JK amteua Jaji Kiongozi mpya

Ndiyo maana naita kujiuma uma.

Hapa unapointi, habari niliyoipokea mimi kutoka kwenye hiyo source ndiyo ilisema hivyo. Chanzo hicho bila ya shaka na chenyewe hakikuwa na uhakika wa muda wa ujaji lakini details nyingine hazikuwa sahihi kabisa kama zinavyoonekana na kusahihishwa.

Mwanakijiji, mimi sijiumiumi wewe, soma maelezo yangu vizuri. Hivi huwa kila kitu unachokipokea unakichukua kama kilivyo. Huwezi hata kuulizia kando. Mimi suala linabaki palepale kuwa UMEPOTOSHA, sitaki tumia lile neno ambalo Mkuu SMU kaniambia kuwa sijui sio la kistaarabu, nimemuomba neno la mtu anayedanganya hajajibu.

Rais Kikwete amemteua Jaji Fakihi Jandu kutoka Mahakama Kuu Iringa kuwa Jaji Kiongozi mpya kuchukua nafasi ya Jaji Salum Massati ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa.

Jaji Jandu alikuwa Wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita hadi alipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na sasa kuwa Jaji kiongozi..

Hapa ndio kwenye tatizo, mtu makini huwezi ambiwa tu jambo na kulichukua bila hata kudodosa. Ungekuwa makini hata huyo jamaa aliyekupa hizi habari ungemuliza inakuwaje ateuliwe kuwa JK wakati ana muda mfupi kama wa mwaka mmoja tangu awe Jaji?. Majibu ya huyo jamaa yangekufanya nawe pamoja na yeye kutafakari, baada ya kutafakari mngeamua kutafuta habari zaidi. Lakini inaonekana ukipata tu habari unataka ujiweke wewe ndio "SOURCE" ya hiyo habari. Habari ni vizuri kuweka "source" yake, mfano unasema imetoka Majira, Michuzi nk. Sasa uliripoti kama wewe ni msemaji wa Ikulu (Rweyemamu) ama Katibu Mkuu Kiongozi (Luhanjo). Huo sio uwandishi. Ama umekuwa Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo?.

Kinachokuponza ni kutaka kila kitu uonekane wewe ndio wa mwanzo, habari haziendi hivyo, ungekuwa uko Ikulu ningesema sawa. Kwa habari yako ungesema kutokana na jamaa aliyenifahamisha masaa machache yaliyopita, Kikwete kateua JK, na huyo JK mpya alikuwa Wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita hadi alipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na sasa kuwa Jaji kiongozi. Hapa tungejua hii habari umeisikia ama umeipata kwa mtu.

Tatizo lingine hupendi kuambiwa ukweli, na waliokuzunguka wanakusifia tu hawakwambii ukweli (hadithi ya Mfalme aliye uchi, na wapambe wanamshangilia kapendeza). Sasa mimi siko hivyo, siwezi sifia kitu kina makosa.
 
Mimi nisiyeamini? Huyo unaemtetea unajua alichosema mwishoni lakini au unatishwa tu na profile?

Kusema kitu hakikuwa sahihi, siyo sawa na kusema uongo!

Waungwana, wengi mmeonyesha maturity and humility kwa kusema kwamba mtu akikosea haina maana ni mwongo

Hii haiitaji uungwana kuona inahitaji commons sense

sawa kabisa, lakini wakuu, sikieni: Ndugu yetu Mwanakijiji anasema kwamba, akisema "kama mwaka mmoja" hiyo ni disclaimer inayotosha kujuimisha miaka mitano!

Inashangaza! "anasema kwamba, akisema "kama mwaka mmoja" hiyo ni disclaimr inayotosha kujumuisha miaka mitano". Sasa mimi nimesema wapi hayo unayosema nimesema. Soma nilichoandika hutapata shida hii ya kusoma kisichoandikwa.



You get that? Kwa lugha ya hisabati, arithmetics, huu ni uwiano wa moja kwa tano. Kwamba siku ikitokea Fulani bin Fulani ana uzoefu wa kazi wa miaka 10, tuseme, Mwanakijiji anaweza kutuletea taarifa akisema "Fulan bin Fulani amekuwa kiongozi kama miaka miwili" halafu baadae ukweli ukijulikana ataanza kuhalalisha hilo potofu kwa kigezo kwamba aliweka neno "kama." Moja kwa tano ni sawa na mbili kwa kumi, na moja inawiana na tano! Na, neno "kama" ukishaliweka basi uko huru kusema chochote kile!

