Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,952
- 10,037
Rais Jakaya Kikwete amezidi kuandika historia katika kipindi chake cha uongozi kwa kuhitimisha kesi ya EPA ambayo kada wa CCM, Rajabu Maranda na \mshirika wake, Farijala wamepewa hukumu ya miaka 21 ambapo watatumikia jela miaka 5. Pia wakitoka jela itatakiwa walipe fedha walizoiba kupitia akaunti ya EPA.
Wananchi wa Tanzania pasipo kujali itikadi inatubidi kupongeza Rais wetu ili tumpe moyo ili aweze kuwashughulikia mafisadi na maovu mengine yanayofanyika nchini mwetu.
Tujikumbushe baadhi ya hatua ambazo JK amethubutu kuchukua katika uongozi wake:-
1. Kuvunja Baraza la Mawaziri ikiwa ni kujiuzulu kwa Waziri Mkuu
2. Kuwafikisha mahakamani viongozi wandamizi wa serikali; Mramba, Yona na Mgonja
3. Kuwapeleka watuhumiwa wa EPA mahakamani
4. Kuwa na moyo wa uvumilivu kwa vyombo vya habari
5. Kutoa vibali vya maandamano kwa vyama vya siasa pasiipo mkomo
NAWAKILISHA
Kwa kweli kwa hayo mekundu JK amefanya uthubutu. Kama si uthubutu angeweza kuzuia kuundwa kwa kamati ya Bunge iliyo mfanya EL ajiuzulu. Katika nchi kama zetu hizi kuruhusu Waziri Mkuu/Rafiki yako asulubiwe kiasi kile huku wewe ukiwa na uwezo wa kuzuia ni uthubutu mkubwa huo. Kama si uthubutu wa Rais si PCCB walikuwa wamemtakasa EL?