Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 661
Zawadi yako lazima iwe na uzito na itoke kwa moyo mmoja. Wanaume wengi hutoa zawadi kwa wanawake ili kuomba msamaha au ili apendwe au ili amshawishi mwanamke awe naye kimapenzi, hii hupunguza nguvu ya zawadi. Mwanamke atapokea zawadi yako na kukushukuru. Ili zawadi yako iwe na uzito kwanza inabidi ujue nafasi yako kwa mwanamke na mpo hatua gani katika mahusiano yenu.
Hatua ya kutongoza. Kama bado hamjaanza mahusiano rasmi lakini umeona anaelekea vizuri unaweza ukampigia simu na kuongea naye kumtakia heri ya siku ya valentine. Kisha panga siku mtoke, hauna haja ya kuwaza sana kuhusu zawadi hatua hizi za mwanzo mana utaonekana una haraka au unajipendekeza.
Hatua ya mahusiano machanga. Hapa umpigie simu (kama hampo pamoja) kumtakia heri ya valentine na upange siku mtoke pamoja. Siku mnayokutana mnunulie zawadi ndogo tu ya kumfanya afurahi, nzuri apa ni kadi zenye maneno mazuri ya kufurahisha. Mchombeze kwa maneno mazuri ajisikie wa thamani kwako.
Hatua ya mahusiano yaliyokomaa. Hapa namaanisha upo kwenye mahusiano na mwanamke anakupenda vizuri (sio kimaigizo). Siku ya valentine mtoe out, mfanyie surprise ya zawadi nzuri pia na kadi yenye maneno mazuri itapendeza. Kama mpo mbali, mtumie zawadi au maua au kadi pia hakikisha unampigia (hasa video call). Kwake haya yote maana yake ni kwamba unamkubali kimapenzi na ana umuhimu kwenye maisha yako na wewe una umuhimu kwenye maisha yake (si ni kweli?).
Kama mwanamke amekuacha au amekuchunia. Au mwanamke ambaye haeleweki yani humuelewi elewi. Hatua hii usifanye chochote, hata kama ulikua unampenda kiasi gani lakini kitendo chake kimeshakuambia kuwa we huna umuhimu kwenye maisha yake kwa sasa, ya nini sasa uendelee kujipendekeza? Mwache aende zake.
Ila akikutafuta ongea naye vizuri, mwache yeye ndo akutakie heri ya valentine basi, usianze kuongea ya moyoni kwamba unateseka bila yeye. Pia kama ndo mmejuana, umemkubali lakini hamjuani hata kidogo si vyema kuanza kufikiria zawadi au kumfanya ajisikie wa muhimu sana kwako kabla hata hajajithibitisha kuwa wa muhimu kwako.
Kumbuka unapomtafuta mwanamke siku ya valentine unamaanisha una muwaza na ana umuhimu kwenye maisha yako, hivyo ni muhimu ujue hatua uliyopo na maneno ya kumuambia mwanamke ili kudumisha na kuboresha mahusiano.
Hatua ya kutongoza. Kama bado hamjaanza mahusiano rasmi lakini umeona anaelekea vizuri unaweza ukampigia simu na kuongea naye kumtakia heri ya siku ya valentine. Kisha panga siku mtoke, hauna haja ya kuwaza sana kuhusu zawadi hatua hizi za mwanzo mana utaonekana una haraka au unajipendekeza.
Hatua ya mahusiano machanga. Hapa umpigie simu (kama hampo pamoja) kumtakia heri ya valentine na upange siku mtoke pamoja. Siku mnayokutana mnunulie zawadi ndogo tu ya kumfanya afurahi, nzuri apa ni kadi zenye maneno mazuri ya kufurahisha. Mchombeze kwa maneno mazuri ajisikie wa thamani kwako.
Hatua ya mahusiano yaliyokomaa. Hapa namaanisha upo kwenye mahusiano na mwanamke anakupenda vizuri (sio kimaigizo). Siku ya valentine mtoe out, mfanyie surprise ya zawadi nzuri pia na kadi yenye maneno mazuri itapendeza. Kama mpo mbali, mtumie zawadi au maua au kadi pia hakikisha unampigia (hasa video call). Kwake haya yote maana yake ni kwamba unamkubali kimapenzi na ana umuhimu kwenye maisha yako na wewe una umuhimu kwenye maisha yake (si ni kweli?).
Kama mwanamke amekuacha au amekuchunia. Au mwanamke ambaye haeleweki yani humuelewi elewi. Hatua hii usifanye chochote, hata kama ulikua unampenda kiasi gani lakini kitendo chake kimeshakuambia kuwa we huna umuhimu kwenye maisha yake kwa sasa, ya nini sasa uendelee kujipendekeza? Mwache aende zake.
Ila akikutafuta ongea naye vizuri, mwache yeye ndo akutakie heri ya valentine basi, usianze kuongea ya moyoni kwamba unateseka bila yeye. Pia kama ndo mmejuana, umemkubali lakini hamjuani hata kidogo si vyema kuanza kufikiria zawadi au kumfanya ajisikie wa muhimu sana kwako kabla hata hajajithibitisha kuwa wa muhimu kwako.
Kumbuka unapomtafuta mwanamke siku ya valentine unamaanisha una muwaza na ana umuhimu kwenye maisha yako, hivyo ni muhimu ujue hatua uliyopo na maneno ya kumuambia mwanamke ili kudumisha na kuboresha mahusiano.