Unaongeza maneno mengi na kwenda mbali kweli. At the end utajikuta ni peke yako umefika huko halafu unashangaa "where is everbody else?"

Waungwana, huyo mtu anaefikiri hivyo hawezi kuonekana kama anafanya makusudi?


hawa waungwana itabidi wajitokeze kukusaidia kwa kweli. Jamani "waungwana" Kuhani anahitaji msaada hapa, call a friend or something.
 
MawazoMatatu, baija bolobi,..naamini Tanganyika Law Society waliandaa orodha hiyo mara baada ya uteuzi wa Augustino Ramadhani kuwa Chief Justice.

..baada ya uteuzi huo Raisi aliwapandisha ngazi kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufaa Jaji Chande, Jaji Masati, na mwingine simkumbuki.

..nadhani kwa sasa hivi idadi ya Majaji wa Mahakama ya Rufaa imetimia.

NB:..tangu orodha hiyo itoke, Jaji Masati amepandishwa kuwa Jaji Kiongozi, na baadaye Jaji wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania.

Kukusahihisha kidogo Mkuu JokaKuu, Rais aliwateua Jaji Steven James Bwana, Jaji Bernard Michael Luanda, Jaji Mohammed Chande Othman na Jaji Sauda Mjasiri mwezi wa pili 2008 kutoka Mahakama Kuu kuwa majaji wa Mahakama ya Rufaa.
 
Sasa kuhani kama anataka tuendelee kujadili ubishi wake, alete tarehe Jaji Jundu alipoteuliwa kuwa Jaji. Kwa sababu hili nalo limepitapita tu baada ya mtu mmoja kutaja jina Mkapa. Na huyo Kuhani ingebidi atuletee hapa tuone kwa sababu anavyobishi utadhani ni Rweyemamu wa Ikulu.
 
Mwanakijiji, mimi sijiumiumi wewe, soma maelezo yangu vizuri. Hivi huwa kila kitu unachokipokea unakichukua kama kilivyo. Huwezi hata kuulizia kando.

Of course not! Na ndiyo maana watu wenye taarifa zaidi wanakuja na kusahihisha au kuweka sawa. Hiyo ndiyo jadi ya JF. Hakuna mtu anayedai kuwa sahihi 100% kwa kila kitu. Hata hivyo hilo si sawa na mtu kudanganya au kusema uongo.

Mimi suala linabaki palepale kuwa UMEPOTOSHA, sitaki tumia lile neno ambalo Mkuu SMU kaniambia kuwa sijui sio la kistaarabu, nimemuomba neno la mtu anayedanganya hajajibu.

Kupotosha ni kule kule kusema uongo, hapa unamaana nilikuwa na lengo la kuudanganya umma nilipotoa taarifa ile. Kwamba, Jundu hakuteuliwa kuwa Jaji kiongozi, kuwa hakutokea Iringa, kluwa hakuwa wakili wa kujitegemea na kuwa hakuwa na muda mfupi. Yote haya ni upotoshaji kwenye mawazo yako.


Hapa ndio kwenye tatizo, mtu makini huwezi ambiwa tu jambo na kulichukua bila hata kudodosa. Ungekuwa makini hata huyo jamaa aliyekupa hizi habari ungemuliza inakuwaje ateuliwe kuwa JK wakati ana muda mfupi kama wa mwaka mmoja tangu awe Jaji?. Majibu ya huyo jamaa yangekufanya nawe pamoja na yeye kutafakari, baada ya kutafakari mngeamua kutafuta habari zaidi. Lakini inaonekana ukipata tu habari unataka ujiweke wewe ndio "SOURCE" ya hiyo habari. Habari ni vizuri kuweka "source" yake, mfano unasema imetoka Majira, Michuzi nk. Sasa uliripoti kama wewe ni msemaji wa Ikulu (Rweyemamu) ama Katibu Mkuu Kiongozi (Luhanjo). Huo sio uwandishi. Ama umekuwa Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo?.

