Jirani yangu kuna kanisa la walokole

Jirani yangu kuna kanisa la walokole

TUnawashukuru Walokole kwa kumpigia makelele huyo mtu anajiita malaria. Maana nayeye, anatupigia kelele kwa mabandiko yake ya udini hapa. Walokole kazi nimoja hapo, kelele mwa mwi. Mkihitaji maspika makubwa zaidi tutayaleta.
 
Duniani hatuwezi fanana Imani na mitazamo. Huwezi lazimisha wote wawe na dini wala huwezi lazimisha wote wasiwe na dini.
Shuleni ulisoma religious tolerance??
Tutumie akili....
Ndiyo maana dini zibaki mioyoni siyo kuleteana kero au kuziingiza dini kwenye mashule ya elimu dunia au serikalini
 
TUnawashukuru Walokole kwa kumpigia makelele huyo mtu anajiita malaria. Maana nayeye, anatupigia kelele kwa mabandiko yake ya udini hapa. Walokole kazi nimoja hapo, kelele mwa mwi. Mkihitaji maspika makubwa zaidi tutayaleta.
Karibu tutwashtaki mahakamani, jitokeze kuwa wakili wao
 
Nifanyeje?
Usiku na mchana ni kwaya tu, wakati mwengine wanatia kanda na kuwasha maspika ya nje wao wapo majumbani.
Hawana Jumamosi, jumapili au ijumaa , siku zote wao ndio hivyo.
Kuna shule karibu nao wanaipata Pata.
Tufanyeje? Tuhame mpaka shule nayo tuihamishe?
Nenda kwa viongozi wa serikali. Watapewa elimu na kuelekezwa. Watu wanahitaji utulivu kwa nyakati flani. Si sawa kutoa sauti za juu katika mazingira yenye watu kwa saa 24, siku hadi siku, mfululizo. Zaweza kusumbua na kuadhiri afya ya watu wengine wanaohitaji umakini juu ya mambo mengine
 
Aisee na mimi nakaa jirani na msikiti
Wana kispika chao cha mwaka 47 kinapiga kelele balaa mtaa mzima

Maudhi zaidi ni asubuhi kuna lijamaa linaongea kwa vitisho kweli watu wakaswali
Dini yangu ukristo.
Kwa kelele makanisa Yana ongoza kuliko misikiti
 
Hi
Weusi tuna shida...nchi hii ina serikali, kisha Halmashauri, kuna MIPANGO MIJI etc.

Watu wanajitafutia eneo, wanaendeleza kama mchwa tu, huduma za kijamii zinapelekwa, jamaa wanaanza kuchukua kodi za majengo, baada ya miaka 10, wanakuja kusema tunapima maeneo hivyo hivyo ilivyojengwa...miaka 2 inayofuata, wanaanza bomoa bomoa kupitisha road.

Yote hayo ni ndani ya miaka pengine 20, baada ya mwaka 2000. Kipindi ambacho nchi tayari ina umri wa mtu mzima.

Sasa, ilipaswa kuwa, MAENEO YA MAKAZI, kusiwe na Duka, bar, genge, kanisa, msikiti n.k
  • Acha makazi yawe makazi
  • Tenga maeneo ya karibu, tena ikiwezekana opposite na makazi au vyovyote, weka huko biashara zote na majengo ya kiimani.

Hii itasaidia hata kupunguza matuta ya kipumbavu barabarani na vibao vya spidi 50.
- Nyumba huku, duka lipo upande wa pili wa road, bar iko upande mwingine...lazima uweke tuta hapo, kuna mlevi, kuna mtoto anayetumwa kwenda dukani n.k

Tunasubiri tuje tupangiwe na weupe! Sisi tunahamasishana kula kwa urefu wa kamba.
Hiyo akili wanayo Sasa mkuu?.
 
Back
Top Bottom