Jk azidi kuandika historia

Kumchagua kiongozi mwanzilishi wa chama cha CCJ na kumpa ulaji wa nguvu ndani ya chama cha CCM.

Na kijana kweli anaonekana anafaa sana kwenye mambo ya Propaganda......

attachment.php
 
Acha uongo wewe, usieleze historia usiyoijua. Tangu suala la EPA lilipokaa mezan, vyombo husika vililishughulikia ki upelelezi na kupata ushahidi wa kujitosheleza kufungua mashtaka. Slaa wala yeyote kutoka sehemu yoyote hana uwezo wa kushinikiza chombo cha sheria kifanye kazi kwa matakwa yao.. UDHAIFU wa hoja. JARIBUN KUPONGEZA KINACHOWAPENDEZA HATA KAMA KINATOKA KWA ADUI YAKO KWA MASLAH YA TAIFA LETU.. Tuache UNAFKI!
 
Pamoja na sifa zote unazomwagia JK maisha ya Watanzania yamezidi kudorora kil kukicha.

Mimi mwenyewe siku hizi nakula mara mbili kwa siku wakati enzi za Mkapa nilikuwa nakula mara 3, 4 hadi 5. Mambo yote hayo aliyoyafanya yametokana na msukumo wa upepo wa kisiasa kwa wakati husika. Mfano kuvunja baraza la mawaziri ni matokeo ya ufisadi wa mawaziri wake amabapo alishindwa kuwalinda vingivyo angeng'oka yeye, kuwafikisha Mramba na Yona mahakamani ni usanii wa kuombea kura za uchaguzi wa 2010.

Kuhusu kuwapeleka wezi wa pesa za EPA mahakamani ikumbukwa kwamba haikuwa matokeo ya hiari yake. Hii ilitokana na msukumo wa wafadhili wa serikali yake ambao walimuwekea ngumu hadi awafikishe mahakamani wezi wa fedha zao. Hata hivyo bado tunawataka vigogo wenyewe wa EPA hasa wa Kagoda Agriculture Limited pamoja na Founders wake (Rostam Azizi, nk).

Pia kuhusu kuruhusu vibali vya maandamano ya wafusi wa upinzani inapaswa ijulikana kwamba si kazi ya Rais wala taasisi yoyote kuruhusu maandamano. Kinachopaswa kufanywa na waandamanaji ni kutoa taarifa kwa polisi juu ya nia yao ya kuandamana lini na muda upi na sio kuomba kibali. Baada ya kutoa taarifa Polisi kazi yao ni kuja kwenye maandamano ili kutoa ulinzi kwa waandamanaji.

TUENDELEE KUJADILIANA
 
7.Kwa kuzunguka dunia kwa kusafiri ameivunja mpaka rekodi ya Vasco da Gama
 
Ndugu yangu Lilombe

Thread yako ni ya maana sana, na huu ndiyo ukweli juu ya Rais J.K. Kuna vitu vingi vizuri sana kavifanya J.K na watanzania tutamkumbuka baada ya 2015! Of course, mabaya yapo ila kumbuka J.K si malaika.

Lakini kwa bahati mbaya hapa JF, inaonyesha hoja yoyote inayomsema vizuri Mh. Rais na serikali yake, kuna namna mbili hoja hiyo inapata mashambulizi:

1. Ubahatike wasiimuvizishe

2. Utegemee matusi na maneno mazito dhidi yako.

Kama unataka hoja yako ipate michango chanya na mingi, sema lolote baya juu ya Serikali yetu na huku ukiwasifia sana CDM. Wambie 2015 watakuwa Magogoni, then utaona furaha ya wana-JF.

Huu ni mtazamo tu, si lazima uwe ukweli wenyewe.

Jk has proven failure.
 
Rais Jakaya Kikwete amezidi kuandika historia katika kipindi chake cha uongozi kwa kuhitimisha kesi ya EPA ambayo kada wa CCM, Rajabu Maranda na \mshirika wake, Farijala wamepewa hukumu ya miaka 21 ambapo watatumikia jela miaka 5. Pia wakitoka jela itatakiwa walipe fedha walizoiba kupitia akaunti ya EPA.

Wananchi wa Tanzania pasipo kujali itikadi inatubidi kupongeza Rais wetu ili tumpe moyo ili aweze kuwashughulikia mafisadi na maovu mengine yanayofanyika nchini mwetu.

Tujikumbushe baadhi ya hatua ambazo JK amethubutu kuchukua katika uongozi wake:-
1. Kuvunja Baraza la Mawaziri ikiwa ni kujiuzulu kwa Waziri Mkuu
2. Kuwafikisha mahakamani viongozi wandamizi wa serikali; Mramba, Yona na Mgonja
3. Kuwapeleka watuhumiwa wa EPA mahakamani
4. Kuwa na moyo wa uvumilivu kwa vyombo vya habari
5. Kutoa vibali vya maandamano kwa vyama vya siasa pasiipo mkomo

NAWAKILISHA


Naamini wewe unamatatizo, nafikiri wewe pia hujui unaongea nini.
Umetumwa ndugu yangu, aliyekutuma ni mjinga anafikiri watanzania leo ni walewale wa miaka ile.
Usiendekeze njaa kula vya bure, fanya kazi, waache CCM wajitetee wenyewe na magamba yao.
 
Kama CDM wanavyojishughulisha na shughuli za mahakama kule NYAMONGO...USHABIKI usio na Maana. We si ulikuwa unapiga kelele kwamba hawashughulikii watuhumiwa wa EPA. Ulitaka yeye ndo awashughulikie au mahakama ndo iwashughulikie?? Usiwe mfinyu wa mawazo.
Kwa watuhumiwa wa EPA ni hao wawili tuuuuuu....??? Vipi wale wanaodaiwa kuwa walizirudisha kimya kimya............??? KWA NINI HAO WA LIMYA KIMYA HAWAJULIKANI LAKINI TUNAAMBIWA WAMERUDISHA.................... acha kujifanya huna ufinyu nwa mawazo.
 