Wakati mwingine habari haziko kwenye sources kama hizo! Vinginevyo kila mtu angekuwa nazo kiurahisi hivyo.

Kinachokuponza ni kutaka kila kitu uonekane wewe ndio wa mwanzo, habari haziendi hivyo, ungekuwa uko Ikulu ningesema sawa. Kwa habari yako ungesema kutokana na jamaa aliyenifahamisha masaa machache yaliyopita, Kikwete kateua JK, na huyo JK mpya alikuwa Wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita hadi alipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na sasa kuwa Jaji kiongozi. Hapa tungejua hii habari umeisikia ama umeipata kwa mtu
.

Hahahaha.. so kinachokusumbua ndiyo hicho! Itakuwaje kama chanzo hicho kilikuwa karibu na hiyo Ikulu? of course siwezi kukiweka hapa na lawama zote nabeba mimi.

Tatizo lingine hupendi kuambiwa ukweli, na waliokuzunguka wanakusifia tu hawakwambii ukweli (hadithi ya Mfalme aliye uchi, na wapambe wanamshangilia kapendeza). Sasa mimi siko hivyo, siwezi sifia kitu kina makosa.

wrong, angalia rekodi yangu kuhusu watu kuniambia ukweli. Sina hofu ya mtu yeyote au sisumbuliwi na mtu yeyote kuniambia ukweli au kile anachoamini ni ukweli. Tatizo langu ni watu ambao wanajaribu kutafuta ujiko wa aina fulani kufanya mashambulizi yasiyo na msingi. Ninaelewa wito wangu ambao sishei na mtu mwingine na ni kwa sababu hiyo anayetaka kuchukua shots kwangu anakaribishwa.

Ukijisikia kukosoa kosoa tu, mimi siyo kiongozi wa CCM ninayetaka kuimbiwa nyimbo za sifa au kushangiliwa kwa sifa za uongo. As a matter of fact, sihitaji sifa yoyote, nafanya ninavyofanya jinsi ninavyofanya. Ukijisikia kero, kereka, ukijisikia chuki chukia, ukijisikia furaha furahia, ukijisikia kukosoa kosoa!

Ni sehemu ya mapambano yale yale. Na sina kinyongo au kisasi kwa mtu yeyote ni tofauti tu ya mitazamo ma mwelekeo.
 
Sasa kuhani kama anataka tuendelee kujadili ubishi wake, alete tarehe Jaji Jundu alipoteuliwa kuwa Jaji. Kwa sababu hili nalo limepitapita tu baada ya mtu mmoja kutaja jina Mkapa. Na huyo Kuhani ingebidi atuletee hapa tuone kwa sababu anavyobishi utadhani ni Rweyemamu wa Ikulu.

baija

.......you are very genuine on this.......hii ligi ya Mwanakijiji Vs Kuhani imetokea mbali............puuhh leeaase wee vuta popcorn zako angalia game........
 
Of course not! Na ndiyo maana watu wenye taarifa zaidi wanakuja na kusahihisha au kuweka sawa. Hiyo ndiyo jadi ya JF. Hakuna mtu anayedai kuwa sahihi 100% kwa kila kitu. Hata hivyo hilo si sawa na mtu kudanganya au kusema uongo..

JF, mimi ni member na sio wa zamani sana, nijuavyo kunaletwa hapa habari kutoka magazetini, press release za serikali, blogu (michuzi), tetesi, kusikia radioni (bbc, clouds nk).

Hahahaha.. so kinachokusumbua ndiyo hicho! Itakuwaje kama chanzo hicho kilikuwa karibu na hiyo Ikulu? of course siwezi kukiweka hapa na lawama zote nabeba mimi.

Kinachonisumbua sio kwamba nahitaji useme nani kakupa habari, kusema tu nimepata habari kutoka kwa jamaa yangu, rafiki (bila kumtaja jina), tunajua wazi umezisikia kutoka sehemu fulani, sasa ukiripoti bila kutaja Source ina maana basi wewe ni msemaji wa Ikulu ama Maelezo. Sema angalau hata nimetumiwa email, hakuna mtu JF atakuuliza ni nani?. Huo ndio uwandishi.

wrong, angalia rekodi yangu kuhusu watu kuniambia ukweli. Sina hofu ya mtu yeyote au sisumbuliwi na mtu yeyote kuniambia ukweli au kile anachoamini ni ukweli. Tatizo langu ni watu ambao wanajaribu kutafuta ujiko wa aina fulani kufanya mashambulizi yasiyo na msingi. Ninaelewa wito wangu ambao sishei na mtu mwingine na ni kwa sababu hiyo anayetaka kuchukua shots kwangu anakaribishwa..

