uzi huo huo kwa kipindi chake kilichobakia. Akiachia nafasi hii imponyoke, atakuwa na shughuli nzito sana ya kukipa CCM uhalali mbele ya umma, na pia mawaziri wengi wataendelea kumchukulia kama mshijaki. Hili litakuwa janga kubwa kwake hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa CCM, Novemba mwaka huu.

Mkuu hadhi yake na CCM kivip, huhitaji kuwa na upeo mkubwa sana kuelewa kuwa JK mwenyewe ndo chanzo cha uozo wote uliopo chamani na hata serikalini kwa kufumbia macho kila aina ya madudu yanayoendelea, sasa hiyo hadhi uanayoizungumzia ni ipi? Mkuu haya ni matokeo ya serikali ya kishkaji so mwache avaune alichopanda na wala sio swala la kurudisha hadhi.
 
Kwa hili la kupingana na marekebisho ya sheria ya katiba kwa sababu ya posho nadhani MASABURI alikuwa sahihi kuhusu viungo wanavyotumia baadhi ya wabunge kufikiri. Inaonekana kuna tatizo kubwa la wabunge wengi kutotumia bongo zao kwa ajili ya kufikiri na kutafakari mambo.

Kuhusu kura ya imani naapa hakuna mbunge wa CCM mwenye ubavu wa kutoa wazo la kupiga hiyo kura achilia mbali kuipiga kura yenyewe. Kwa mfumo wetu wa kikatiba wabunge ni wawakilishi wa chama na siyo wa wananchi kama wanavyotaka kutuaminisha. Wakipiga kutokuwa na imani na Rais maana yake ni kuwa hawana imani na Mwenyekiti wa chama chao ambacho ndio kimewaweka bungeni.
 
Reshuffle kirahisi ivyo jamani!
Wasije wakamuua JK kwa pressure!
 
Bunge linaendelea. Anna Makinda ndani. Sisi tuendelee na huu "uvumi" tu.
 
ili kulinda heshima hata jk anapaswa kukaa pembeni........mtu mbishi sana huyu!!!!

Hakuna haja ya JK kukaa pembeni kwa hili suala ya marekebisho ya katiba. Badala yake anatakiwa ashikilie uzi uleule ili tupate katiba ambayo itawawajibisha hawa wachumia tumbo wanaojiita wawakilishi wa wananchi. JK anatekeleza kwa vitendo falsafa yake kwa wafanyakazi kuwa siyo kila kitu lazima ukubaliane na mawazo ya watu wengine kuna wakati inabidi uchukue za mbayu wayu (i.e. wabunge wa CCM) uchanganye na za kwako.
 
Back
Top Bottom