Kwa watuhumiwa wa EPA ni hao wawili tuuuuuu....??? Vipi wale wanaodaiwa kuwa walizirudisha kimya kimya............??? KWA NINI HAO WA LIMYA KIMYA HAWAJULIKANI LAKINI TUNAAMBIWA WAMERUDISHA.................... acha kujifanya huna ufinyu nwa mawazo.

May be mkuu kuna sheria mbili kuw aukirudisha mali uliyoiba unasamehewa ila ukikataa ndo unapeleka ndani na hii inafanya kazi kwa wakubwa tuu
 
Acha uongo wewe, usieleze historia usiyoijua. Tangu suala la EPA lilipokaa mezan, vyombo husika vililishughulikia ki upelelezi na kupata ushahidi wa kujitosheleza kufungua mashtaka. Slaa wala yeyote kutoka sehemu yoyote hana uwezo wa kushinikiza chombo cha sheria kifanye kazi kwa matakwa yao.. UDHAIFU wa hoja. JARIBUN KUPONGEZA KINACHOWAPENDEZA HATA KAMA KINATOKA KWA ADUI YAKO KWA MASLAH YA TAIFA LETU.. Tuache UNAFKI!
NA hapo mezani aliliweka na nani kama si CDM........................ SI MLIBISHA NA MWISHO MKAACHIA NA MKAOTA MAGAMBA NA SASA MNAHANGAIKA KUYAVUA.................................... Kuna siku utatumwa kukata hicho kichwa chako, na utakata kweli.................
 
NA hapo mezani aliliweka na nani kama si CDM........................ SI MLIBISHA NA MWISHO MKAACHIA NA MKAOTA MAGAMBA NA SASA MNAHANGAIKA KUYAVUA.................................... Kuna siku utatumwa kukata hicho kichwa chako, na utakata kweli.................

Hivi wanapongeza kipi hapa maana hakipo cha kupongeza wala hakuna aliyeonyesha amefanya kazi nzito baada ya haya mambo kuibuliwa wangekuwa wanapongezana kama wangekuwa ni wao waliyaanzisha na kuyapeleka mahakamani
 
Kwa watuhumiwa wa EPA ni hao wawili tuuuuuu....??? Vipi wale wanaodaiwa kuwa walizirudisha kimya kimya............??? KWA NINI HAO WA LIMYA KIMYA HAWAJULIKANI LAKINI TUNAAMBIWA WAMERUDISHA.................... acha kujifanya huna ufinyu nwa mawazo.

Maswali mengi kuliko majibu,wanafaidi mafisadi.
 
JK no at all
i reserve my comment on this stupid prezidaa isije ikawa

.. Jk ni mvumilivu mnoo.... sasa anagalia lugha zinazotumiwa na wana JF.. kama hiyo... ushalaanika wewe meryttina
 
Inabidi JK akubali la sivyo anaweza kukutwa na ya Gadafi. Gadafi alikuwa hafanyi hivyo kwa hiyo kumfagilia Jk kwa hilo ni umbumbu tu unawasumbua na si vinginevyo. Aache iliaone peoples power.
 
.. Jk ni mvumilivu mnoo.... sasa anagalia lugha zinazotumiwa na wana JF.. kama hiyo... ushalaanika wewe meryttina


Anyway Jk ni rais ambaye kweli sijategemea kufanya mambo kama hayo anayofanya maana aliingia madarakani kwa kishindo na anaondoka kwa kuanguka kwa kishindo... Watanzania ni waoga sana wa maendeleo wanaona wakibadili chama watakufa........ufinyu wa mawazo.


UKIOGOPA KUCHAMBA KWA KARATASI JARIBU WEMBE
 
unamsifu JK ambaye awali Dr.slaa alipotaja majina ya mafisadi na ufisadi wa EPA jk alipuuza? alidhani atafunika skendo ili kwa kupuuza? matokeo yake ilibainika wazi kuwa hata yeye (jk) ni fisadi kweli. EPA ndiyo iliyomweka madarakani 2005 na kuendelea hadi sasa. akijipeleka yeye mahakamani ndipo tutamsifu kwa ujasiri wake.
 
Hilo changa la macho tu! Dagaa wanatiwa ndani, wakati mapapa wanatanua na ma-hammer yao!!! Hao watatoka kwa msamaha wa Rais ktk sherehe za kitaifa nani anabisha? Kwa nn kesi ya akina Mramba/yona na hii ipi ilianza??? upo hapo???:pound:

KWELI KILIO CHA SAMAKI MACHOZI YENDA NA MAJI!!!!!:pound:
 
Mimi nitamkumbuka JK kwa yafuatayo:
-Ni Rais aliyeweka rekodi ya kuingia madarakani kwa pesa nyingi chafu.
-Ameisambaratisha CCM kwa makundi ambayo hayatasuluhishika.
-Zanzibar imekuwa NCHI.
-Ameishirikisha familia yake kikamilifu kwenye SIASA.
-Akianguka, akinyanyuka anasonga mbele.
-Ni bingwa wa semina elekezi kusikoelekea.
 
.. Jk ni mvumilivu mnoo.... sasa anagalia lugha zinazotumiwa na wana JF.. kama hiyo... ushalaanika wewe meryttina

Na kweli.......... ni mvumilivu mno................ maana amevumilia maovu yote yaliyotokea ndani ya nchi hiii likiwemo lile la list ya wale wanaoharibu bandari .............. na ndiyo maana hadio leo yanaendelea.............
 
Back
Top Bottom