Wewe ni nani watu watafute UJIKO, na baada ya ujiko inakuwaje. Unadhani hapa tuko Viwanja va Namfua, Singida ama Unga Limited, Arusha tunashusha sera watu watuone ili kupata ujiko. Ukiniona barabarani utajua huyu ndio Mfumwa ili nipate huo ujiko. Acha KUJISHEBEDUA kwamba mtu anapokwambia ukweli basi anatafuta ujiko, yaleyale niliyosema hadithi ya Mfalme aliyekaa utupu. Hapa JF, tunajadiliana tu, sidhani kuna mtu hapa anatafuta SIFA ama UJIKO kwa kujadiliana na mwingine.

Ukijisikia kukosoa kosoa tu, mimi siyo kiongozi wa CCM ninayetaka kuimbiwa nyimbo za sifa au kushangiliwa kwa sifa za uongo. As a matter of fact, sihitaji sifa yoyote, nafanya ninavyofanya jinsi ninavyofanya. Ukijisikia kero, kereka, ukijisikia chuki chukia, ukijisikia furaha furahia, ukijisikia kukosoa kosoa!

Ni sehemu ya mapambano yale yale. Na sina kinyongo au kisasi kwa mtu yeyote ni tofauti tu ya mitazamo ma mwelekeo.

Hivi wewe kuambiwa ukweli ni mapambano?, hii ni kuwekana sawa tu, ama kuelimishana. Kila mtu kuna alijualo na ambalo halijui, tukiwa pamoja ndio tunasawazisha.
 
JF, mimi ni member na sio wa zamani sana, nijuavyo kunaletwa hapa habari kutoka magazetini, press release za serikali, blogu (michuzi), tetesi, kusikia radioni (bbc, clouds nk).

that is where you are wrong, I don't depend on news from other websites au news sources!



Kinachonisumbua sio kwamba nahitaji useme nani kakupa habari, kusema tu nimepata habari kutoka kwa jamaa yangu, rafiki (bila kumtaja jina),

that is the whole point..nikisema jamaa, rafiki n.k nitaingia kwenye lawama nyingine kabisa.

tunajua wazi umezisikia kutoka sehemu fulani, sasa ukiripoti bila kutaja Source ina maana basi wewe ni msemaji wa Ikulu ama Maelezo.

Tafsiri ya maana inaweza kuwa yeyote ile.

Sema angalau hata nimetumiwa email, hakuna mtu JF atakuuliza ni nani?. Huo ndio uwandishi.

Bado unataka kujua chanzo.... you won't. Nikiwa ninataka kuweka chanzo huwa naweka chanzo. In this one I didn't, and I stand on that one.


Wewe ni nani watu watafute UJIKO, na baada ya ujiko inakuwaje. Unadhani hapa tuko Viwanja va Namfua, Singida ama Unga Limited, Arusha tunashusha sera watu watuone ili kupata ujiko.

mmh.. motives za watu ziko za aina nyingi sana, sitaki kuspeculate. Ninayafanya haya kwa muda mrefu na ninajua mashambulizi nikiyaona. Yako na ya Kuhani ni mashambulizi.

Ukiniona barabarani utajua huyu ndio Mfumwa ili nipate huo ujiko. Acha KUJISHEBEDUA kwamba mtu anapokwambia ukweli basi anatafuta ujiko, yaleyale niliyosema hadithi ya Mfalme aliyekaa utupu. Hapa JF, tunajadiliana tu, sidhani kuna mtu hapa anatafuta SIFA ama UJIKO kwa kujadiliana na mwingine.

Kuna kitu kinaitwa mijadala na kuna kitu kinaitwa mashambulizi ya kwako na ya Kuhani siyo mijadala ni mashambulizi, na mashambulizi yana lengo moja tu kuangamiza.. well, ni sehemu ya mapambano tu.



Hivi wewe kuambiwa ukweli ni mapambano?, hii ni kuwekana sawa tu, ama kuelimishana. Kila mtu kuna alijualo na ambalo halijui, tukiwa pamoja ndio tunasawazisha.

Hapana, hukufanya hivyo, watu wanaojaribu kumuweka mtu mwingine sawa, kumsahihisha au kujaribu kufafanua kitu hawafanyi ulichofanya wewe na anachofanya Kuhani. Mlichofanya ni kujaribu kurusha makombora yasiyo na moto.

Hivi kwanini sijambishia aliyeleta taarifa ya kuhusu muda wa Jaji Jundu? Umeona alivyoleta hoja yake kuiweka sawa, sasa kama ningetaka kubishana ningebishana na yeye.
 
Mwanakijiji,Kuhani,Mfumwa,Pundamilia,Philemon M,Mawazomatatu,Baija,Jobo,...

..hivi majukumu ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ni yapi?

..ngazi za Majaji ktk mahakama kuu ni zipi? kuna tofauti gani kati ya Jaji wa Mahakama Kuu mkoa X, na Jaji Mfawidhi mahakama kuu mkoa X?

..kuna walioleza kwamba the smaller "J number" a judge has, the higher ranking and senior he/she is.

..ni mamlaka ina jukumu la kutoa promotions kwa Majaji within the Mahakama Kuu?

..naomba kujua kama kuna uwezekano, say J10, anaweza kuruka ngazi na kuwa J7, huku J9 na J8 wakiwa hawajapanda ngazi.

..zaidi ya seniority kuna vigezo gani vingine vinatumika ktk kuwapandisha ngazi majaji within mahakama kuu, na hata kwenda mahakama ya rufaa? ninauliza hivi kwasababu kuna majaji ambao walikuwa junior kwa Jaji Fakihi Jundu wamepewa promotion za kwenda Mahakama ya Rufaa.
 
that is where you are wrong, I don't depend on news from other websites au news sources!.

Uungwana ni jambo zuri sana, ina maana ndugu yangu una waandishi dunia nzima. Ina maana zile "Breaking News" unazoziweka kule kwako zote unapata toka kwa waandishi waliozagaa dunia nzima?. Kuwa mkweli tafadhali!. Hayo mashirika makubwa tu kama BBC, CNN, DW nk nayo hupata habari toka "source" tofauti kuna wakati.

Bado unataka kujua chanzo.... you won't. Nikiwa ninataka kuweka chanzo huwa naweka chanzo. In this one I didn't, and I stand on that one.

Mkuu hapa anataka kubadili mada, ili tujadiliane kuhusu chanzo. Mimi nimesema hata kama hutaki kukitaja chanzo, ulipoweka habari mwanzoni unesema umeipata toka kwa mtu ambaye namuhifadhi. Usilete habari kama wewe ni msemaji wa Ikulu, Mahakama ya Kuu ama Maelezo. Usigeuze mada tafadhali, hatuzungumzii unipe chanzo, uwe unasema umepata wapi habari unapoitoa mara ya kwanza, tena habari tete (sijui ni eno sahihi, Mkuu SMU ataniambia kama sio sahihi nitaomba radhi).

mmh.. motives za watu ziko za aina nyingi sana, sitaki kuspeculate. Ninayafanya haya kwa muda mrefu na ninajua mashambulizi nikiyaona. Yako na ya Kuhani ni mashambulizi.

Kuna kitu kinaitwa mijadala na kuna kitu kinaitwa mashambulizi ya kwako na ya Kuhani siyo mijadala ni mashambulizi, na mashambulizi yana lengo moja tu kuangamiza.. well, ni sehemu ya mapambano tu. !.

Siwezi kumjibia Kuhani. Kwangu mimi na wengine hapa ni mijadala, soma "post" yangu ya kwanza kabisa katika hii "thread", ndio utajua kama nakushambulia ama mjadala. Usipende kuhisi, soma bila kuwa na mawazo HASI kichwani. Kama utaona kila Mfumwa analoandika kujadiliana nawe ni mapambano, basi utalichukulia ni mapambano tu. Lakini kama utasoma "with open mind", utakuta kuwa tunajadiliana tu na sikushambulii.

Hivi kwanini sijambishia aliyeleta taarifa ya kuhusu muda wa Jaji Jundu? Umeona alivyoleta hoja yake kuiweka sawa, sasa kama ningetaka kubishana ningebishana na yeye.

Kwani hapa tunabishana ama kueleweshana?.
 
Mwanakijiji,Kuhani,Mfumwa,Pundamilia,Philemon M,Mawazomatatu,Baija,Jobo,...

..hivi majukumu ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ni yapi?

..ngazi za Majaji ktk mahakama kuu ni zipi? kuna tofauti gani kati ya Jaji wa Mahakama Kuu mkoa X, na Jaji Mfawidhi mahakama kuu mkoa X?

..kuna walioleza kwamba the smaller "J number" a judge has, the higher ranking and senior he/she is.

..ni mamlaka ina jukumu la kutoa promotions kwa Majaji within the Mahakama Kuu?

..naomba kujua kama kuna uwezekano, say J10, anaweza kuruka ngazi na kuwa J7, huku J9 na J8 wakiwa hawajapanda ngazi.

..zaidi ya seniority kuna vigezo gani vingine vinatumika ktk kuwapandisha ngazi majaji within mahakama kuu, na hata kwenda mahakama ya rufaa? ninauliza hivi kwasababu kuna majaji ambao walikuwa junior kwa Jaji Fakihi Jundu wamepewa promotion za kwenda Mahakama ya Rufaa.

Basically mimi ninaungana na mchangiaji mmoja ambaye ameeleza kuwa kazi za Jaji kiongozi ni za kiutawala zaidi. Hata hivyo mjadala huu sioni kama una nguvu sana ya kuhoji uteuzi ambao karibuni wachangiaji wengi hawana facts zinazohusu teuzi za majaji zaidi ya kufikiria seniority. Seniority is not an absolute criteria, kitu cha msingi ni uwezo wa kiutendaji alionao mteuliwa. Si kila jaji anaweza kuwa Jaji Kiongozi hata kama amekuwa jaji kwa muda mrefu. Nadhani mjadala huu hauna tija zaidi ya kujadili hoja katika mtazamo finyu na hoja nyepesi.
 
Ogah, nimekuelewa.
Ubishi huu una undani wake. Kuna watu wanamfanya Mwana Kijiji kuwa punching bag lao au wanafanya mazoezi ya hoja (wako darasani). Nyumba yetu inaungua (TZ), kuhani na Mfumwa wanakazana kuua panya wanaokimbia moto!
 
MKJJ yapasa u grow kimawazo.!!!...kama muungwana, Mfumwa kakuweka sawa juu ya ethics za kuleta habari...!!! next time ukileta habari kuwa makini usikurupuke kama wanavyokurupuka wengine!!!!

Bahati mbaya ingine historia yako na Kuhani, unaona hata ktk mada hii ni mapambano. Umekuwa mtu wa lugha, lkn matumizi yako ya neno "kama" hayakustahili kabisa, otherwise ulikuwa na ajenda yako kichwani...!!!

Bahati mbaya ingine unajijengea tabia kama za mawaziri wa serikali yetu, wanapokosea au kuteleza hawataki kuonekana wamekosea, watataka kuweka lahaja zao nyingi kuonekana hawakukosea. otherwise mijadala kama hii haiwezi kwisha....na ndio maana hata lugha za kuwataka wajiuzulu na wao wanakuwa hawatuelewi...!!!!
 
..orodha ya Majaji wa Mahakama Kuu. hii siyo the most recent. it could be about two years old. source yangu ni Tanganyika Law Society.

..Majaji wa Mahakama ya Rufaa.

1 Mh. Jaji Mh. Jaji Augustino S.L. Ramadhani Jaji Mkuu

2 JR.1 Mh. Jaji Damian Z. Lubuva

5 JR.2 Mh. Jaji John A. Mroso

6 JR.3 Mh. Jaji Eusebia Nicholaus Munuo

7 JR.4 Mh. Jaji Harold Reginald Nsekela

8 JR.5 Mh. Jaji January Henry Msoffe

9 JR.6 Mh. Jaji Simon N. Kaji
10 JR.7 Mh. Jaji Edward Mukandara Kakwezi Rutakangwa

11 JR.8 Mh. Jaji Engera Arnold Kileo

12 JR.9 Mh. Jaji Nathalia Philip Kimaro

13 JR.10 Mh. Jaji Laurean Butulaniza Kelegeya

14 JR.11 Mh. Jaji Mbarouk Salim Mbarouk

..kuna mchangiaji anaweza kutueleza kwanini Majaji wa Mahakama ya Rufaa wameorodheshwa kama # 1,2,5,6..14? kwanini hakuna # 3 na 4?

Kuweka rekodi sawa. JR 6 ni marehemu
 
Ogah, nimekuelewa.
Ubishi huu una undani wake. Kuna watu wanamfanya Mwana Kijiji kuwa punching bag lao au wanafanya mazoezi ya hoja (wako darasani). Nyumba yetu inaungua (TZ), kuhani na Mfumwa wanakazana kuua panya wanaokimbia moto!

Mkuu baija bolobi, "Acha wazee waende vitani, na watoto shule...". Kama huna hoja kaa kimya. "Bendera fata upepo", ukiona kila kitu cha Mwanakijiji unga mkono, manake wewe hutaki kumfanya "punching bag". Kama unasoma majina basi ukikwazo, nakushauri soma "posts" na "udigest" vinavyoandikwa kuliko kukimbilia kuwa kuna undani.

Mimi sina undani ndani ya huu mjadala, NAOMBA UUWEKE WAZI HUO UNDANI unaosababisha UBISHI (wakati huu ni mjadala).
 
Mkuu baija bolobi, "Acha wazee waende vitani, na watoto shule...". Kama huna hoja kaa kimya. "Bendera fata upepo", ukiona kila kitu cha Mwanakijiji unga mkono, manake wewe hutaki kumfanya "punching bag".
======

Halafu unambishi Mwana Kijiji kuwa haupo kwenye mapambano wakati uko vitani kama unavyosema. Umeambiwa nafasi za uteuzi zimeisha au zinakaribia kwisha?
.
 
MKJJ yapasa u grow kimawazo.!!!...kama muungwana, Mfumwa kakuweka sawa juu ya ethics za kuleta habari...!!! next time ukileta habari kuwa makini usikurupuke kama wanavyokurupuka wengine!!!!

Bahati mbaya ingine historia yako na Kuhani, unaona hata ktk mada hii ni mapambano. Umekuwa mtu wa lugha, lkn matumizi yako ya neno "kama" hayakustahili kabisa, otherwise ulikuwa na ajenda yako kichwani...!!!

Bahati mbaya ingine unajijengea tabia kama za mawaziri wa serikali yetu, wanapokosea au kuteleza hawataki kuonekana wamekosea, watataka kuweka lahaja zao nyingi kuonekana hawakukosea. otherwise mijadala kama hii haiwezi kwisha....na ndio maana hata lugha za kuwataka wajiuzulu na wao wanakuwa hawatuelewi...!!!!

Jiunge tu kwenye huo mstari...
 

...Nadhani mjadala huu hauna tija zaidi ya kujadili hoja katika mtazamo finyu na hoja nyepesi.

Huwezi kuwa na mjadala wala hoja wala mitazamo kabla ya kwanza kuwa na facts!

Hatukuwa na facts, tulipotoshwa!

Mjadala ulihusu uzoefu wa mteule, hoja nyingi zikishutumu uteuzi wa jaji ambae ana "kama mwaka mmoja."

Ilipofahamika kwamba hilo si kweli ikawa kama umeme umezimika ghafla kwenye tafrija ya kumshutumu Rais kwa kuteua jaji mwenye mwaka mmoja. Mziki ukazima ghafla, bia hazitoki, shutuma hazitoki, ubwabwa hautoki.

Siku nyingine tuwe na facts kwanza.

Pati imekwisha turudini nyumbani!
 
Mkuu baija bolobi, "Acha wazee waende vitani, na watoto shule...". Kama huna hoja kaa kimya. "Bendera fata upepo", ukiona kila kitu cha Mwanakijiji unga mkono, manake wewe hutaki kumfanya "punching bag".

Mtu hujifunga kwa maneno yake mwenyewe!
 
Back
Top Bottom